Kama Taifa tukubali kuna makosa yalifanyika, tujirekebishe yasijirudie, japokuwa ni ngumu kuondoa makovu yaliyopatikana


Umelazimisha kutoa mifano irrelevant, matokeo yake mifano yako haichekeshi, haifikirishi na wala haina mashiko.
 
Hakuna anayetaka kupendwa na wote acha upotoshaji, hoja ni unachukiwa kwa nini, na mifumo ya kutoa haki inafanyaje kazi chini yako. Mwenendo wa taasisi za kutoa haki tunaona kwa macho yetu ukiwa na hofu ya maamuzi ya mtu muovu.
Wahuni wanaomchukia ni sababu ya yule jamaa aliekimbilia kwa amsterdam
 
Umelazimisha kutoa mifano irrelevant, matokeo yake mifano yako haichekeshi, haifikirishi na wala haina mashiko.
Narudia Chadema kumefanyika mapunduzi Mnaoita Covid 19 wamepindua Mbowe Gadafi na wamepindua Tundu Lisu Hussein mbarak na wamepindua Godbless Lema Mugabe na wewe Tindio Saddam Hussein wakatinga Bungeni

Kazi kwenu
 
😃MKUU TINDO nchi ambazo zinatii Sheria walau 85💯 zilifanyeje mpaka zikafika hapo.

Shida sio kufungwa Wala kuuliwa.

Shida Ni Jambo la ujumla kutizamwa KIBINAFSI.

CHANZO CHA YOTE SIO SERIKALI Bali UBONGO ZETU na Nini tunahitaji tumekabizi mikononi mwa wanasiasa.
 
Narudia Chadema kumefanyika mapunduzi Mnaoita Covid 19 wamepindua Mbowe Gadafi na wamepindua Tundu Lisu Hussein mbarak na wamepindua Godbless Lema Mugabe na wewe Tindio Saddam Hussein wakatinga Bungeni

Kazi kwenu

Nasema hivi, haichekeshi.
 

Hebu fafanua hapo jambo la jumla kutazamwa kibanafsi. Halafu toa mapendekezo nini kifanyike ambacho kitakuwa sio kukabidhi majitaji kwa wanasiasa. Maana mpaka sasa mambo yote ya nchi hii yote yanaamuliwa na wanasiasa na sio kada nyingine yoyote.
 
K
Kwahiyo hata kama sio 33 Ni 2. Wewe unaona sawa? Kwanini mtu akiwa CCM anakuwa mjinga kiasi hiki!!
 
Mkuu mleta mada jua tu kwamba nchi hii hivi sasa ni “hopeless case”. Iko katika mazingira ambayo walioshika madaraka kupitia nyenzo ya chama dola wameyadhibiti kikamilifu na hakuna kinachowatisha kusababisha walegeze msimamo.

Kilichotokea Afrika ya Kusini, ni kwamba zile “multinational enterprises” ambazo ndizo zinadhibiti uchumi wa nchi hiyo zilishtuka kuwa zinapoteza fursa kubwa za uwekezaji na biashara Afrika na duniani kwa ongezeko la vikwazo. Kilikuwa ndio kipindi utandawazi unapigiwa debe kwa nguvu sana. Halafu wakagundua hata viongozi wa ANC walikuwa tayari kwa muafaka utakaohakikisha uchumi wa nchi hauathiriki. Hivyo wakaona kukumbatia “apartheid” ili tu kulinda makaburu/weupe wa hali ya chini (working class) ni ujinga. Wakapiga deal na Mandela kukabidhi serikali kwa weusi na kuitisha “Truth and Reconciliation Commission”.

Hapa kwetu hakuna kinachowasukuma wanaoshika madaraka kutaka maelewano na mwananchi yeyote. Nguvu ya dola ni jibu tosha kwa kero yoyote. Na ujumbe wa mwisho unaotolewa ni kila mtu ahangaike na maisha yake na ya wategemezi wake. Hata masuala ya covid message ni hiyo hiyo. Watanzania hatuna kitu cha kupigania pamoja kinachojulikana kama “common interests” - maslahi ya pamoja. It’s everyone for himself and God for all of us.
 
Hakuna uvunjifu wowoye wa haki za binadamu Tanzania. Hao uliowataja ni viherehere vyao yu vya kujifanya wajuaji na wajuaji wenzao wakawafanyia ya kuwafanyia.
 
Tii sjeria bila shuruti, vinginevyo utapigwa tu
 
Tungepita njia anayopita Rais Mwinyi kuwaunganisha Wazanzibari nafikiri tungefika pazuri. Hii chuki iliyoasisiwa na CCM mpya au awamu ya tano italiangamiza Taifa.
Nadhani dawa ya moto ni moto
Ngoja ifike pande yao.
Watajua hawajui
 
Ushauri unawezekana kutekelezeka kama kuna uongozi lkn kama Kuna utawala wa kidikteta, hili haliwezekani.

Dikteta huwa anawachukulia wananchi kama vitu siyo watu. Anawaburuza anavyotaka.
DIKTETA kishafurushwa na mambo yake yalishazikwa naye pale Chato siku ya tarehe 26/3/ 21.

Ile kauli ya Rais SSH kuwa atakaa na viongozi wa vyama vya Siasa naamini inabeba maudhui ya maridhiano
 
kauli ya Rais SSH kuwa atakaa na viongozi wa vyama vya Siasa naamini inabeba maudhui ya maridhiano
Mama SSH naona naye kama hayuko serious. Amewaandikia chadema kwamba hoja wanazotaka kumpeoekea wampelekee John Shibuda (mwenyekiti wa baraza la vyama vya siasa) ambaye ndiye atazipeleka kwa SSH).

Why ? Mama yuko serious kweli??
 
Mama SSH naona naye kama hayuko serious. Amewaandikia chadema kwamba hoja wanazotaka kumpeoekea wampelekee John Shibuda (mwenyekiti wa baraza la vyama vya siasa) ambaye ndiye atazipeleka kwa SSH).

Why ? Mama yuko serious kweli??
At least kuna sehemu ya kuanzia. Let's appreciate kwa chochote kidogo kinachokuja. Mbona yule MWEHU hakupata kutoa hata huo mwongozo zaidi ya kumfuatulia risasi Lissu na kubomoa Bilicanas.

Tuchukue kilichopo mezani, halafu tuombe kingine
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…