Kama tuhuma dhidi ya Kinana zilikuwa siyo za ukweli basi Msigwa ana uwezo mdogo wa akili. Kama zilikuwa na ukweli basi kuna dili lilichezwa

Kama tuhuma dhidi ya Kinana zilikuwa siyo za ukweli basi Msigwa ana uwezo mdogo wa akili. Kama zilikuwa na ukweli basi kuna dili lilichezwa

Enzi zile ilikua kama mashindano kwa wabunge wa cdm kuibua chochote ili kujipatia umaarufu zaidi
Sio wabunge tu, hata sisi hapa Jamvini, tulikuwa kila mara tunamuongelea Kinana hivyo! Kila akijitokeza, tulikuwa tunasema anamaliza tembo wetu!
Inawezekana alishindwa kutushtaki, kwani tumejificha. Msigwa, akajilipua, kama Lyatonga alivyokuwa amejilipua ile issue ya milioni 900.
 
Chadema walishapotezxa ueleke pale walipomchukua Lowassa na Sumaye kuwa wanachama wao na kumteua Lowassa kuwa mgombea wao wa utiketi ya urais kwani walionyesha kushindwa kusimamia kauli zao pia watu makini waliachanaa nao sasa hivi wamebaki na watu wanaoitwa nyumbu ambao wanaamini kila linalosemwa na uongozi wao
 
Ndugu watanzania wenzangu,

Natumaini mko salama.

Kama kichwa cha habari hapo juu kinavyojieleza. Nilimsikiliza kwa makini sana ndugu Msigwa wakati akiongea na wanahabari kuhusu kuomba msamaha kwa Kinana dhidi ya tuhuma za ujangili alizozitoa bungeni. Katika maelezo yake, mambo mawili niliweza kuyadadavua: (a) Kama tuhuma zilikwa siyo zaukweli, he is really a low-IQ political leader ever, na (b) kama zilikuwa na ukweli, basi kuna dili limechezwa kati ya hawa watu wawili kulinda maslahi yao.

Kwanini Msigwa nimemuita a low-IQ political leader ever? Kwanza kabisa na mnukuu “Katika kesi hiyo iliyosikilizwa na kuhukumiwa na jaji Zainabu Mluke, nilikutwa na hatia baada ya kushindwa kuthibitisha tuhuma zangu hizo mbele ya mahakama. Leo nakiri mbele yenu, kupitia ninyi mbele ya watanzania kwamba, tuhuma hizo nilizozitoa mara kadha dhidi ya Kinana, hazikuwa na ukweli wala ushahidi wowote, taarifa nilizopewa nakuzitumia hazikuwa na ukweli bali malengo potofu ya kisiasa na kizandiki. Nachukua full responsibility, kwa sababu mimi nilikuwa waziri kivuli, nilipaswa nifanye homework yakutosha pamoja na kwamba taarifa hizo nilipewa na mtu ninayemuamini”………

Kwanza nilianza kwa kutafiti ili nijue kiwango cha elimu cha msigwa, nkaipata CV yake ambayo inaonyesha, Msigwa ana shahanda ya kwanza (Theology) 2004-2007, All African Bible College, Durban, Kwazulu Natal, South Africa (ABBC-Durban). Hii ndiyo elimu ya juu aliyonayo ndugu Msigwa kwasasa. Kwa kiwango hiki cha elimu, na wadhifa wa uongozi aliokuwa nao (waziri kivuli-mali asili na utalii), siamini kama kweli alikuwa hajui kama hauna nyaraka za kuthibitisha unachokisema, utakuwa unaudangaya umma.

Isitoshe, sina uhakika kama Msigwa hakujua kuwa kauli zake hizo tayari zimeathiri reputation yake (Hapa na maana ya kwamba, Msigwa atakuwa na ujasiri gani tena wa kuuambia umma kwa jambo lolote lile?). Hii inafanana na tuhuma za ufasidi walizompa Lowasa, baadae hao hao wakamsafisha akawa tena siyo fisadi, na jambo hili (political gambling), imeathiri taswila ya chama mpaka leo. Upeo wa kufikiria wa Msigwa hapa ulikuwa mdogo sana, inaonekana maslahi binafsi yalitawala bila kufikilia kwa kina ni kwa kiwango gani hizi kauli zinaenda kuiathiri his political career.

Msigwa alitakiwa ajifunze kwa Dr. Slaa, mzee huyo alikuwa akiambatana na nyaraka kwa kila tuhuma aliyokuwa akiitoa kwa serikali au mtu binafsi. Hapa naona thamani ya mzee Slaa ndani ya CDM. Kutokuwepo kwa mzee huyu, chama kimekosa watu weledi na focus ya c hama iko dilemma mpaka leo. It is time to go back to the drawing board, au Chama kitafute mathink tank wapya.

