Kama ni kweli gari la wanawake BAWACHA limepigwa mawe wahusika wakamatwe

Kama ni kweli gari la wanawake BAWACHA limepigwa mawe wahusika wakamatwe

MamaSamia2025

JF-Expert Member
Joined
Mar 29, 2012
Posts
14,588
Reaction score
32,361
Nimesikitishwa mno na habari niliyosoma kwenye ukurasa rasmi wa Askofu wa CHADEMA ndugu Emanuel Mwamakula kuhusu basi la wanawake wa CHADEMA mkoa wa Mwanza waliokuwa wakitoka Dar kupigwa mawe huko Singida. Hiki ni kitendo kiovu kinachopaswa kulaaniwa. Vijana wanaotuhumiwa kufanya hivyo wakamatwe na kufikishwa mahakamani.

Ninawasihi vijana kutoka familia maskini kujikita kupambana kuuondoa umaskini kwenye familia zao badala ya kujihusisha na matukio maovu. Hakuna mtoto wa kigogo wa CCM au upinzani utamkuta kwenye matukio kama haya. Yaani hata kukuta mtoto wa kigogo anatukana mtandaoni ni ngumu. Wazazi wao wanajua kabisa kiongozi unatakiwa uwe na busara na kujiepusha kabisa na jinai.

Tusubiri taarifa ya polisi kwa ufafanuzi zaidi.
 
Ndani ya CCM kuna mashetani na maharamia ya ajabu, na hayo ndiyo yanayoambukiza uovu kwa watoto wetu.

CCM.ni alama ya uwepo wa shetani Duniani.

Ni wakati wa wote wenye Roho wa Mungu kujitenga na shetani CCM.
 
Ndani ya CCM kuna mashetani na maharamia ya ajabu, na hayo ndiyo yanayoambukiza uovu kwa watoto wetu.

CCM.ni alama ya uwepo wa shetani Duniani.

Ni wakati wa wote wenye Roho wa Mungu kujitenga na shetani CCM.
We chizi si bure
 
Wanaccm karibia wote wamekuwa na kinga ya dola pindi wanapowafanyia uhalifu wapinzani hasa cdm. Wakati wa Magufuli ilikuwa kama imehalalishwa waccm kuwafanyia uhalifu cdm, na polisi walikuwa wanaona fahari cdm kufanyiwa ukatili na wanaccm. Ikafikia hadi afisa yoyote wa vyombo vya dola akiwafanyia ukatili cdm kupandishwa cheo, ama kuongeza nafasi yake ya kupandishwa cheo. Hata sasa chini ya Samia bado hali ni hiyohiyo, japo si kwa kiwango cha ilivyokuwa wakati wa Magufuli.

Hayo ya Singida ni muendelezo wa hilo, kuelekea uchaguzi iwapo cdm watashiriki ndio itakuwa mbaya zaidi. Kibaya zaidi hakuna atakayechukuliwa hatua na mamlaka kwa uhalifu huo.
 
Mmeanza mtindo wa kujitengenezea scenario ili kupata tukio ambalo lita sound na wapuuzi waone huruma hatimaye waone mnaonewa na mpate wanachama kwa njia ya huruma.
 
Mmeanza mtindo wa kujitengenezea scenario ili kupata tukio ambalo lita sound na wapuuzi waone huruma hatimaye waone mnaonewa na mpate wanachama kwa njia ya huruma.
Uliishia darasa a ngapi? Ulianza lini kushabikia na kufuatilia siasa za Tanzania???? Jifunze ili upate maarifa zaid
 
Makundi ya Mbowe na Lisu wameshaanza kupopoana mawe

Hao watakuwa Timu Lisu waliowapopoa mawe wenzao hao timu Mbowe
 
Mmeanza mtindo wa kujitengenezea scenario ili kupata tukio ambalo lita sound na wapuuzi waone huruma hatimaye waone mnaonewa na mpate wanachama kwa njia ya huruma.
Lissu pia mlisema amejipiga risasi.
 
Ndani ya CCM kuna mashetani na maharamia ya ajabu, na hayo ndiyo yanayoambukiza uovu kwa watoto wetu.

CCM.ni alama ya uwepo wa shetani Duniani.

Ni wakati wa wote wenye Roho wa Mungu kujitenga na shetani CCM.
Mimi sijataja kuwa wahusika ni CCM au chama fulani. Hao ni wahalifu bila kujali chama. Tumia akili kabla ya ku-comment
 
Huu ni mwanzo Ninadhani target Yao kubwa ni gari ya Mwenyekiti wa Chadema Taifa.
 
Ushamba tu unazani kuzaliwa marekani ni big deal ?
Una roho mbaya hata maandishi yako tu yanaonyesha hivyo. Pambana na hali yako. Kuna sababu ya kula mmoja wetu kuzaliwa alikozaliwa. Kwahiyo hata kuongelea tu ni aina Fulani ya kwamba umechafukwa.
 
Nimesikitishwa mno na habari niliyosoma kwenye ukurasa rasmi wa Askofu wa CHADEMA ndugu Emanuel Mwamakula kuhusu basi la wanawake wa CHADEMA mkoa wa Mwanza waliokuwa wakitoka Dar kupigwa mawe huko Singida. Hiki ni kitendo kiovu kinachopaswa kulaaniwa. Vijana wanaotuhumiwa kufanya hivyo wakamatwe na kufikishwa mahakamani.

Ninawasihi vijana kutoka familia maskini kujikita kupambana kuuondoa umaskini kwenye familia zao badala ya kujihusisha na matukio maovu. Hakuna mtoto wa kigogo wa CCM au upinzani utamkuta kwenye matukio kama haya. Yaani hata kukuta mtoto wa kigogo anatukana mtandaoni ni ngumu. Wazazi wao wanajua kabisa kiongozi unatakiwa uwe na busara na kujiepusha kabisa na jinai.

Tusubiri taarifa ya polisi kwa ufafanuzi zaidi.
Hao ni wazushi wamezoeleka
 
Back
Top Bottom