Kama ndo ukweli huu! Siungi mkono Beno kurejea Jangwani maana alimdharau Kocha

Kama ndo ukweli huu! Siungi mkono Beno kurejea Jangwani maana alimdharau Kocha

Nlichogundua wengi humu mnachangia kwa kuongozwa na ushabiki usio na tija..... Yaani kwa kuwa mna mahaba na timu basi mko tayari kusimama nayo hata wakikosea mkidhani mnasaidia.... Mkataba mnaposaini unaweka majukumu ya pande zote mbili za klabu na mchezaji.... Yeye mchezaji ni kucheza mpira na timu ni kumpa stahiki zake sasa Yanga inapokiuka clause za mkataba inakuaje benno aonekane mbaya ilihali mchezaji akitoroka kambi au akichelewa mazoezini naye huwa amekiuka mkataba na huwa anaadhibiwa licha ya kuwa na sababi za msingi sasa kwanini mnaangalia upande mmoja??

Mtu hajalipwa pesa yake na ana matatizo mlitaka afanyeje?? Ana madeni mlitaka afanyeje?? Kwanini timu isikope imlipe??

Shida watu humu mnaongozwa na mahaba ndio maana mpira wa Tanzania haukuwi.... No wonder hakuna timu ya bongo imewahi fanya vzuri kimataifa maana mmejaa uswahili sana na ubabaishaji na washabiki wenyewe ndio wanafiki hivi hatutofika kokote.
Nahisi unahisi watu wote wako na ushabiki maandazi kwa sababu tu na wewe ndivyo ulivyo. Si kila ulivyo wewe ndivyo walivyo wengine. Hebu fuatilia mtiririko wa hoja zangu kwanza halafu unioneshe wapi nimesema Beno ni mbaya. Fuatilia mtiririko wa hoja zangu kama hutaona f nimetamka bila kugegeza kwamba si vyema mchezaji kukutwa na yaliyomkuta Beno. Kama umefuatilia kwa makini hoja zangu utabaini kwamba nimesisitiza Beno na kama yeye asaidiwe kujua namna ya kukabiliana na hali kama hiyo, vinginevyo anaweza kukosa kuvuna matunda ya kipaji chake naTaifa - siyo Yanga unayolazimisha kuwa ndiyo ninayoitetea - litakosa faida ya kipaji chake. Badala ya kukaa na kulaumu Utanzania na Uswahili kuwa ndiyo sumu ya mpira wetu, unaonaje ukaamua kuanza kubadilika wewe kwa kutaka kufahamu hoja kabla ya kuidandia? Kwa sababu naamini wewe tangu mwanzo unauchukuia na kuukataa Utanzania na Uswahili. Siamini kwamba kauli yako hiyo dhidi ya Uswahili na Utanzania imetokana na hoja yangu. Kwa sababu mimi kama ni Mtanzania au Mswahili basi ni mmoja tu. Hao wengine umewapata wapi wanaotosheleza kuharibu mpira wa Tanzania, kama tangu mwanzo hukuwa na mtizamo huo mbaya dhidi ya Watanzania na Waswahili?
 
kila siky huwa nasema Simba na Yanga zinaongozwa na watu ambao typically ni wahuni wa mjini.sishangai kwa haya tunayoyaona
 
Kwahiyo mtu asidai haki zake kisa atakosa maslahi fulani ya muda mrefu?? Kubalini kwamba yanga ilikosea kuahidi kumlipa ilihali haina pesa sio mnamdhulumu mtu na pesa zake hamumpi.... Trust me akienda FIFA kama yule mkenya wa Yanga enzi hizo aliyewalipisha million 40 ndio mtaelewa kwamba dawa ya Deni ni kulipa sio kelele kelele na uswahili.

Nikuulize swali hivi mchezaji asipofuata mkataba mngemtetea hivi?? Kwanini timu isipofuata mnawatetea?? Hizi double standards zitawapeleka wapi??

