Kama nchi tumefeli kwenye Ufunguzi wa African Football League

Umeeleza vizuri, ila kuna mambo ya kuwekana sawa kidogo. Mechi ile ya ufunguzi wala haikuwa ya Simba, ila ilikuwa ya CAF na FIFA, na wao ndiyo waliamua kila kitu kuhusu ile mechi.

Ndiyo maana tunaona mshirika wa FIFA, ambaye ni EA Sport ndiyo aliyepanga kila kitu kuhusu sherehe ya ufunguzi itakavyokuwa na kwa muda upi.

Na hata kazi ya kurekodi mechi ile ilisimamiwa nao wakitumia vifaa vya Azam na kuwakodi watendaji wa Azam. Camera zilipangwa kwa maelekezo yao.

Hata idadi ya camera zilizokuwepo uwanjani iliwekwa kwa matakwa yao. Zilikuwa mara mbili ya ambazo Azam huwa wanatumia kwa kawaida yao. Na alama zote za Azam zilifunikwa.

Hivyo, suala kama la Simba Queen kucheza mechi pale halikuwa na nafasi kwa CAF na FIFA. Hata Simba yenyewe ililazimika hadi kuwanunulia tiketi baadhi ya watu wake ili kuingia uwanjani.

Kwa kuwa kwenye mashindano haya kuna Visit Rwanda na Visit Saudia, moja kwa moja Simba inapoteza haki ya kuvaa jezi ya Visit Tanzania hata kama ingekuwa na mkataba na Simba.

Tanzania imeshawahi kutangaza vivutio vyake CNN, kwenye gazeti la Mirror na hata kwenye EPL kupitia uwanja wa soka wa klabu ya Everton, na juzi tu kwenye Royal Tour.

Haya bado ni mashindano mapya, yana mechi chache bado, nadhani ni sawa pia kujipa muda wa kuona kwanza mrejesho wake kabla na sisi kuweka hela.

Tanzania kama nchi kwa ufunguzi kufanyika Tanzania, imepata faida. FIFA na CAF walitumia hela wakiwa Tanzania, tena siyo hela kidogo. Hivyo, ule uhaba dola unaweza kupoa kidogo kwa sasa.

Ova
 
Ufunguzi wa AFL ulisimamiwa na wenyewe waandaaji wa AFL, mwanzo mpaka mwisho. Tanzania ilikuwa inatwa support tu.
 
Unajua gharama za hayo matangazo lakini au unalaumu tu.
Mm naona tumefanikiwa maana Africa zima inaizungumzia Tanzania kwa sasa..

Ninachoomba serikali itumie hizi fursa za michezo na burudani vizuri sana kuvutia wawekezaji kiuchumi.
Mfano. Serikali inaweza kuwekeza kwenye kumbi za burudani ili tuhost matamasha makubwa mbalimbali.
Pia serikali inaweza kuwezesha miundombinu ya michezo mbalimbali.

Secta ya michezo na burudani ikitendewa haki tutafika mbali sana
 
hiki kitu hata mimi nilikiwaza, mikataba ingewahiwa mwanzo kabisa tungepata display nzuri tu
 
Hivi unajua kwamba yale ni mashindano chini ya uangalizi wa CAF na sio TFF wala Simba?

Unajua kwamba ile haikuwa mechi ya hisani au testimonial match...?
Anajiropokea tu,msameheni.
 
Caf wanamjua ali kiba?
Kwa nn ile nafasi ya alikiba kutumbuiza wasingewapa team za academy
Kwahyo unataka kusema hapo misri alikiba hajulikani?? ..unajua kuwa wimbo aliotumbuiza ali alipangiwa na caf?
 
Kwahyo unataka kusema hapo misri alikiba hajulikani?? ..unajua kuwa wimbo aliotumbuiza ali alipangiwa na caf?
Acha uongo Caf na FIFA wanaijua sumu aliambiwa asi perform nyimbo inayohusiana na team yoyote katika zile mbili ila hakuambiwa nyimbo ya ku perform tumia akili kidogo.
 
Anajiropokea tu,msameheni.
Nyinyi ndio mnadandia gari kwa mbele unasoma tu title ya thread halafu una type utopolo ungesoma nilichoandika chote sidhani kama ungeandika hizo pumba zako.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…