Hawa wawili (Msigwa na Kinana), kunauwezekano wamekula dili pamoja. Inawezekana ushindi wa Kinana uliambatana na Msigwa kutakiwa kumlipa Kinana findia ya kumchafua, na inawezekana ni hela ndefu sana ambayo msigwa ilimshinda kuilipa (just my speculation), ndiyo ikampa kinana fulsa ya kumwambia Msigwa amsafishe mbele ya umma (you scratch my back I scratch yours).

Nawasilisha kwa majadiliano

Kejuu
Kwani kwenye hiyo kesi Mh. Msigwa hakuwakirishwa na Wakili Nguli Tundu Lissu? Hata ushauri tu ili ashinde kesi? Ahahahahahahh! Wakili Nguli Tundu Lissu!!!
 
Sio wabunge tu, hata sisi hapa Jamvini, tulikuwa kila mara tunamuongelea Kinana hivyo! Kila akijitokeza, tulikuwa tunasema anamaliza tembo wetu!
Inawezekana alishindwa kutushtaki, kwani tumejificha. Msigwa, akajilipua, kama Lyatonga alivyokuwa amejilipua ile issue ya milioni 900.
Lyatonga alishinda kwenye Kesi ya Milioni 900!
 
Ndugu watanzania wenzangu,

Natumaini mko salama.

Kama kichwa cha habari hapo juu kinavyojieleza. Nilimsikiliza kwa makini sana ndugu Msigwa wakati akiongea na wanahabari kuhusu kuomba msamaha kwa Kinana dhidi ya tuhuma za ujangili alizozitoa bungeni. Katika maelezo yake, mambo mawili niliweza kuyadadavua: (a) Kama tuhuma zilikwa siyo zaukweli, he is really a low-IQ political leader ever, na (b) kama zilikuwa na ukweli, basi kuna dili limechezwa kati ya hawa watu wawili kulinda maslahi yao.

Kwanini Msigwa nimemuita a low-IQ political leader ever? Kwanza kabisa na mnukuu “Katika kesi hiyo iliyosikilizwa na kuhukumiwa na jaji Zainabu Mluke, nilikutwa na hatia baada ya kushindwa kuthibitisha tuhuma zangu hizo mbele ya mahakama. Leo nakiri mbele yenu, kupitia ninyi mbele ya watanzania kwamba, tuhuma hizo nilizozitoa mara kadha dhidi ya Kinana, hazikuwa na ukweli wala ushahidi wowote, taarifa nilizopewa nakuzitumia hazikuwa na ukweli bali malengo potofu ya kisiasa na kizandiki. Nachukua full responsibility, kwa sababu mimi nilikuwa waziri kivuli, nilipaswa nifanye homework yakutosha pamoja na kwamba taarifa hizo nilipewa na mtu ninayemuamini”………

Kwanza nilianza kwa kutafiti ili nijue kiwango cha elimu cha msigwa, nkaipata CV yake ambayo inaonyesha, Msigwa ana shahanda ya kwanza (Theology) 2004-2007, All African Bible College, Durban, Kwazulu Natal, South Africa (ABBC-Durban). Hii ndiyo elimu ya juu aliyonayo ndugu Msigwa kwasasa. Kwa kiwango hiki cha elimu, na wadhifa wa uongozi aliokuwa nao (waziri kivuli-mali asili na utalii), siamini kama kweli alikuwa hajui kama hauna nyaraka za kuthibitisha unachokisema, utakuwa unaudangaya umma.

Isitoshe, sina uhakika kama Msigwa hakujua kuwa kauli zake hizo tayari zimeathiri reputation yake (Hapa na maana ya kwamba, Msigwa atakuwa na ujasiri gani tena wa kuuambia umma kwa jambo lolote lile?). Hii inafanana na tuhuma za ufasidi walizompa Lowasa, baadae hao hao wakamsafisha akawa tena siyo fisadi, na jambo hili (political gambling), imeathiri taswila ya chama mpaka leo. Upeo wa kufikiria wa Msigwa hapa ulikuwa mdogo sana, inaonekana maslahi binafsi yalitawala bila kufikilia kwa kina ni kwa kiwango gani hizi kauli zinaenda kuiathiri his political career.

