Kama ningepewa nafasi ya kukushauri....

Kama ningepewa nafasi ya kukushauri....

Joined
Jul 26, 2017
Posts
25
Reaction score
48
Ndugu zangu wa-Tanzania mambo vipi? Mko poa? Kama jibu ni ndio basi fresh na kama sio basi hakuna tabu, ila ninamachache ya kuzungumza na ninyi then niende zangu.

Nisikilize sasa,

Hakuna kipindi kigumu wanachopitia watanzania kama kipindi hiki na wengine wameanza kwenda mbali zaidi na kutafuta watu wa kuwatupia lawama, wengine wakimtupia lawama Mh. Mwigulu Nchemba kwa sababu ya tozo, na wakidai kuwa yeye ndio sababu ya kupoyeza amani za watu. Ni kweli kuna "tozo" zimeongezeka lakini niwathibitishie kuwa hakuna kitu ambacho kitadumi milele lakini pia hata kama kitadumu basi njia ya kulitatua tatizo hilo sio kulalamika, njia sahihi ni kutokufuatilia kabisa vilinge, mikusanyiko ambayo watu wanakutana kujadili mambo hayo, badala yake hiyo nguvu inayotumia kulaumu watu na viongozi ingehamishiwa katika kazi hakuna mtu ambaye angeendelea kulalamika.

NINI UFANYE...

Hiki ni kipindi kigumu sana kwa watanzania, hasa watu wanaojikita zaidi katika kufuatilia habari, imagine, unataka kupumzika, mara unasikia Yanga na Simba wako hivi, mara Mandoga kafanya hiki, ujatulia mara tozo ziko juu, ujatulia mara, mishahara haijaongezeka, mwisho wa siku hali hii inakupelekea na wewe kuingia katika kikundi cha walalamishi na hapo ndipo unapoanza kujiua zaidi.

Jambo la Msingi,

Unapaswa kuwaza zaidi ya kila changamoto inayokutokea, kama fedha imekuwa kikwazo, unapaswa kuwaza mara kumi zaidi ya serikari namna ya kujitatulia. Kama tozo, anza kujikata wewe mwenyewe tozo na kujiwekea akiba kwako, i mean ujilazimishe hata kama hupendi, jifanye wewe ndio Mwigulu Nchemba wa maisha yako, usijipe sababu za kijinga jitoze mwenyewe na jiwekee akiba na ikitoke wenzako wanalalamika wewe uko mbali mno. Ujinga mkuu ni kuanza kulalamika hovyo unapoona mambo hayaendi vizuri, sasa sijui unadhani nani atakuja kukutatulia matatizo yako? Hakuna mtu wa kuja kukusaidia usipoamua kithabiti kuwa Mwigulu Nchemba wa maisha yako. Sijui naelewek vile? Eeeh, haya ngoja nikomee hapa kama hujaelewa rudia kusoma, kama umedaka japo machache nipe tano!! Mwigulu Nchemba wa Maisha yako ni Wewe, anza kujitoza tozo katika maisha yako na iweke katika akiba zako, hutajutia.


Thanks All. - Deus Michael Ndololo
 

Attachments

  • IMG_20220208_115233.jpg
    IMG_20220208_115233.jpg
    697.6 KB · Views: 10
unapaswa kuwaza mara kumi zaidi ya serikari namna ya kujitatulia
Mkuu watu wanaenda extra miles nini ×10 watu wanafika Mpaka ×1000 zaidi ya serikali ndio maana unasikia malalamiko

Ungejiuliza tena kisha tafakari alafu fanya updates kwenye huu uzi upo so shallow kuna vitu umeacha kuelezea kwa marefu na mapana

Tuelezee hizo fikra zako ulizofikiria ×10 zaidi ya serikali ukiacha hii ya kujiwekea Akiba ambayo ipo tangu karne na karne na wachumi wanaendelea kuzindua zingine mpya

Wewe umevumbua nini ambacho hakijawahi kuonekana na wala hakijawahi kutumika?

Hio ndio tunaita ×10 zaidi ya .........

Copy that
 
Asante kwa ushauri kwani unadhani watu hawahangaiki kujikwamua kutokana na hali hii watu wanaumiza vichwa mnoo uhalisia wa humu mitandaoni na kwa ground ni tofauti
 
Mkuu watu wanaenda extra miles nini ×10 watu wanafika Mpaka ×1000 zaidi ya serikali ndio maana unasikia malalamiko

Ungejiuliza tena kisha tafakari alafu fanya updates kwenye huu uzi upo so shallow kuna vitu umeacha kuelezea kwa marefu na mapana

Tuelezee hizo fikra zako ulizofikiria ×10 zaidi ya serikali ukiacha hii ya kujiwekea Akiba ambayo ipo tangu karne na karne na wachumi wanaendelea kuzindua zingine mpya

Wewe umevumbua nini ambacho hakijawahi kuonekana na wala hakijawahi kutumika?

Hio ndio tunaita ×10 zaidi ya .........

Copy that
Rafiki,
Moja kati ya vitu nilivyolenga kumuelimisha mtu mmoja ni namna ya kuwaza zaidi ya serikali yetu, huku nikipinga sana swala la kulalamikia watu (either ni viongozi au la) lakini pia swala la kuweka akiba sio swala la kuzoweleka, ni swala ambalo linahitaji ukuaji day to day, ni kweli ni msingi ulioanza tangu kipindi cha mababu zetu, lakini hata sasa tunaweza kuendelea kuuboresha zaidi na zaidi kwa kuendelea kuiwekeza zaidi na zaidi akiba uliyojitunzia. Pia, nirudie, akiba aizoeleki na ukiona umeanza kuizoea basi uko chini yakiwango husika, ongeza kiwango cha akiba unachoweka.
 
Asante kwa ushauri kwani unadhani watu hawahangaiki kujikwamua kutokana na hali hii watu wanaumiza vichwa mnoo uhalisia wa humu mitandaoni na kwa ground ni tofauti
Ni kweli rafiki, lakini idadi kubwa ya wanaolalamika inazidi kuongezeka kwa kasi mno mpaka inatia huruma. Tena mbaya zaidi kila mtu anawatupia wengine na hilo ndio kosa kubwa zaidi.
 
Back
Top Bottom