Kama ndo ukweli huu! Siungi mkono Beno kurejea Jangwani maana alimdharau Kocha

Kama ndo ukweli huu! Siungi mkono Beno kurejea Jangwani maana alimdharau Kocha

Mpira ni ajira na siyo kufanya hisani,utachezaje wakati familia inalala njaa....
Aangalie future yake,pale jangwani njaa na longolongo mob

Sent using Jamii Forums mobile app
Alichokosea Benno ni kutaka kurudi tena mahali waliposhindwa kumlipa mshahara. Nilitegemea wakati huu atakuwa kwenye mahakama za michezo akisaka haki zake. Yanga haina pesa kwa sasa ana uhakika gani kwamba wakati huu atalipwa.
 
BENNO KAKOLANYA SIMAMA WEWE MWENYEWE.

Mambo yaliharibika zaidi mara baada ya kuondoka George Lwandamina, timu ikawa chini ya Noel Mwandila akisaidiwa na Shadrack Nsajigwa 'Fusso' . . wachezaji kugoma ikawa kawaida, hadi anawasili Mwinyi Zahera hiyo tabia iliendelea! Yanga SC ikawa ina unga unga kikosi, si unakumbuka ile safari ya Algeria kucheza na USM Alger? timu ilipowasili JKNIA kocha wetu alishangazwa sana na jinsi timu inavoenda kienyeji licha ya kuwa Yanga ni timu kubwa.

Baada ya michuano ya SportPesa kule Kenya kumalizika ndipo kwa mara ya kwanza Mwinyi Zahera aliwaita wachezaji wake , namnukuu

"Hii ni kazi na mnapaswa kuiheshimu, mnafahamu fika timu haina hela nataka tukubaliane kama huwezi kucheza bila kulipwa pesa yako basi naomba mapema kabisa nikuruhusu uondoke, ninyi mliomaliza mikataba yenu na bado mnatamani kuendelea hapa ningewashauri nyie sinyeni Yanga hela yenu mtaipata tu japo yawezekana isiwe leo ama kesho "

Baada ya hapo Mwalimu akawapa muda wachezaji wa kufikiri na kwenda kushauriana na watu wao wa karibu, Wachezaji wote waliridhia kuwa wapo tayari kuipigania Yanga licha ya changamoto za kipesa ndipo wengine wakasaini hata bila signing fees! Hapo ndipo Yanga ikawa kitu kimoja pasipo kuangalia sana maslahi ya kifedha, ukiwa na shida ya kipesa unamweleza mwalimu naye anatoa pesa yake na kukupatia, furaha ikarudi na umoja ukajengeka siku hadi siku.

Usiku wa kuamkia tarehe 4 November, 2018 majira ya saa 7 usiku timu ikiwa hotelini kocha mkuu akagongewa mlango na meneja wa timu! hata kabla ya kufungua kocha akasikia " Kocha, Kocha Benno anaondoka" . . . Zahera akafungua mlango haraka kisha akawaambia naomba mwiteni Benno, muwahini haraka! ndipo Benno akarudi na kukaa chumbani kwa kocha kwa maongezi.

"Benno kulikoni unataka kuondoka? tumefanya kikao saa 5 usiku kama una tatizo si ungenambia muda ule iweje usubiri tukiwa tumelala ndipo utoroke? kumbuka kama timu tulikubaliana kuwa tupo tayari kufanya kazi licha ya ukata, iweje utusaliti na unajua fika kesho tuna mechi ngumu dhidi ya Ndanda. . nakuomba baki hapa kama una shida sana tutaongea naomba tufocus kwa mchezo wa ujao kwanza" , Benno aliendelea kushikilia msimamo wake kuwa anaondoka, kuangalia nje kumbe tayari meneja wake amekuja kumchukua.

Simu za viongozi wala kocha akawa hapokei, baada ya wiki meneja wake akajitokeza kuwa anaupa uongozi wa Yanga siku 3 uwe umemlipa mteja wake la sivyo Benno atakuwa mchezaji huru! Siku tatu zikapita kisha wiki ikakatika ndipo Benno kwa kushirikiana na meneja wake wakawasilisha barua ya kuvunja mkataba Yanga SC.

