Hakuna kosa hapo, watawaachia muda si mrefu, kama vile Kitimoto kuna watu hawali na wengine wanakula 😂Hii kisheria imekaaje?
Mteja amekuja akauliza mishkaki kiasi gani, ukamjibu 100. Akaamua kununua bila kuuliza nyama ya mnyama gani.
Apo muuzaji kosa lake lipo wapi endapo akajitetea kuwa mnunuaji hakuuliza ni nyama ipi.
Dini safi halafu mwezi wa mfungo, nini lengo laoHamza Rajabu (20), Omary Mohamed (12) na Mussa Juma (30)
Kwa taarifa yako ni kwamba wapo wanaouza mishkaki ya nyani sana tu labda wahusika hawajafuatilia, endeni pembezoni mwa mji pelelezi mtaambiwaNi mnyama ambaye amekuwa akitumia nyama kama chakula chake kikuu. Pamoja na kuwa na sifa hizo, miaka ya zamani mnyama huyo alikuwa akitumiwa kama kitoweo na kabila moja maarufu hapa nchini.
Hata hivyo, mkoani Morogoro suala la mbwa kuwa kitoweo ni jambo geni na si utamaduni wa makabila yaliyopo mkoani hapa kutumia nyama ya mbwa kama chakula ama kitoweo.
Recently kuna jamaa anaitwa manati alitengeneza supu ya mnyama akapika na matofuKwani wananchi wa Tanangozi, iringa wao wanasemaje?
Yaani hata kama ni ugumu wa hela sio kwa hawa jamaa!Hata hivyo, mkoani Morogoro suala la mbwa kuwa kitoweo ni jambo geni na si utamaduni wa makabila yaliyopo mkoani hapa kutumia nyama ya mbwa kama chakula ama kitoweo.
Baadhi ya wananchi wa Manispaa ya Morogoro wamelaani vikali kitendo cha baadhi ya wauza mishikaki ndani ya manispaa hiyo kutumia nyama ya mbwa kama mishikaki na kuiomba Serikali kufanya uchunguzi ili kuwabaini wauzaji hao, ikiwa ni pamoja na kuwachukulia hatua za kisheria.
Kuonyesha ukweli wa madai yao, Aprili 26, 2021 katika daraja kuu la barabara iendayo Iringa eneo la Relini, wananchi waliokuwa wakipita njia waliwakuta vijana watatu wanaodaiwa ni wauzaji mishikaki nje ya kituo cha mabasi yaendayo mikoani cha Msamvu Morogoro wakiwa wanachuna ngozi ya mbwa.
Walisema waliwaona vijana hao wakichuna mnyama lakini hawakujua kama ni mbwa, kilichowashtua ni pale walipoona pembeni kichwa cha mbwa, ndipo walipowafuata na wao kuonyesha mashaka, waliwakamata na kuwahoji na baadaye kuwapeleka kituo cha Polisi Msamvu, na baadaye watuhumiwa hao kuhamishiwa kituo kikuu cha Polisi Morogoro.
Mkazi wa Mafisa, Anold Alexanda alisema ni jambo la kushangaza kukuta wauza mishikaki wakitenda jambo hilo, kwani wanaondoa imani ya watu kuendelea kula nyama maeneo ya Msamvu.
“Hawa watu wanafahamika kwa uuzaji wa mishikaki hasa majira ya usiku, ndio wamekuwa wakiuza mara nyingi, unawakuta pale Puma kituo cha mafuta na Dodoma stendi. Watu tunakula na wanatuuzia mishkaki bila hata kujua kama ni ya mbwa ama la,” alisema Alexanda.
“Mimi ni mtumiaji mkubwa wa mishikaki na nimekuwa nikienda mara kwa mara wanapouzia, kiukweli wamenihuzunisha, ninachoomba hatua kali zichukuliwe dhidi yao,” aliongeza.
Dereva wa bodaboda eneo la Msamvu ndani, Abdallah Pawa alisema kwa tukio hilo, Serikali iwachukulie hatua kwa kuwalisha watu nyama za mbwa bila ridhaa yao. Aliwashauri wauza chakula katika maeneo mbalimbali manispaa ya Morogoro kuwa makini, waaminifu na maeneo wanayonunua nyama waepukane na nyama za kununua mitaani katika sehemu zisizofahamika.