Msigwa alitakiwa ajifunze kwa Dr. Slaa, mzee huyo alikuwa akiambatana na nyaraka kwa kila tuhuma aliyokuwa akiitoa kwa serikali au mtu binafsi. Hapa naona thamani ya mzee Slaa ndani ya CDM. Kutokuwepo kwa mzee huyu, chama kimekosa watu weledi na focus ya c hama iko dilemma mpaka leo. It is time to go back to the drawing board, au Chama kitafute mathink tank wapya.

Hawa wawili (Msigwa na Kinana), kunauwezekano wamekula dili pamoja. Inawezekana ushindi wa Kinana uliambatana na Msigwa kutakiwa kumlipa Kinana findia ya kumchafua, na inawezekana ni hela ndefu sana ambayo msigwa ilimshinda kuilipa (just my speculation), ndiyo ikampa kinana fulsa ya kumwambia Msigwa amsafishe mbele ya umma (you scratch my back I scratch yours).

Nawasilisha kwa majadiliano

Kejuu
Labda ndiyo Kinana anakaribishwa CDM
 
"Mchngaji" Peter Msigwa si tu amejichafua, lakini ile kitu wazungu wanaita intergrity, imeporomoka mmpaka sifuri.
Angalia vizuri "Mchungaji" nimewekea inverted comms kuonyesha kuwa hata hadhi ya kulisha kondoo sasa hana, hawezi kuwa mwongo na akawa mchungaji wa kanisa lolote la Kikristo.
Mtu mwongo n muuaji.
Msigwa alipata wapi ujasiri wa kuongea unsubstantiated claims ambazo zingepelekea kuumizwa au kuuwawa kwa Nd Kinana?
Amri moja ya Mungu kati ya zile kumi: "USIMSHUHUDIE MTU UONGO"

Katika hili Msigwa amefeli, na kalazimishwa kukiri kutokana na amri za kimahakama, otherwise angeishi na uongo huo dama dumu.
Tatizo siyo msigwa, tatizo mfumo wa kutafuta info wa makamanda ulimuingiza chaka na sidhan km unajitendea haki kufikia hatua ya kumuita muuaji.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu achana na utamaduni wa Mabeberu!! Africa kusema uwongo sio tatizo ni utamaduni wetu.

1 . Tuliambiwa ndege ingefuata dawa Madagascar lakini baadaye tukaambiwa sio dawa ni malighafi kwenye utafiti.
2. Tuliambiwa tz haikuhudhuri mkutano wa EAC kwa sababu haikualikwa lakini baadaye waziri wa Rwanda alidai taarifa ilitolewa ila tuligoma kwenda.
Mkuu tambua kuna uwongo mzuri wenye faida na usio na faida. Huu uwongo hapa kwetu tz unafaida.
 
Tatizo siyo msigwa, tatizo mfumo wa kutafuta info wa makamanda ulimuingiza chaka na sidhan km unajitendea haki kufikia hatua ya kumuita muuaji.

Sent using Jamii Forums mobile app
MWONGO NI MUUAJI!
Leo Kariakoo ni kiasi cha mtu kupiga kelele MWIZI...MWIZI...!
Na kama utadumu na roho yako kwa dk 20 unabahati.
Msigwa ndicho alichofanya lakini hakufanikiwa.
 
Kumbe kuna mchezo wa kuhalalisha matatizo yasiyokuwepo ili kutafuta sifa binafsi za kijinga jinga hv.watanzania wanahitaji umakini wa hali ya juu.
 
Matatizo ndani ya chama chochote cha siasa huwa yanasababishwa na ukosefu wa adabu na ujanja ujanja wa kijinga wa baadhi ya wanachama kuona wao wanajua sana kuliko wangine,hoja inapoletwa mezani hasa ile inayotilia shaka mienendo na uvunjaji wa sheria na kanuni zinazo ongoza chama ni vema sana ikatiliwa maanani na si kuidharau,siku zote ukweli huwa una tabia ya kuchelewa na ukifika watu huumbuka na hata wasijue wapi kwa kuweka sura zao,na badala yake watu hubaki kuwa kama kituko fulani kwenye jamii,tukumbuke ss sote kwamba siasa zetu bado ni changa sana na hivyo basi zinahitaji msingi ulio bora ili ziweze kukomaa na kuleta maendeleo ya kweli katika jamii zetu na taifa kwa ujumla.hivyo basi hatutafanikiwa kamwe kwa kuendelea kujenga siasa zetu kwenye msingi wa Uongo na kuuweka ukweli pembeni,jamii zetu zitaendelea kuishi ktk umaskini wa mali na fikra hata wasijue wanasimama wapi ili kulipigania taifa.
 
Back
Top Bottom