Kama ni wapenzi na mnafichiana simu basi hampendani

Kama ni wapenzi na mnafichiana simu basi hampendani

ndege JOHN

JF-Expert Member
Joined
Aug 5, 2015
Posts
21,643
Reaction score
51,642
Achana na hizi kauli kwamba usishike simu ya mumeo/mkeo ikiwa unataka kulinda penzi..hizo ni kauli za watu malaya au wasio waaminifu kwenye mapenzi yao.kimsimgi kama mnapendana na mwenzako inatakiwa hata akusaidie kuchart kwenye ma group funny kama ya classmate..yaani kama umechoka na unaona inahitajika uonekane uko active sio vibaya kumpa simu mwenzi wako aendelee na stori.mimi mke wangu kashajua ninapenda jamiiforum na yeye analipenda jukwaa la MMU ila sio kuchangia yeye anapenda tu kusoma comment zenu.sijaona sababu bado ya kuficha sijawahi kumsaliti hata siku moja na labda ikija kutokea nikalazimika siwezi kutengeneza mazingira ya huyo nyumba ndogo anitafute tafute kwenye simu kiasi nikawa na wasiwasi na hofu kwenye simu mbele ya mwenzangu.
 
Kisa cha kukagua simu ni kuhisi mwenza wako anatumia njia za siri kama zako kucheat.

Hivyo unamlia timing, ukiona ke/me anakagua sana simu yako huku wewe huna time na simu yake jua anakucheat, hivyo anafuta kulevel mzani ajione hana hatia kukucheat.
 
Wewe umeshasema hauchepuki ndio maana unajiamini kumuachia simu mtu wako, hizi mbuzi nyingine zinajua zinachofanya ndio maana zinatetea kutoshika simu ya mwenza wako, anyway jiandae kuambiwa wewe ni dhaifu na siyo mwanaume rijali kisa hauchepuki
 
Tunaposema usishike simu ya mume/mke tunamaanisha usiipekue. Hakuna sababu ya kupekuana kwenye simu. Unatafuta nini? ili iweje? Na haimaanishi tunachepuka... simu haizuii mtu kuchepuka na haionyeshi mchepukaji. (hasa kama mchepukaji anajielewa) Kwenye simu ya kila mmoja kuna siri zaidi ya kuchepuka... wakati mwingine kuna mambo ya familia, ofisi na issue binafsi ambazo hupaswi kuzijua hadi uambiwe! Kwa hiyo tuliza kiuno... kama kuna la kuambiwa utaambiwa... usilitafute kwa kupekua simu. Zaidi ya yote jifunze kuishi kwa kutafuta kuwa na amani daima ambapo utaipata kwa kutofukunyua yasiyokuhusu kwenye simu!
 
Tunaposema usishike simu ya mume/mke tunamaanisha usiipekue. Hakuna sababu ya kupekuana kwenye simu. Unatafuta nini? ili iweje? Na haimaanishi tunachepuka... simu haizuii mtu kuchepuka na haionyeshi mchepukaji. (hasa kama mchepukaji anajielewa) Kwenye simu ya kila mmoja kuna siri zaidi ya kuchepuka... wakati mwingine kuna mambo ya familia, ofisi na issue binafsi ambazo hupaswi kuzijua hadi uambiwe! Kwa hiyo tuliza kiuno... kama kuna la kuambiwa utaambiwa... usilitafute kwa kupekua simu. Zaidi ya yote jifunze kuishi kwa kutafuta kuwa na amani daima ambapo utaipata kwa kutofukunyua yasiyokuhusu kwenye simu!
[emoji1635]
 
Back
Top Bottom