Ghafla mbele ya waandishi wa habari , Benno akakabidhiwa milioni 2 kutoka kwa Cyprian Msiba kisha akaahidi sasa atarejea kambini kuitumikia Yanga ndipo akaonana na rungu zito la Zahera.

Mpaka hapo utaweza kugundua kwanini Mwinyi Zahera anagoma kumrudisha kikosini japo moyoni mwake anatamani sana kuwa na golikipa kama Benno kikosini mwake ila anatambua hasara ya kumpokea ni kubwa kuliko kumkataa, ukizingatia yeye ndiye aliyebeba maono ya timu! vijana wote ambao hawajalipwa lakini maslahi yao wameweka kando nao wanaufuatilia huu mchezo!

USHAURI WANGU!
Mwinyi Zahera ni muwakilishi wa hisia za kikosi chake, Kamwe Benno asitegemee msamaha binafsi kutoka kwa Zahera! Benno amewakosea na kuwasaliti wachezaji wenzie, Benchi la ufundi, viongozi na mashabiki wa Yanga SC! anachopaswa kufanya ajitokeze yeye binafsi na kulisimamia hili swala liishe aache kusemewa, aambatane na ndugu yake wa karibu wakawaombe msamaha wachezaji huko ndipo msamaha wake utaweza kupatikana sio kwa Zahera, wachezaji wakimsamehe kwa dhati wao ndio wataongea na mwalimu! kwa jinsi Zahera anavoishi na wanaye msitegemee akawa mwamuzi katika hili.

Hili jambo sio dogo kama mdhaniavyo, likichukuliwa kirahisi laweza kuleta mpasuko katika kikosi chetu na kuharibu heshima aliyojijengea mwalimu wetu, Benno acha kujiona star na kuamini nguvu ya mashabiki ndio itakayokurejesha kikosini! Omba msamaha wewe binafsi , kwa dhati kabisa watafute wachezaji, benchi la ufundi waombe msamaha amini nakwambia hao ndio wana password za kureset msimamo wa Zahera.

Copy and paste from Mr. Hissan Salum Iddi

Thanks...Ila Beno kamwe hawezi kurudi Yanga...inavyoonekana meneja wake ambaye ni kiongozi wa Simba alikula njama na wanasimba wenzake kuhakikisha Yanga inahujumiwa ...Kwa hiyo huyo meneja atalazimika kumtafutia timu huyo anayeitwa Beno..na ni vema asajiliwe Simba, ila kwa Yanga hawezi kurudi tena...Yanga wana msimamo..mamluki hawatakiwi kabisa ndani ya Yanga...Na kwa kusema ukweli huo ndiyo mwisho wa soka ya Beno...hakuna mchezaji aliyewahi kuisaliti Yanga na akaendelea kuwika huko aendako...Hovyo kabisa huyo Beno...alijua kuwa yeye ni mtu mhimu ndani ya kikosi kutokana na alivyodaka siku ya mechi ya dhidi ya Simba..magazeti yakampamba na akavimbishwa kichwa..ma-simba yakaona kuwa huo ndio ulikuwa wakati wa kuihujumu Yanga kwa hiyo wakamshawishi aisaliti timu...awaulize akina Munishi, Niyonzima na Bartez...Munishi au Dida sasa anashindwa kudaka hata mpira uliopigwa mita 30...huyo Bartez toka alivyofungwa goli la 'kinamna' la Kichuya la mpira wa kona, ndiyo basi tena...huyo Niyonzima akairingia Yanga pamoja na ukweli ilimsaidia mno pamoja na mmoja wa wazazi wake, akaenda Simba sasa huko anakula wa 'chuya'...list ya walioisaliti Yanga na wakaharibikiwa ni wengi...
 