“Tumesikia mmoja wao hao vijana ni wakala mkubwa wa wauza nyama za mishikaki hasa ya ile ya mia mia, kinachotakiwa ni kuepuka nyama za kununua mitaani, sio kila nyama unayoletewa unanunua, unatakiwa kuchukua nyama sehemu sahihi ukijua hii ni nyama ya mnyama fulani,” alisema.
Mfanyakazi wa stendi ya Msamvu, Samson Jonas alisema: “Idadi ya watu wanaoingia na kutoka hapa Msamvu ni wengi, huyu jamaa ni muuaji na atafanya wale wafanyabiashara wa mishikaki kukosa wateja, kwani si wote wanaouza nyama ya mbwa, wapo wanaouza mishikaki ya ng’ombe, mbuzi ama kuku.
“Hata sasa ukienda buchani lazima uangalie kwato kama nyama iliyopo ni mbuzi, ng’ombe ili ununue, sasa hivi watu wameshtuka, huyu jamaa katuumiza sana kiukweli,” aliongeza Jonas.
Muuza chipsi Mussa Said maarufu kama dokta Shiba alisema ameumia kama mfanyabishara kwa taarifa hiyo, na kuwataka wateja kuondokana na hofu hiyo kwani chakula kinachouzwa ndani ya kituo cha mabasi Msamvu ni salama. Kamanda wa polisi mkoa wa Morogoro, Fotunatus Muslimu alipoulizwa juu ya kuwepo kwa tukio hilo, alikiri kukamatwa kwa watuhumiwa watatu na kwamba wanafanyiwa mahojiano.
Waliokamatwa kutokana na tuhuma hizo za kukutwa wakichuna ngozi ya mbwa na kudai kuwa ni wauzaji mishikaki ni Hamza Rajabu (20), Omary Mohamed (12) wote wakazi wa Msamvu na Mussa Juma (30) mkazi wa Mtawala.
MWANANCHI
Utakuwa mteja mjinga. Mishikaki ya kuku na ng’ombe hata bei hutofautiana. Unakula mshikaki wa 100 unategemea uwe wa ng’ombe au kuku? Na mishikaki ya mbuzi wala siyo maarufu kihivyo. Kama hutaki hata kuuliza mishikaki ni ya nini, basi wewe ni mla mbwa.Hii kisheria imekaaje?
Mteja amekuja akauliza mishkaki kiasi gani, ukamjibu 100. Akaamua kununua bila kuuliza nyama ya mnyama gani.
Apo muuzaji kosa lake lipo wapi endapo akajitetea kuwa mnunuaji hakuuliza ni nyama ipi.
Ifinono twilyage mbetuli....Wahehe mnasemaje?
Daaa ..kenge mbona ngumu Sana kumpataDah isijekuwa na ya Masika nayo ni idog daaah, kuna kipindi walisema mishkaki ya urojo wa Baba Amina ni ya kenge daah
Haahaaa[emoji16][emoji16] mi vyakula vya njiani vyote huwa moyo unastuka sanaNimekoma
Ila kuku si anajulikana jamani [emoji23][emoji23] au nae Kuna mbadala wake
Inaotesha nywele matakoniMimi nataka kujua madhala ya kula mbwa tuanzie kwanza hapo?
Unakulaje nyama za kuokoteza barabarani ?Mbwa ni mnyama ambaye amekuwa akitumiwa na binadamu kwa muda mrefu kwa ajili ya ulinzi katika maeneo mbalimbali, ikiwamo majumbani.
Ni mnyama ambaye amekuwa akitumia nyama kama chakula chake kikuu. Pamoja na kuwa na sifa hizo, miaka ya zamani mnyama huyo alikuwa akitumiwa kama kitoweo na kabila moja maarufu hapa nchini.
Hata hivyo, mkoani Morogoro suala la mbwa kuwa kitoweo ni jambo geni na si utamaduni wa makabila yaliyopo mkoani hapa kutumia nyama ya mbwa kama chakula ama kitoweo.
Baadhi ya wananchi wa Manispaa ya Morogoro wamelaani vikali kitendo cha baadhi ya wauza mishikaki ndani ya manispaa hiyo kutumia nyama ya mbwa kama mishikaki na kuiomba Serikali kufanya uchunguzi ili kuwabaini wauzaji hao, ikiwa ni pamoja na kuwachukulia hatua za kisheria.