Mwingine anakuja na hoja eti wengine hawadai?? Kwahiyo kwa kuwa wengine wamekubali kutapeliwa basi inajustify beno kutapeliwa pia??

Tubadilike kama tunataka kusaidia mpira wetu ukue otherwise tutaendelea kuwa wasindikizaji tu
Je wote wanaodai wangegoma timu si ingeshuka daraja,wewe hudai? Wewe hudaiwi? Kudaiwa ni utapeli?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nahisi unahisi watu wote wako na ushabiki maandazi kwa sababu tu na wewe ndivyo ulivyo. Si kila ulivyo wewe ndivyo walivyo wengine. Hebu fuatilia mtiririko wa hoja zangu kwanza halafu unioneshe wapi nimesema Beno ni mbaya. Fuatilia mtiririko wa hoja zangu kama hutaona f nimetamka bila kugegeza kwamba si vyema mchezaji kukutwa na yaliyomkuta Beno. Kama umefuatilia kwa makini hoja zangu utabaini kwamba nimesisitiza Beno na kama yeye asaidiwe kujua namna ya kukabiliana na hali kama hiyo, vinginevyo anaweza kukosa kuvuna matunda ya kipaji chake naTaifa - siyo Yanga unayolazimisha kuwa ndiyo ninayoitetea - litakosa faida ya kipaji chake. Badala ya kukaa na kulaumu Utanzania na Uswahili kuwa ndiyo sumu ya mpira wetu, unaonaje ukaamua kuanza kubadilika wewe kwa kutaka kufahamu hoja kabla ya kuidandia? Kwa sababu naamini wewe tangu mwanzo unauchukuia na kuukataa Utanzania na Uswahili. Siamini kwamba kauli yako hiyo dhidi ya Uswahili na Utanzania imetokana na hoja yangu. Kwa sababu mimi kama ni Mtanzania au Mswahili basi ni mmoja tu. Hao wengine umewapata wapi wanaotosheleza kuharibu mpira wa Tanzania, kama tangu mwanzo hukuwa na mtizamo huo mbaya dhidi ya Watanzania na Waswahili?
Mkuu nafkiri sentensi ya kwanza inaonyesha kuwa najibu collectively hoja zenu humu na sio yako specifically. Sababu wewe binafsi sijaona ukizungumzia kabisa suala la wajibu wa mkataba unakimbilia kushauri subjectively bila kuangalia upande wa mkataba kisheria unasemaje..... Nilitegemea wwe uwe mstari wa mbele kumshauri awashtaki Yanga FIFA alipwe pesa zake kwa kukiuka mkataba we unashauri avumilie kucheza bila kulipwa kama kina Adebayor?? Ilihali muda huo kuna viongozi wa Yanga wananufaika na pesa za timu na kufuja??

Inachopaswa ni washabiki wote kuwaambia Yanga waombe radhi na wamlipe hela zake maana ndio wajibu wao kwenye mkataba ila contrary naona mnataka ashauriwe vizuri na sio kusimamia msimamo wa sasa??
Mbaya zaidi kuna mwingine anashauri eti Benno ndio aombe radhi kisa kudai haki zake!! Hivi hatujui kama mtu amekiuka mkataba una haki ya kuvunja mkataba?? Yaani mambo ya kisheria mnataka muingizie busara cjui ujuaji mwingi wakati wanasaini mkataba Benno alipewa Masharti kibao ambayo naye angekiuka angetimuliwa ila sioni humu mtu akisema Benno kacheza nafasi yake wote ni lawama tu hivi mpira wetu utafika kokote??

Hakuna kuzunguka wote kwa sauti mmoja inatakiwa tumsupport beno sio kuingiza maoni yetu wakati yye anaumia na njaa it ain't fair kabisa
 
Je wote wanaodai wangegoma timu si ingeshuka daraja,wewe hudai? Wewe hudaiwi? Kudaiwa ni utapeli?