Thanks...Ila Beno kamwe hawezi kurudi Yanga...inavyoonekana meneja wake ambaye ni kiongozi wa Simba alikula njama na wanasimba wenzake kuhakikisha Yanga inahujumiwa ...Kwa hiyo huyo meneja atalazimika kumtafutia timu huyo anayeitwa Beno..na ni vema asajiliwe Simba, ila kwa Yanga hawezi kurudi tena...Yanga wana msimamo..mamluki hawatakiwi kabisa ndani ya Yanga...Na kwa kusema ukweli huo ndiyo mwisho wa soka ya Beno...hakuna mchezaji aliyewahi kuisaliti Yanga na akaendelea kuwika huko aendako...Hovyo kabisa huyo Beno...alijua kuwa yeye ni mtu mhimu ndani ya kikosi kutokana na alivyodaka siku ya mechi ya dhidi ya Simba..magazeti yakampamba na akavimbishwa kichwa..ma-simba yakaona kuwa huo ndio ulikuwa wakati wa kuihujumu Yanga kwa hiyo wakamshawishi aisaliti timu...awaulize akina Munishi, Niyonzima na Bartez...Munishi au Dida sasa anashindwa kudaka hata mpira uliopigwa mita 30...huyo Bartez toka alivyofungwa goli la 'kinamna' la Kichuya la mpira wa kona, ndiyo basi tena...huyo Niyonzima akairingia Yanga pamoja na ukweli ilimsaidia mno pamoja na mmoja wa wazazi wake, akaenda Simba sasa huko anakula wa 'chuya'...list ya walioisaliti Yanga na wakaharibikiwa ni wengi...
National team asahau kucheza tena labda kocha atangaziwe kikosi na tff,na Simba wenyewe waliomshawishi wanaweza kumuacha mitaani, maana wabongo huwa wanafanya mambo kwa maslahi yao tu
 
hivi umeshawaona wale wachezaji wa zamani waliocheza mpira kwa mapenzi hali zao zikoje, Benno kachagua mpira kuwa ajira yake na nyinyi mnatakiwa kumlipa sio kuanza kukoroma wakati pesa hamna.Hivi hapa nani anaweza kufanya kazi bila kulipwa hao watumishi wa serikali ikifika tarehe 25 mshahara haujatoka utaona post kibao za kulaumu serikali lakini nyie mnamshutumu bila kujua huyu mtu ana majukumu yake na familia yake nyinyi mnaomshutumu ndio nyinyi ambao mtamcheka baadae wakati amefulia mnyonge mnyongeni haki yake mpeni
 
Maslahi ya Mchezaji ni miongoni mwa vipengele muhimu kwenye mkataba, endapo mchezaji hajatimiziwa matakwa yake kimkataba ilaumiwe klabu si mchezaji kama mnavupmzodoa Benno. Punguzeni mahaba mjaddili bila kuegemea popote.
 
Kwanza atumtKi tena hana ata shukrani.....

Alikua majeruhi msimu mzima akatibiwa na team na kupewa mshahara, watu walimvumilia yeye kuvumilia kashindwa? Inaonyesha alitaman sana team ifungwe ili umuhimu wake uonekane......!

Sent using Jamii Forums mobile app
Kweli kabisa mkuu
 
  • Thanks
Reactions: Oxx
Maslahi ya Mchezaji ni miongoni mwa vipengele muhimu kwenye mkataba, endapo mchezaji hajatimiziwa matakwa yake kimkataba ilaumiwe klabu si mchezaji kama mnavupmzodoa Benno. Punguzeni mahaba mjaddili bila kuegemea popote.
Usidhani kila mafanikio hayana changamoto mkuu,ni karibia timu nzima inamadai na kocha alishakaa nao na kuwapa msimamo wao,why hakuondoka pale? Kwasoka la Bongo atastrugle sana
 
hivi umeshawaona wale wachezaji wa zamani waliocheza mpira kwa mapenzi hali zao zikoje, Benno kachagua mpira kuwa ajira yake na nyinyi mnatakiwa kumlipa sio kuanza kukoroma wakati pesa hamna.Hivi hapa nani anaweza kufanya kazi bila kulipwa hao watumishi wa serikali ikifika tarehe 25 mshahara haujatoka utaona post kibao za kulaumu serikali lakini nyie mnamshutumu bila kujua huyu mtu ana majukumu yake na familia yake nyinyi mnaomshutumu ndio nyinyi ambao mtamcheka baadae wakati amefulia mnyonge mnyongeni haki yake mpeni
Yanga haiwezi kumlipa na alishaondoka sasa anarudi wapi?
 
