Kama tunataka Katiba Mpya, Tusiionee "Haya" Haki ya awaye yote

Kama tunataka Katiba Mpya, Tusiionee "Haya" Haki ya awaye yote

brazaj

JF-Expert Member
Joined
Jul 26, 2016
Posts
31,698
Reaction score
41,733
Haki za binadamu zikiwamo za kuishi, usalama, kulindwa, kujilinda, kusikilizwa n.k, si hisani. Anasema beberu: "Human rights aren't negotiable."

Hizo haziombwi. Zaidi sana anasema beberu: "Human rights are enforceable."

Tunataka Katiba Mpya. Ni haki yetu. Haki hupiganiwa.

Hatuwezi kuwa ndumila kuwili katika haki. Haki ni haki hata kama kwako binafsi inaweza kuwa ni kero. Hapo ndipo mambo ya ngoswe huingia.

"Haki za wapenzi wa jinsia moja zinihusu vipi mimi au wewe usiyehusika?"

Nikiwa mhanga wa panya road, nimewahi kuandika uzi nikiitisha kujilinda ikiwamo kwa kutumia nguvu zetu wenyewe:

Dar: Panya road wavamia nyumba 24, wanne wajeruhiwa

Hii nikiamini: "katika utawala usiowajibika, mtaji wa maskini ni nguvu zake mwenyewe."

Kujilinda huku hakuna maana ya kukiuka haki za msingi za wengine:

1. Mhalifu hawezi kutambuliwa kwa macho yake, rangi yake, umbo lake, mavazi yake, ongea yake, nk.

2. Mtu atabakia kuwa mtuhumiwa hadi mahakama imkute na hatia.

3. Mtuhumiwa asikamatwe pasipo na upelelezi wa kutosha kufanyika, kuweza kumfikisha mahakamani.

CHADEMA (nawaita kwa jina) na wapigania haki wote, mnayo dhima ya kuyasemea haya wazi wazi na bila ya kuchelewa mno.

IMG_20220916_233133_436.jpg


Kigugumizi chenu kinafanya hadi wajinga sugu (wapumbavu) kujinasibu kuwa wana hoja.

Panya road ni nani?

Kwa hakika hata aliyetokomea na kina Ben, Lijenje, Azory na kuweka watu kwenye viroba naye ni panya road tu!
 
Umafia ambao hufanywa na system kwa kigezo Cha maslahi ya taifa kumbe kwa maslahi binafsi ya watawala ni mbaya Sana Kama wafanyavyo Panyaroad kwa maslahi ya kipato kwa njia haramu
 
Umafia ambao hufanywa na system kwa kigezo Cha maslahi ya taifa kumbe kwa maslahi binafsi ya watawala ni mbaya Sana Kama wafanyavyo Panyaroad kwa maslahi ya kipato kwa njia haramu

Ni lazima kuwawajibisha panya road:

1. Wako wapi Ben, Lijenje, Azory?
2. Nani walikuwa kwenye viroba?
3. Nani walipanga kumwua Lissu?
4. Nani walipanga kumwua Mwakyembe?
5. Nani walipanga kumwua Mangula?
6. Nk, nk.

Orodha ni ndefu na haina mwisho.

NInakazia: Haki za awaye yote ni haki, kulindwa kwake hakuna mjadala.
 
Kumbe! Umenitoa usingizini mleta mada. Kunya anye kuku, akinya bata kaharisha.

Uovu unaofanywa na serikali dhidi ya wapigania demokrasia unaitwa maslahi ya taifa. Uovu unaofanywa na wapigania tumbo dhidi ya wenye nacho unaitwa uhalifu.

Uovu ni uovu tu.
 
Kumbe! Umenitoa usingizini mleta mada. Kunya anye kuku, akinya bata kaharisha.

Uovu unaofanywa na serikali dhidi ya wapigania demokrasia unaitwa maslahi ya taifa. Uovu unaofanywa na wapigania tumbo dhidi ya wenye nacho unaitwa uhalifu.

Uovu ni uovu tu.

Tunahitaji sauti au chama kitakachokuwa mstari wa mbele kuukemea uhalifu wote bayana na bila kusubiri.

Tutofautishe siasa na haki za binadamu.

Haki za binadamu haziwezi kuwa kwenye mjadala.
 
Safari yetu bado ndefu sana, tunataka sheria zivunjwe pale polisi wanapokamata panyarodi, lakini hatutaki watawala wavunje sheria wanapokataza mikutano ya hadhara kwa vyama vya siasa, huku wao wakiendelea kuzurura mikoani.

Kumbe hizi haki wakati mwingine zinaweza kukurera lakini ndio inabidi uvumilie, kama ambavyo watawala watakerwa siku ambayo wapinzani wataanza mikutano yao ya kisiasa, ndivyo ambavyo, wengine watakerwa pale ambapo panyarodi watakamatwa na kupelekwa mahakamani, badala ya kuchukuliwa sheria mkononi.
 
Safari yetu bado ndefu sana, tunataka sheria zivunjwe pale polisi wanapokamata panyarodi, lakini hatutaki watawala wavunje sheria wanapokataza mikutano ya hadhara kwa vyama vya siasa, huku wao wakiendelea kuzurura mikoani.

Kumbe hizi haki wakati mwingine zinaweza kukurera lakini ndio inabidi uvumilie, kama ambavyo watawala watakerwa siku ambayo wapinzani wataanza mikutano yao ya kisiasa, ndivyo ambavyo, wengine watakerwa pale ambapo panyarodi watakamatwa na kupelekwa mahakamani, badala ya kuchukuliwa sheria mkononi.

Kwa hakika tuna jamii ya kushangaza sana. Anaeleweka Ulimwengu anapotahadharisha:

IMG_20220914_180443_804.jpg


Mheshimiwa Mbowe aliliangazia hili pia.

Inawezekana vipi kudai haki zako kama hauheshimu za wengine?

Kwamba ni mkuki kwa nguruwe tu?
 
Back
Top Bottom