Sent using Jamii Forums mobile app
Mkuu Timu lazima ionyeshe juhudi za kujali wachezaji mfano Borussia Dortmund iliwahi kukaribia kufilisika hata mishahara ya wachezaji ikakaribia kukauka walichofanya walienda kusaidiwa na mahasimu wao Bayern Munich na leo hii ipo vzuri kiuchumi mbona sijaona effort yeyote ya Yanga kulipa hayo madeni?? Klabu ni wachezaji sio majengo ni heri wauze hata assets za timu pesa ipatikani iwalipe wachezaji otherwise ni haki kabisa timu nzima ikigoma maana kisheria mikataba yao imekiukwa na hata wakienda FIFA wanashinda kesi

Let's be realistic guys.... Hata leeds ilipofulia iliuza mastaa wake wote ikaanza upyaa kama Yanga nao hawana pesa si iuze timu nzima iwalipe madeni yao ianze na wachezaji wa ACADEMY?? Kigumu kipi?? Yaani timu haina hela ila inataka ijaze mastaa..... Mkishindwa mnataka wachezaji ndio wateseke

Kwa staili hii mpira wetu huendi kokote
 
Mkuu zito hii nchi watu hawajui mpira ni ushabiki maandazi tu.
 
Beno yupo sahihi hta mbwa wako uliemfuga kama haumpi chakula lzma atakutoroka, na msimu wa kupeleka watoto shule ndio huu, vyura fc hatuwachangii

Sent using Jamii Forums mobile app
 
mpeni hela zake acheni kutafuta vichaka vya kuwanyima haki wachezaji wenu

Sent using Jamii Forums mobile app
Ndugu yangu Yawezekana uko sahihi kwa kile unachosema. Lakini napenda nikueleze kitu kimoja ambacho wachezaji wengi wa mpira wa miguu wa Afrika Mashariki hawana. Kitu hicho ni uthubutu, kujituma kwa kutoa damu na jasho jingi wakati wa kutafuta mafanikio. Ukisikia simulizi za wachezaji wa Afrika Magharibi waliofanikiwa Ulaya utachoka. Wamepitia Changamoto nyingi sana hata kulala na njaa wakati wakitafuta mafanikio. Lakini leo hii Ulaya nzima imejaa wachezaji wa Afrika Magharibi. Wachezaji kutoka Afrika Mashariki ni kuwahesabu kama McDonald Maliga, Wanyama na Mbwana Samata. Tukubaliane huwezi kufanya kazi bila mshahara lakini inabidi uangalie na mwenendo wa kiuchumi wa firm/company unayofanyia kazi. Hapo ndio kuna kitu kinaitwa kugeuza Changamoto (challenge) kuwa fursa (opportunity). Zaidi jaribu kusoma historia ya mchezaji mmoja anaitwa C. Tiote nina imani utatoa machozi.
 
Mkuu nafkiri sentensi ya kwanza inaonyesha kuwa najibu collectively hoja zenu humu na sio yako specifically. Sababu wewe binafsi sijaona ukizungumzia kabisa suala la wajibu wa mkataba unakimbilia kushauri subjectively bila kuangalia upande wa mkataba kisheria unasemaje..... Nilitegemea wwe uwe mstari wa mbele kumshauri awashtaki Yanga FIFA alipwe pesa zake kwa kukiuka mkataba we unashauri avumilie kucheza bila kulipwa kama kina Adebayor?? Ilihali muda huo kuna viongozi wa Yanga wananufaika na pesa za timu na kufuja??

Inachopaswa ni washabiki wote kuwaambia Yanga waombe radhi na wamlipe hela zake maana ndio wajibu wao kwenye mkataba ila contrary naona mnataka ashauriwe vizuri na sio kusimamia msimamo wa sasa??
Mbaya zaidi kuna mwingine anashauri eti Benno ndio aombe radhi kisa kudai haki zake!! Hivi hatujui kama mtu amekiuka mkataba una haki ya kuvunja mkataba?? Yaani mambo ya kisheria mnataka muingizie busara cjui ujuaji mwingi wakati wanasaini mkataba Benno alipewa Masharti kibao ambayo naye angekiuka angetimuliwa ila sioni humu mtu akisema Benno kacheza nafasi yake wote ni lawama tu hivi mpira wetu utafika kokote??

