Kama Taifa tukubali kuna makosa yalifanyika, tujirekebishe yasijirudie, japokuwa ni ngumu kuondoa makovu yaliyopatikana

Kama Taifa tukubali kuna makosa yalifanyika, tujirekebishe yasijirudie, japokuwa ni ngumu kuondoa makovu yaliyopatikana

Nyankurungu2020

JF-Expert Member
Joined
Oct 2, 2020
Posts
4,170
Reaction score
6,757
Kuendelea kushupaza shingo kuwa hakuna makosa yaliyofanyika juu ya uvunjifu wa haki za binadamu hapa nchini kwetu ni kupoteza muda. Maana ni kutaka kujenga taswira isiyofaa kuwa mauaji, ukatili na uvunjifu wa sheria ni jambo la kawaida.

Tukubali kuwa kuna makosa makubwa yalifanywa na vyombo vya dola na yanaendelea kufanywa na vyombo vya dola. Maana mbali ya watu wanaojulikana kama Lissu, Saanane, Alphonse Mawazo bado kuna malalamiko makubwa juu ya ukiukwaji wa haki za binadamu unaofanywa na vyombo vya dola. Mbaya zaidi viongozi wanajua na wanafumba macho.

Tusishupaze shingo, tukubali makosa yalifanyika na tujirekebishe maana kukosolewa au kupata mawazo kinzani ni sehemu ya maisha. Hii nchi ni ya kwetu sote.

Lakini je nani atayafuta makovu yaliyopatikana na udhalimu waliofanyiwa akina Alphonse Mawazo, Tundu Lissu, Ben Saanane na wengine wengi ambao hawajulikani?
 
Kuna uvunjifu wa haki za watu sana ndani nchi hii. Mf; wiki mbili zilizopita maeneo ya Tengeru kuna trafik aligombana na bodaboda yule boda akatoroka pikipiki ikabaki.

Kesho yake wale askari wamekuja wanapiga kila mwendesha pikipiki awe boda hasiwe boda unajua hujui wakawashika na kuwapeleka mahakamani baada ya hapo magereza ya kisongo wiki mbili.

Kwa tabia kama hizi, wananchi hawezi kuvipenda hivi vyombo vya dola wala kuvipa ushirikiano wa maana.
 
Waadhirika ambao bado wapo hai walipwe na wale waliokufa kwa sababu za kisiasa kama vile Mdogo wetu Akwilina, ndgu zetu Ben saanane, Azory Gwanda, Mawazo, na wengine wengi Familia zao ziombwe radhi na kulipwa fidia.
 
Kuendelea kushupaza shingo kuwa hakuna makosa yaliyofanyika juu ya uvunjifu wa haki za binadamu hapa nchini kwetu ni kupoteza muda. Maana ni kutaka kujenga taswira isiyofaa kuwa mauaji, ukatili na uvunjifu wa sheria ni jambo la kawaida....
Kama yule Luena wa Ifakara na yule wa Hananasifu waliuliwa kikatili sana.
 
Kuendelea kushupaza shingo kuwa hakuna makosa yaliyofanyika juu ya uvunjifu wa haki za binadamu hapa nchini kwetu ni kupoteza muda. Maana ni kutaka kujenga taswira isiyofaa kuwa mauaji, ukatili na uvunjifu wa sheria ni jambo la kawaida....
Vile thread mbuzi umevianza tena
 
Angalau ungeongelea wale wanyonge wanaokufa kwa kukosa huduma za afya ningekuona wa maana kumbe ni hao wasaka tonge na umaarufu wa kisiasa ndio wanawakilisha watanzania milioni 50 [emoji1787][emoji1787][emoji1787]
 
Waadhirika ambao bado wapo hai walipwe na wale waliokufa kwa sababu za kisiasa kama vile Mdogo wetu Akwilina, ndgu zetu Ben saanane, Azory Gwanda, Mawazo, na wengine wengi Familia zao ziombwe radhi na kulipwa fidia.
Na kwa mujibu wa maandiko katika vitabu vitakatifu. Tunasoma kuwa kuna dhambi ambazo husamehewa kwa kuwaomba msamaha watendewa, wala sio kwa Mungu. Vinginevyo Mungu hahusiki na msamaha unaoombwa.
 
Back
Top Bottom