Kwa wale wote wanaomuunga mkono kwa dhati Beno, naomba wabaki na muono wao huo mioyoni mwao. Kumlishia Beni msimamo huo ni kumpotosha. Kweli mpira ni ajira, kweli anastahili kulipwa, kweli si vyema familia kulala njaa huku anadai mshiko wake. Lakini msimamo wa kugoma na hatimaye kususiwa ni kujaribu hatimaye yake pana inayomsubiri kwa kutetea sasa yake finyu. Asidhani hao akina Christiano, Samatta, Messi na wengine wanaovuna mamilioni hivi sasa kuwa wanachopata ni mavuno ya juhudi zao pekee. Wanachopata ni mavuno ya kustahamili adha na karaha nyingi za ndani na nje ya uwanja, pengine kubwa kuliko hata hizo za Beno kutolipwa fedha yake; angalau posho la kila mechi alikuwa anapata, angalau alikuwa na mwalimu aliyetambua shida zake na akawa tayari kumsaidia, angalau adha hizo anazipata akiwa nchini kwao, angalau muda wote huo familia yake iko pamoja naye, angalau kuna wenye akili kama zake wanaomchochea na kumuunga mkono. Pitia maisha ya wachezaji kama akina Adebayor, Lukaku, Ronaldo Gaucho (Ronaldinho) na wachezaji wengi hasa wa Kiafrika wanaocheza soka la kulipwa Ulaya na utabaini kumbe hii inayoitwa adha ya Kakolanya si chochote.
Naomba tuwape moyo na Ushauri vijana wetu hawa ili vipawa vyao viwatumikie wao na sisi leo na kesho badala ya kuwaharibu kwa miono a kishabiki ambayo itaishia kutukosesha matunda ya vipawa hivyo sisi kama Taifa lakini zaidi wao kushindwa kunufaika na matunda mengi ya jasho lao jingi kwa kuendekeza kidogo wanachokosa hivi sasa.
Anayejua annajua tu,ndio maana utumwa hauishi duniani.Wasomi mnajadili kama vichaa,Benno hakuzaliwa na yanga ana haki kukipigania kipaji na haki yake kwa ngivu zote.Atachezea timu zingine au hata akifa masikini kuliko kuwatumikia hao wachumia tumbo wa yanga.Siungi mkono hoja ya kubembeleza masikini.Na mkuu ukitaka kujua watanzania sisi wapuuzi subiri tetesi zitoke anaenda simba uone.Hakuna tunalolijua.
 
hivi umeshawaona wale wachezaji wa zamani waliocheza mpira kwa mapenzi hali zao zikoje, Benno kachagua mpira kuwa ajira yake na nyinyi mnatakiwa kumlipa sio kuanza kukoroma wakati pesa hamna.Hivi hapa nani anaweza kufanya kazi bila kulipwa hao watumishi wa serikali ikifika tarehe 25 mshahara haujatoka utaona post kibao za kulaumu serikali lakini nyie mnamshutumu bila kujua huyu mtu ana majukumu yake na familia yake nyinyi mnaomshutumu ndio nyinyi ambao mtamcheka baadae wakati amefulia mnyonge mnyongeni haki yake mpeni
Mkuu kilichopo wachezaji wa Yanga wamekubali kuishi nje ya utaratibu( wamekubali kucheza bila maslahi). Beno yeye kwa vile anategemea mpira na hawezi tena kusubiti kupata maslahi yake hakutakiwa kugeuka nyuma tangu siku alipojiengua kambini. Yanga haijamnyima Beno haki yake isipokuwa hali ni ngumu ndani ya klabu. Beno alichotakiwa kufanya ni kwenda mbele zaidi kudai haki yake hadi kieleweke. Unaporudi tena mahali uliposaliti harakati za wenzako tukuelewe vipi? Ndio kudai haki kwenyewe ndio huko?!
 