Hakuna kuzunguka wote kwa sauti mmoja inatakiwa tumsupport beno sio kuingiza maoni yetu wakati yye anaumia na njaa it ain't fair kabisa
Mkuu uko sahihi Kuhusu madai ya Benno ila alichokisema Coach Zahera ni njia aliyotumia kudai maslahi. Kwanza Coach alikaa nao akawaeleza hali ya kiuchumi ya Timu na akatoa option kuwa ambaye anaona hawezi kucheza mpira kutokana na hali ilivyo kwenye Timu basi atafute Timu nyingine. Zaidi ya hapo Benno ameondoka usiku wa manane baada ya kupokea ushawishi kutoka next-door. Elimu elimu elimu inahitajika kwa wachezaji wetu. Ndio maana mambo ya mikataba huwa hayamshindi Emmanuel Okwi.
 
Mkuu uko sahihi Kuhusu madai ya Benno ila alichokisema Coach Zahera ni njia aliyotumia kudai maslahi. Kwanza Coach alikaa nao akawaeleza hali ya kiuchumi ya Timu na akatoa option kuwa ambaye anaona hawezi kucheza mpira kutokana na hali ilivyo kwenye Timu basi atafute Timu nyingine. Zaidi ya hapo Benno ameondoka usiku wa manane baada ya kupokea ushawishi kutoka next-door. Elimu elimu elimu inahitajika kwa wachezaji wetu. Ndio maana mambo ya mikataba huwa hayamshindi Emmanuel Okwi.
Yeah upo sahihi sana,vijana wa kibongo hawana Elimu yoyote, mwashiuya alipokuja yanga akaulizwa tukulipe shilling ngapi akasema laki tatu,wakamwambia tutakupa laki tano akachanganyikiwa kabisa....so hawana watu sahihi wa kuwaongoza
 
Kwahiyo mtu asidai haki zake kisa atakosa maslahi fulani ya muda mrefu?? Kubalini kwamba yanga ilikosea kuahidi kumlipa ilihali haina pesa sio mnamdhulumu mtu na pesa zake hamumpi.... Trust me akienda FIFA kama yule mkenya wa Yanga enzi hizo aliyewalipisha million 40 ndio mtaelewa kwamba dawa ya Deni ni kulipa sio kelele kelele na uswahili.

Nikuulize swali hivi mchezaji asipofuata mkataba mngemtetea hivi?? Kwanini timu isipofuata mnawatetea?? Hizi double standards zitawapeleka wapi??

Mwingine anakuja na hoja eti wengine hawadai?? Kwahiyo kwa kuwa wengine wamekubali kutapeliwa basi inajustify beno kutapeliwa pia??

Tubadilike kama tunataka kusaidia mpira wetu ukue otherwise tutaendelea kuwa wasindikizaji tu
Shida ww huna taarifa za kutosha sakata la Beno ndo maana unalaumu,Ungekuwa welo infomudi,usingekuwa unateseka sana,hayo ya kutapeliana waulize ndugu zako waliokula hadi hela ya msiba wa mafisango
 
