Kama ulitarajia Yanga kushinda basi hujui mpira

Kama ulitarajia Yanga kushinda basi hujui mpira

Mutangi

Senior Member
Joined
Oct 13, 2020
Posts
128
Reaction score
248
Japo wakati mwingine mpira unakuwa na matokeo ya kushangaza lakini kuna wakati lazima uonyeshe uwezo ili uweze kuwa bingwa. Yanga wametembelea ngekewa hadi kufika fainali. Kwanza kucheza shirikisho halikuwa lengo lao wakati msimu unaanza. Lengo lilikuwa kucheza Champions league ambapo tangu karne ya 21 ianze hawajui michuano hii inafananaje. Kwa sababu ya uwezo mdogo wakatolewa wakaangukia shirikisho.

Ukiangalia njia waliyopitia hadi kufika final unaona kabisa walikuwa wanakutana na timu mbovu. Hawa waarabu tangu mashindano yaanze hawajawahi kushinda ugenini ila leo wamemfunga yanga ugenini. Tena ni vile tu walicheza kwa kujihami lakini ni dhahiri kuwa wakitaka kufunga anytime wanaenda wanafunga.

Kwa mtu wa mpira hapaswi kuumia japo kufungwa inauma. Hatua waliyofika msimu huu ni kubwa sana kwa upande wao, ni hatua ambayo hawajawahi kuifikia. Swali la kujiuliza ni je wataweza kufika huko kwenye msimu unaokuja? Kama msimu huu umefika fainali maana yake msimu unaofuata usipofika final unakuwa umeunderperform.

Mashabiki wa yanga wanaona Champions league haina tofauti na confederation. Wanaona Simba kutolewa robo fainali na bingwa mtetezi ni udhaifu kwa simba. Mimi natamani msimu ujao yanga wafuzu kucheza Champions league tuone kama watafika hata hiyo robo.

Mwsho kabisa niwashukuru waarabu kwa kutuletea utulivu, maana hali ilikuwa ngumu, kelele zilikuwa nyingi mno.
 
Hata hivyo sisi kama Simba viongozi wetu ndo shida, Kuna wachezaji wengi wazuri Kwa Nini hatusajili tuochukua magalasa
Na kukumbatia wachezaji wazee. Labda super league itawaamsha usingizini, ngoja tuone.
 
Japo wakati mwingine mpira unakuwa na matokeo ya kushangaza lakini kuna wakati lazima uonyeshe uwezo ili uweze kuwa bingwa. Yanga wametembelea ngekewa hadi kufika fainali. Kwanza kucheza shirikisho halikuwa lengo lao wakati msimu unaanza. Lengo lilikuwa kucheza Champions league ambapo tangu karne ya 21 ianze hawajui michuano hii inafananaje. Kwa sababu ya uwezo mdogo wakatolewa wakaangukia shirikisho.

Ukiangalia njia waliyopitia hadi kufika final unaona kabisa walikuwa wanakutana na timu mbovu. Hawa waarabu tangu mashindano yaanze hawajawahi kushinda ugenini ila leo wamemfunga yanga ugenini. Tena ni vile tu walicheza kwa kujihami lakini ni dhahiri kuwa wakitaka kufunga anytime wanaenda wanafunga.

Kwa mtu wa mpira hapaswi kuumia japo kufungwa inauma. Hatua waliyofika msimu huu ni kubwa sana kwa upande wao, ni hatua ambayo hawajawahi kuifikia. Swali la kujiuliza ni je wataweza kufika huko kwenye msimu unaokuja? Kama msimu huu umefika fainali maana yake msimu unaofuata usipofika final unakuwa umeunderperform.

Mashabiki wa yanga wanaona Champions league haina tofauti na confederation. Wanaona Simba kutolewa robo fainali na bingwa mtetezi ni udhaifu kwa simba. Mimi natamani msimu ujao yanga wafuzu kucheza Champions league tuone kama watafika hata hiyo robo.

Mwsho kabisa niwashukuru waarabu kwa kutuletea utulivu, maana hali ilikuwa ngumu, kelele zilikuwa nyingi mno.
Mlikjwa mnagugumia maumivu chinichini..

Kuna ubingwa wa Ligi na Azam cc na Medali au ubingwa wa caf cc.

Endelea kjgugumia maumivu tu
 
Yanga amepambana simba alishindwa kufika hatua hii
 
" Kwanza kucheza shirikisho halikuwa lengo lao wakati msimu unaanza, lengo lilikuwa wacheze champions league ambapo tangu karne ya 21 ianze hawajui michuano hii inafananaje "
 
Ilikuwa ni ngumu sana kwa yanga kushinda gemu ya leo, kwa sababu alikuwa anacheza kutafuta matokeo wakati huo huo akijilinda, i guess kilichotokea leo kwa wanayanga ndicho kitaenda ku happen kwa hawa ndugu zetu waarabu.
 
Ilikuwa ni ngumu sana kwa yanga kushinda gemu ya leo, kwa sababu alikuwa anacheza kutafuta matokeo wakati huo huo akijilinda, i guess kilichotokea leo kwa wanayanga ndicho kitaenda ku happen kwa hawa ndugu zetu waarabu.
Tusubiri tuone
 
Ilikuwa ni ngumu sana kwa yanga kushinda gemu ya leo, kwa sababu alikuwa anacheza kutafuta matokeo wakati huo huo akijilinda, i guess kilichotokea leo kwa wanayanga ndicho kitaenda ku happen kwa hawa ndugu zetu waarabu.
Wale hawana cha kupotezaaa, kule wao ni mashambulizi mwanzo mwengaaaaaa
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]

Mtaonaaaaa
 
Back
Top Bottom