Thanks...Ila Beno kamwe hawezi kurudi Yanga...inavyoonekana meneja wake ambaye ni kiongozi wa Simba alikula njama na wanasimba wenzake kuhakikisha Yanga inahujumiwa ...Kwa hiyo huyo meneja atalazimika kumtafutia timu huyo anayeitwa Beno..na ni vema asajiliwe Simba, ila kwa Yanga hawezi kurudi tena...Yanga wana msimamo..mamluki hawatakiwi kabisa ndani ya Yanga...Na kwa kusema ukweli huo ndiyo mwisho wa soka ya Beno...hakuna mchezaji aliyewahi kuisaliti Yanga na akaendelea kuwika huko aendako...Hovyo kabisa huyo Beno...alijua kuwa yeye ni mtu mhimu ndani ya kikosi kutokana na alivyodaka siku ya mechi ya dhidi ya Simba..magazeti yakampamba na akavimbishwa kichwa..ma-simba yakaona kuwa huo ndio ulikuwa wakati wa kuihujumu Yanga kwa hiyo wakamshawishi aisaliti timu...awaulize akina Munishi, Niyonzima na Bartez...Munishi au Dida sasa anashindwa kudaka hata mpira uliopigwa mita 30...huyo Bartez toka alivyofungwa goli la 'kinamna' la Kichuya la mpira wa kona, ndiyo basi tena...huyo Niyonzima akairingia Yanga pamoja na ukweli ilimsaidia mno pamoja na mmoja wa wazazi wake, akaenda Simba sasa huko anakula wa 'chuya'...list ya walioisaliti Yanga na wakaharibikiwa ni wengi...