Hapa hapazungumziwi usomi wala u-Yanga. Panazungumziwa namna ya kuvumilia na kustahamili machache ya mpito ili kupata hatma yenye neema zaidi. Mandela hakuzaliwa na ANC, lakini angeweza kutolewa mapema gerezani akawa mtu huru kama tu angekana madai ya ANC ya uhuru wa walio wengi. Alivumilia na kustahamili miaka 27 gerezani na akatoka akiwa mtu bora zaidi na nchi yake ikawa huru. Buffon hakuzaliwa na (timu ya ) Juventus, lakini akakubali kubaki nayo iliposhushwa Daraja na nakisi (deficit) tangulizi ya alama kadhaa za kuanzia Serie B. Matokeo yake akaipandisha tena na kuishia na heshima iliyoambatana na mapato mengi zaidi kuliko aliyoyakosa kwa kucheza Serie B msimu mzima. Fuatilia wafanikiwa wengi, kama siyo wote : Lukaku, Mwalim Nyerere, Diamond, Pele, Mzee Kenyatta, ...... na utabaini wamefikia mafanikio yao kwa kustahamili kwa makusudi adha ambazo kama wangependa wangeweza kuziepuka.
Aidha, hata kiuchezaji ndani ya dakika za mchezo, kunahitajika ustahamilivu wa makusudi ili uwe mchezaji bora zaidi. Huo haupatikani kwa mazoezi ya dawati la ufundi wala kwa kipaji cha mchezo wenyewe, bali hupatikana kwa kuizowesha nafsi kustahamili adha na karaha. Wanaoshindwa, hata wawe timamu kiasi gani kimwili, hata wawe na kipaji kiasi gani, wanashindwa kufikia kilele chao cha mafanikio na kukosesha timu au wapenzi wao na mataifa yao ladha ya uwezo wao. Mwangalie Tyson aliyeshindwa kustahamili adha za mchezoni hadi akaamua kumn’gata sikio Holyfield, ikawaje na amekuwaje? Hakuwa amechezewa rafu za makusudi kweli? Mwangalie Serena Williams aliyeshindwa kuvumilia uonevu wa mwamuzi na kumtolea maneno mabaya kwenye fainali ya US Open ya Tennis, ikawaje? Hakuwa timamu? Hakuwa ameonewa kweli?Mwangalie Zidane alivyoikosesha Ufaransa Kombe la Dunia kwa kushindwa kuhimili udhia. Unadhani hakuwa na timamu kimwili? Au hakuwa na kipaji? Hakuwa ameudhiwa kweli?
Mazoezi ya stahamala na uvumilvu kama huo hayapatikani uwanjani, wala hayanolewi na kauli za ‘nani hakuzaliwa wapi’. Yanapatikana kwa kujifunza kutoka kwa walioweza na walioshindwa, na kwa kuwasaidia vijana wetu pale tunapowaona wanaelekea kwenye kukosa mengi kwa sababu ya machache. Lau Samatta ambaye ‘hakuzaliwa Simba’ asingepewa gari aliyoahidiwa pale alipoamua kurudi timu yake ya mchangani, tungekuwa tunaimba wimbo wake hii leo?
Naomba ujifunze kutoka maisha ya Mahatma Gandhi, Mwasisi wa mataifa ya India, Pakistan na Bangladesh na uirithishe kwa Kakolanya na wenye mtizamo kama wake. Gandhi ametanabahisha kwamba kulipiza jicho kwa jicho kutaishia na dunia ya vipofu watupu (an eye for an eye will make the whole world blind). Wakatabahu.
Mkuu Asprin jamaa kamtaja Mahtma Ghandi.
 
Beno hatukutako tena.

Siyo mtu wa kuhesabia pale unapotaka kuanza naye safari kwani atakuacha katikati ya jangwa. Ni mbinafsi. Anajali furaha yake. Hajali kazi yake. Hata mimi kama shabiki na mwanachama sitaki huyu msaliti arudi pale.
Once a snitch always a snitch.
Let karma hunt his ego. Pumbavu kabisa.
Hata uwe vipi bora kama nidhamu huna tunakutenga tu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu Timu lazima ionyeshe juhudi za kujali wachezaji mfano Borussia Dortmund iliwahi kukaribia kufilisika hata mishahara ya wachezaji ikakaribia kukauka walichofanya walienda kusaidiwa na mahasimu wao Bayern Munich na leo hii ipo vzuri kiuchumi mbona sijaona effort yeyote ya Yanga kulipa hayo madeni?? Klabu ni wachezaji sio majengo ni heri wauze hata assets za timu pesa ipatikani iwalipe wachezaji otherwise ni haki kabisa timu nzima ikigoma maana kisheria mikataba yao imekiukwa na hata wakienda FIFA wanashinda kesi