Thanks...Ila Beno kamwe hawezi kurudi Yanga...inavyoonekana meneja wake ambaye ni kiongozi wa Simba alikula njama na wanasimba wenzake kuhakikisha Yanga inahujumiwa ...Kwa hiyo huyo meneja atalazimika kumtafutia timu huyo anayeitwa Beno..na ni vema asajiliwe Simba, ila kwa Yanga hawezi kurudi tena...Yanga wana msimamo..mamluki hawatakiwi kabisa ndani ya Yanga...Na kwa kusema ukweli huo ndiyo mwisho wa soka ya Beno...hakuna mchezaji aliyewahi kuisaliti Yanga na akaendelea kuwika huko aendako...Hovyo kabisa huyo Beno...alijua kuwa yeye ni mtu mhimu ndani ya kikosi kutokana na alivyodaka siku ya mechi ya dhidi ya Simba..magazeti yakampamba na akavimbishwa kichwa..ma-simba yakaona kuwa huo ndio ulikuwa wakati wa kuihujumu Yanga kwa hiyo wakamshawishi aisaliti timu...awaulize akina Munishi, Niyonzima na Bartez...Munishi au Dida sasa anashindwa kudaka hata mpira uliopigwa mita 30...huyo Bartez toka alivyofungwa goli la 'kinamna' la Kichuya la mpira wa kona, ndiyo basi tena...huyo Niyonzima akairingia Yanga pamoja na ukweli ilimsaidia mno pamoja na mmoja wa wazazi wake, akaenda Simba sasa huko anakula wa 'chuya'...list ya walioisaliti Yanga na wakaharibikiwa ni wengi...
Kwa hiyo ninyi huwa mnawaroga wanaowasaliti.
 
Kwanza atumtKi tena hana ata shukrani.....

Alikua majeruhi msimu mzima akatibiwa na team na kupewa mshahara, watu walimvumilia yeye kuvumilia kashindwa? Inaonyesha alitaman sana team ifungwe ili umuhimu wake uonekane......!

Sent using Jamii Forums mobile app
Kawe wewe kipa uzibe pengo lake acheni haki zake.mbona wewe hukua kipa.
 
BENNO KAKOLANYA SIMAMA WEWE MWENYEWE.

Mambo yaliharibika zaidi mara baada ya kuondoka George Lwandamina, timu ikawa chini ya Noel Mwandila akisaidiwa na Shadrack Nsajigwa 'Fusso' . . wachezaji kugoma ikawa kawaida, hadi anawasili Mwinyi Zahera hiyo tabia iliendelea! Yanga SC ikawa ina unga unga kikosi, si unakumbuka ile safari ya Algeria kucheza na USM Alger? timu ilipowasili JKNIA kocha wetu alishangazwa sana na jinsi timu inavoenda kienyeji licha ya kuwa Yanga ni timu kubwa.

Baada ya michuano ya SportPesa kule Kenya kumalizika ndipo kwa mara ya kwanza Mwinyi Zahera aliwaita wachezaji wake , namnukuu

"Hii ni kazi na mnapaswa kuiheshimu, mnafahamu fika timu haina hela nataka tukubaliane kama huwezi kucheza bila kulipwa pesa yako basi naomba mapema kabisa nikuruhusu uondoke, ninyi mliomaliza mikataba yenu na bado mnatamani kuendelea hapa ningewashauri nyie sinyeni Yanga hela yenu mtaipata tu japo yawezekana isiwe leo ama kesho "

Baada ya hapo Mwalimu akawapa muda wachezaji wa kufikiri na kwenda kushauriana na watu wao wa karibu, Wachezaji wote waliridhia kuwa wapo tayari kuipigania Yanga licha ya changamoto za kipesa ndipo wengine wakasaini hata bila signing fees! Hapo ndipo Yanga ikawa kitu kimoja pasipo kuangalia sana maslahi ya kifedha, ukiwa na shida ya kipesa unamweleza mwalimu naye anatoa pesa yake na kukupatia, furaha ikarudi na umoja ukajengeka siku hadi siku.