Kuonyesha ukweli wa madai yao, Aprili 26, 2021 katika daraja kuu la barabara iendayo Iringa eneo la Relini, wananchi waliokuwa wakipita njia waliwakuta vijana watatu wanaodaiwa ni wauzaji mishikaki nje ya kituo cha mabasi yaendayo mikoani cha Msamvu Morogoro wakiwa wanachuna ngozi ya mbwa.
Walisema waliwaona vijana hao wakichuna mnyama lakini hawakujua kama ni mbwa, kilichowashtua ni pale walipoona pembeni kichwa cha mbwa, ndipo walipowafuata na wao kuonyesha mashaka, waliwakamata na kuwahoji na baadaye kuwapeleka kituo cha Polisi Msamvu, na baadaye watuhumiwa hao kuhamishiwa kituo kikuu cha Polisi Morogoro.
Mkazi wa Mafisa, Anold Alexanda alisema ni jambo la kushangaza kukuta wauza mishikaki wakitenda jambo hilo, kwani wanaondoa imani ya watu kuendelea kula nyama maeneo ya Msamvu.
“Hawa watu wanafahamika kwa uuzaji wa mishikaki hasa majira ya usiku, ndio wamekuwa wakiuza mara nyingi, unawakuta pale Puma kituo cha mafuta na Dodoma stendi. Watu tunakula na wanatuuzia mishkaki bila hata kujua kama ni ya mbwa ama la,” alisema Alexanda.
“Mimi ni mtumiaji mkubwa wa mishikaki na nimekuwa nikienda mara kwa mara wanapouzia, kiukweli wamenihuzunisha, ninachoomba hatua kali zichukuliwe dhidi yao,” aliongeza.
Dereva wa bodaboda eneo la Msamvu ndani, Abdallah Pawa alisema kwa tukio hilo, Serikali iwachukulie hatua kwa kuwalisha watu nyama za mbwa bila ridhaa yao. Aliwashauri wauza chakula katika maeneo mbalimbali manispaa ya Morogoro kuwa makini, waaminifu na maeneo wanayonunua nyama waepukane na nyama za kununua mitaani katika sehemu zisizofahamika.
“Tumesikia mmoja wao hao vijana ni wakala mkubwa wa wauza nyama za mishikaki hasa ya ile ya mia mia, kinachotakiwa ni kuepuka nyama za kununua mitaani, sio kila nyama unayoletewa unanunua, unatakiwa kuchukua nyama sehemu sahihi ukijua hii ni nyama ya mnyama fulani,” alisema.
Mfanyakazi wa stendi ya Msamvu, Samson Jonas alisema: “Idadi ya watu wanaoingia na kutoka hapa Msamvu ni wengi, huyu jamaa ni muuaji na atafanya wale wafanyabiashara wa mishikaki kukosa wateja, kwani si wote wanaouza nyama ya mbwa, wapo wanaouza mishikaki ya ng’ombe, mbuzi ama kuku.
“Hata sasa ukienda buchani lazima uangalie kwato kama nyama iliyopo ni mbuzi, ng’ombe ili ununue, sasa hivi watu wameshtuka, huyu jamaa katuumiza sana kiukweli,” aliongeza Jonas.
Muuza chipsi Mussa Said maarufu kama dokta Shiba alisema ameumia kama mfanyabishara kwa taarifa hiyo, na kuwataka wateja kuondokana na hofu hiyo kwani chakula kinachouzwa ndani ya kituo cha mabasi Msamvu ni salama.
Kamanda wa polisi mkoa wa Morogoro, Fotunatus Muslimu alipoulizwa juu ya kuwepo kwa tukio hilo, alikiri kukamatwa kwa watuhumiwa watatu na kwamba wanafanyiwa mahojiano.
Waliokamatwa kutokana na tuhuma hizo za kukutwa wakichuna ngozi ya mbwa na kudai kuwa ni wauzaji mishikaki ni Hamza Rajabu (20), Omary Mohamed (12) wote wakazi wa Msamvu na Mussa Juma (30) mkazi wa Mtawala.
Kwa maeneo unayoishi inawezekana ikawa ngumu ila hapa kitaa tunapishana nao kama wana tu.Daaa ..kenge mbona ngumu Sana kumpata
mzee piga tuu.. hata ukipata Punda peleka tuuMbwa kafanana na mbuzi kiumbo kwa hio hata laza zitakua mule mule.. Haya mambo ya kuchagua kitoweo cjui tumetoa wapi