Let's be realistic guys.... Hata leeds ilipofulia iliuza mastaa wake wote ikaanza upyaa kama Yanga nao hawana pesa si iuze timu nzima iwalipe madeni yao ianze na wachezaji wa ACADEMY?? Kigumu kipi?? Yaani timu haina hela ila inataka ijaze mastaa..... Mkishindwa mnataka wachezaji ndio wateseke

Kwa staili hii mpira wetu huendi kokote
Mnachoshindwa kuelewa nyinyi mashabiki wa Simba ni kuwa mkataba unasainiwa kati ya pande mbili au zaidi. Pili, kila mkataba unaweza kuvunjwa wakati wowote ule, ili mradi pande hizo ziafikiane na terms. Kwa hiyo, kuna "terms" za kusaini mkataba na "terms" za kuvunja mkataba. Hilo bila ushabiki wote tunakubaliana.

Baada ya hapo, sasa tujadili issue ya Beno.
Yanga walikiuka "term(s)" za mkataba.kwa kutomlipa Beno, signing bonus. Yanga inawalipa mshahara wachezaji wake ila tatizo kubwa ni signing bonus.
Kuna waliolipwa nusu na kuna ambao hawajalipwa kabisa. Hili ni kosa kwa upande wa Yanga. Na wachezaji wana haki ya kuvunja mkataba na Yanga, na wakaendelea kuwa free agents.
Wakaombwa na kushauriwa na mwalimu, wakakubali kuichezea Yanga kwa sababu mbalimbali iwe kuwapa nafasi Yanga, ku showcase talents zao na kutumia muda huu kuongeza skills, kuwatunzia heshima mashabiki ambao wengine wamewaunga mkono tangu mchangani, na kulinda hadhi ya ligi na soka ya Tanzania kwa ujumla. Kwa hili nawapa heshima sana, na sitawalaumu hata wakifungwa mechi zote zitazofuata.

Kama walikubali hivyo, basi wawe hivyo na akitokea mchezaji au wachezaji wasiotaka kuendelea, basi waondoke watuachie timu yetu sisi tutachukua hata wachezaji wa kichangani. Lakini, kwa kufuata ushauri, wachezaji wengi wameanza kupata fedha na heshima kubwa kutoka kwa mashabiki. Yanga hiyohiyo mnayoita masikini inapanda ndege kuliko karibu timu zote na mzuka wa mashabiki wake hauna mfano.

Beno, amekataa kucheza bila kulipwa kwanza na sisi mashabiki tunakubali. Ila, atuache kwa sasa hivi, hatumtaki na wakimrudisha, wataleta mgogoro. Kwa hiyo bora aende Simba au Azam.
 
Maneno meeengi siasa tupu. Lipa hela ya dogo ana familia yule,mnataka huduma bure?mpira ni ajira,tena ingekuwa mimi nawapeleka mahakamani kabisa
 
.
Wakaombwa na kushauriwa na mwalimu, wakakubali kuichezea Yanga kwa sababu mbalimbali iwe kuwapa nafasi Yanga, ku showcase talents zao na kutumia muda huu kuongeza skills, kuwatunzia heshima mashabiki ambao wengine wamewaunga mkono tangu mchangani, na kulinda hadhi ya ligi na soka ya Tanzania kwa ujumla. Kwa hili nawapa heshima sana, na sitawalaumu hata wakifungwa mechi zote zitazofuata.

Kama walikubali hivyo, basi wawe hivyo na akitokea mchezaji au wachezaji wasiotaka kuendelea, basi waondoke watuachie timu yetu sisi tutachukua hata wachezaji wa kichangani. Lakini, kwa kufuata ushauri, wachezaji wengi wameanza kupata fedha na heshima kubwa kutoka kwa mashabiki. Yanga hiyohiyo mnayoita masikini inapanda ndege kuliko karibu timu zote na mzuka wa mashabiki wake hauna mfano.