Usiku wa kuamkia tarehe 4 November, 2018 majira ya saa 7 usiku timu ikiwa hotelini kocha mkuu akagongewa mlango na meneja wa timu! hata kabla ya kufungua kocha akasikia " Kocha, Kocha Benno anaondoka" . . . Zahera akafungua mlango haraka kisha akawaambia naomba mwiteni Benno, muwahini haraka! ndipo Benno akarudi na kukaa chumbani kwa kocha kwa maongezi.

"Benno kulikoni unataka kuondoka? tumefanya kikao saa 5 usiku kama una tatizo si ungenambia muda ule iweje usubiri tukiwa tumelala ndipo utoroke? kumbuka kama timu tulikubaliana kuwa tupo tayari kufanya kazi licha ya ukata, iweje utusaliti na unajua fika kesho tuna mechi ngumu dhidi ya Ndanda. . nakuomba baki hapa kama una shida sana tutaongea naomba tufocus kwa mchezo wa ujao kwanza" , Benno aliendelea kushikilia msimamo wake kuwa anaondoka, kuangalia nje kumbe tayari meneja wake amekuja kumchukua.

Simu za viongozi wala kocha akawa hapokei, baada ya wiki meneja wake akajitokeza kuwa anaupa uongozi wa Yanga siku 3 uwe umemlipa mteja wake la sivyo Benno atakuwa mchezaji huru! Siku tatu zikapita kisha wiki ikakatika ndipo Benno kwa kushirikiana na meneja wake wakawasilisha barua ya kuvunja mkataba Yanga SC.

Ghafla mbele ya waandishi wa habari , Benno akakabidhiwa milioni 2 kutoka kwa Cyprian Msiba kisha akaahidi sasa atarejea kambini kuitumikia Yanga ndipo akaonana na rungu zito la Zahera.

Mpaka hapo utaweza kugundua kwanini Mwinyi Zahera anagoma kumrudisha kikosini japo moyoni mwake anatamani sana kuwa na golikipa kama Benno kikosini mwake ila anatambua hasara ya kumpokea ni kubwa kuliko kumkataa, ukizingatia yeye ndiye aliyebeba maono ya timu! vijana wote ambao hawajalipwa lakini maslahi yao wameweka kando nao wanaufuatilia huu mchezo!

USHAURI WANGU!
Mwinyi Zahera ni muwakilishi wa hisia za kikosi chake, Kamwe Benno asitegemee msamaha binafsi kutoka kwa Zahera! Benno amewakosea na kuwasaliti wachezaji wenzie, Benchi la ufundi, viongozi na mashabiki wa Yanga SC! anachopaswa kufanya ajitokeze yeye binafsi na kulisimamia hili swala liishe aache kusemewa, aambatane na ndugu yake wa karibu wakawaombe msamaha wachezaji huko ndipo msamaha wake utaweza kupatikana sio kwa Zahera, wachezaji wakimsamehe kwa dhati wao ndio wataongea na mwalimu! kwa jinsi Zahera anavoishi na wanaye msitegemee akawa mwamuzi katika hili.

Hili jambo sio dogo kama mdhaniavyo, likichukuliwa kirahisi laweza kuleta mpasuko katika kikosi chetu na kuharibu heshima aliyojijengea mwalimu wetu, Benno acha kujiona star na kuamini nguvu ya mashabiki ndio itakayokurejesha kikosini! Omba msamaha wewe binafsi , kwa dhati kabisa watafute wachezaji, benchi la ufundi waombe msamaha amini nakwambia hao ndio wana password za kureset msimamo wa Zahera.

Copy and paste from Mr. Hissan Salum Iddi
Umesahahau mkuu kuweka wazi, kwamba Meneja wake aliyemtoa kambini pia ni kiongozi wa mikia a.k.a vibonde wa Mashujaa



Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom