Kama tunapokea msaada wa kuondoa umasikini ina maana tunakiri kuwa Nchini tuna Watu Masikini? Je Masikini hao nao wanatozwa tozo au wanapewa unafuu?

Kama tunapokea msaada wa kuondoa umasikini ina maana tunakiri kuwa Nchini tuna Watu Masikini? Je Masikini hao nao wanatozwa tozo au wanapewa unafuu?

May Day

JF-Expert Member
Joined
May 18, 2018
Posts
6,311
Reaction score
9,027

Sweden grants 100bn/- for fund TASAF Phase II - IPP Media

https://www.ippmedia.com › news › sweden-grants-100...
Nimeona kama Nchi tumepokea Msaada kwa ajili ya Mpango wa kupunguza umasikini Nchini.

Hii inamaanisha ya kuwa kama Serikali tunakiri ya kuwa Sehemu ya Wananchi wetu ni Masikini na Wanahitaji Msaada.

Kama ndivyo ni vipi tena kutoka Serikali hiyohiyo tunaaminishana ya kuwa Watanzania wote tuna uwezo wa kulipa tozo kupitia miamala?

Je, ni kwamba Viongozi wetu Serikalini hawazungumzi lugha moja? wapo wanaoamini kuna Masikini na wapo wanaoamini ya kuwa Wote wana mapato?.

Je, Serikali ya Sweden inajua ya kuwa Masikini wetu wana uwezo wa kulipa tozo?.

Ndio kusema 'Masikini' huyu akipokea kiasi cha shilingi elfu ishirini ya kumuondolea Umasikini iwapo atatumia mtandao kuhamisha pesa hiyo itapunguzwa na Serikali hiyohiyo iliyoamthibitisha kuwa yeye ni Masikini, na hiyo 20000 waliyompa wanaamini ni kubwa sana kwake na inafaa kupunguzwa kama tunavyowapunguzia kina Bakhresa na Mo Dewji?.
 
Tanzania haijawahi kumpata kiongozi mwenye uwezo wa kupunguza umasikini kwa watu wake.Ripoti zinadai Tanzania Kila mwaka inazalisha masikini na hii ni kutokana na viongozi wetu kutokua na mikakati na sera nzuri za kiuchumi.
 
Mkitaka Mambo yanyooke badilini CCM ikae kando mtaona unafuu wa maisha
 
Tozo ya uzalendo haina macho ndugu, hadi zile nyumba mbavu za mbwa kule vijijini zinapigwa kodi ya jengo kupitia malipo ya LUKU...
 
TASAF wanatoa mpaka elf 8 kwa kaya masikini, sijui itasaidia nini?
Sasa ndio najiuliza huyu Mtu anayeidhinishwa kabisa na Serikali kwamba ni Masikini na anapewa 8000, inakuwaje tena hawa Mabilionea wa Serikalini wanapata kiburi cha kupiga debe kwamba Watanzania wana uwezo na wanaridhia kukatwa pesa zao?.

Yaani kuna Mtu kabisa anafikiri anatumia akili zake kwa kuamini ya kuwa ni sawa na haki kuwakata pesa kundi moja la Masikini ili kwenda kuwajengea Masikini wengine barabara na Zahatati?.
 
Sasa ndio najiuliza huyu Mtu anayeidhinishwa kabisa na Serikali kwamba ni Masikini na anapewa 8000, inakuwaje tena hawa Mabilionea wa Serikalini wanapata wapi kiburi cha kupiga debe kwamba Watanzania wana uwezo na wanaridhia kukatwa pesa zao?.

Yaani kuna Mtu kabisa anafikiri anatumia akili zake kwa kuamini ya kuwa ni sawa na haki kuwakata pesa kundi moja la Masikini ili kwenda kuwajengea Masikini wengine barabara na Zahatati.
Anaye fanya hivyo mshahara wake haukatwi kodi na wala hajui bei ya vitu sokoni maana analetewa kila kitu
 
Unafuu upo kwenye kuwajengea uwezo,ukiona ana mudu kufanya miamala zaidi ya buku basi sio maskini.

Waziri kasema wamebaini miamala mil.29-30 daily ina transact kwenye buku and below sasa hao hawakatwi tozo.
 
Back
Top Bottom