Beno, amekataa kucheza bila kulipwa kwanza na sisi mashabiki tunakubali. Ila, atuache kwa sasa hivi, hatumtaki na wakimrudisha, wataleta mgogoro. Kwa hiyo bora aende Simba au Azam.
Na shida ndio inaanzia hapa kwamba waliombwa?? Mi nikajua kuna commitment clause walisainishwa kuwa walipwe wasilipwe wasiache kucheza...... Kumbe ni maneno tu na sio sheria?? Sasa umeona wapi watu wanakubaliana kwa maneno?? Hivi leo nikisema Benno hakukubali hilo utakataaje ilihali hawakusaini mkataba wowote utakaowafunga kisheria kiasi kwamba wakikiuka watatimuliwa?? Sasa kama klabu zetu zinaongowa kiswahili hivi kwa maneno ya korido tutafika kweli??

Nimeshatoa mfano Leeds iliokuwa timu tishio Uingereza ilipokuwa inafilisika iliamua kuuza wachezaji wake mastaa sababu ingekosa hata mishahara sasa kwanini Yanga wasiige?? Kwanini msiuze hao mastaa wenye mishahara mikubwa mkaenda kusajili wachezaji wakujitolea ndio muwasainishe commitment clauses kuwa anacheza ila hakuna kulipwa? Kwanini hamko formal na washabiki hamuwaelezi ukweli viongozi wenu kuwa wamefeli kuendesha timu??

Actually timu ina umri mkubwa kuliko hata Tanzania ila inashindwa kuwa na assets za kuiendesha club wakati wa crisis kma hizi?? Hata uwanja tu mmeshindwa kujenga leo hii Azam ana uwanja na financial capacity kuliko timu zenu kongwe?? Badala mshauri mabadiliko mmekalia kuleta mahaba kwa timu..... Hii haisaidii kabisa.

Wachezaji kususa ni kawaida mkuu hata Diego Costa aliweka mgomo baridi kusikia griezmann analipwa mara 4 kuliko yeye ila muhimu muwape haki zao kma hamuwezi muwauze sio kuwatesa hivi alafu wakishindwa mnaanza kuwatukana

Huyo zahera haelewi mpira wa bongo siku akikosa ligi na simba ikamfunga kma 6-0 kama naona mtakavyomgeuka na kumtimua na matusi juu.... Yetu macho na masikio
 
Ndio tumeshashindwa kumlipa... Kaandika barua ya kuvunja mkataba ...basis atulie au aende kamati ya hadhi za wachezaji ama mahakama ya michezo lakini sii kurudi tena alipoomba mkataba uvunjwe
Nlichogundua wengi humu mnachangia kwa kuongozwa na ushabiki usio na tija..... Yaani kwa kuwa mna mahaba na timu basi mko tayari kusimama nayo hata wakikosea mkidhani mnasaidia.... Mkataba mnaposaini unaweka majukumu ya pande zote mbili za klabu na mchezaji.... Yeye mchezaji ni kucheza mpira na timu ni kumpa stahiki zake sasa Yanga inapokiuka clause za mkataba inakuaje benno aonekane mbaya ilihali mchezaji akitoroka kambi au akichelewa mazoezini naye huwa amekiuka mkataba na huwa anaadhibiwa licha ya kuwa na sababi za msingi sasa kwanini mnaangalia upande mmoja??

Mtu hajalipwa pesa yake na ana matatizo mlitaka afanyeje?? Ana madeni mlitaka afanyeje?? Kwanini timu isikope imlipe??

Shida watu humu mnaongozwa na mahaba ndio maana mpira wa Tanzania haukuwi.... No wonder hakuna timu ya bongo imewahi fanya vzuri kimataifa maana mmejaa uswahili sana na ubabaishaji na washabiki wenyewe ndio wanafiki hivi hatutofika kokote.
 
Back
Top Bottom