Kama umewahi kushuhudia live nguvu za giza pita hapa uweke ushuhuda wako

Kama umewahi kushuhudia live nguvu za giza pita hapa uweke ushuhuda wako

anayesema uchawi muongo labda awe amezaliwa marekani.
kisa changu cha mwisho ni kipindi nafanya kazi nida kama IT kabla wakati huo hatujapunguzwa na wengine kibarua kuota nyasi.

Tulipendekezwa majina yetu toka juu,kuwa tunatakiwa kwenda kilwa na mafia kwa ajili ya kuandikisha watu kwenye vitambulisho vya taifa,cha ajabu wafanyakazi wenzetu watano waligoma kata kata kiasi cha kuwa radhi hata kuacha kazi,ki upande wangu nilishangaa kwanin lakini sababu yao kubwa ni kwamba wana alleg na kupanda ndege vile videge vidogo[emoji3][emoji3][emoji3][emoji3],tuliwacheka sana na kuwaona washamba maana wengi ndo tulikuwa tumetoka fresh from school(ujana maji ya moto)

Wenyewe siku ya safari hao nakumbuka tulikodiwa ndege kabisa na nida mfkoni tumepewa pesa ya kutosha,naweza kusema kuwa kilwa na swhemu yenye maskini mno na maisha duni kwa kipindi kile sijui sasa hivi,tuliingia wenyewe na wenzetu wanawake walikuwa masista duu kweli kweli uzungu mwingi,tumekuja wenyewe kupokewa na pick up ya halmashauri hao mpka ofisini,kufika pale tukapewa intro kuhusu kilwa na mtu (XXXX)aisee upande wangu amani ikanitoka kabisa ikafikia hatua nikataka kusema jamani kama vipi nirudi tu dar safari hii na mimi nkawa nachekwa na wenzangu,yule mtu (XXX)mwenyeji wetu akasema kesho kuna wazee atatukutanisha nao kwa ajili kwa ajili ya utambulisho hao tukapelekwa guest hizo gest sasa

[emoji3][emoji3][emoji3] ni kama nyumba zile za zanzibar(magofu)sasa kuna jamaa zangu wa arusha wakasema hapa hatuwezi kulala bila ya kustua,wakatoka wakaenda zao club piga sana pombe sasa ili wasilale na pombe ikabidi wapitie buchani ili na wale wafanyakazi wengne wa kike wakifika wachemshe supu nyinginge wanywe usiku ule ule na nyingne wapike asubuhi,

walirudi saa 8 usiku maana sisi ambao si wanywaji hatukwenda walivyorudi wenyewe wakapika supu nusu ile nusu nyngne wakachmsha watakula asubuhi.Mwenyewe ndo nlikuwa wa kwanza kuamka asubuhi naamka naangalia kwenye sufuria nakuta ngozi ya nyani na vidole vimekatwa katwa vizuri,nkawaamsha jamaa kuja kuona hivi acha waanze kutapika maana hang over zilikata wengine wakapandwa na hasira wakatoka kwenda buchani kulianzisha kufika pale buchani wakakutana na nyumba ya udongo (boma)ambayo haishi mtu,sasa wale wa dada wakaanza kulia na wengne kutaka hata kurudi dar piga simu dar tunaambiwa ndege ni mpka next week,

kufupisha tu story tulikaa siku 3 mashine hazifanyi kazi, nakumbuka siku ya 3 ote tulijikuta tumelala nje na viboxa vyetu,wenye night dress[emoji3][emoji3][emoji3][emoji3][emoji3],yalikuja kuisha baada ya kukutana na wazee wa mji na kutupa ruksa ambayo ilitolewa na mzee(XXX) wa kilwa.

uchawi upo nmeficha mambo mengi sababu mnaweza kuunganisha dot mkawajua wahusika

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Naona pm kumejaa[emoji23][emoji23]
Kuna jamaa angu alifumaniwa na mke wake,ugomvi ulikua mkubwa kiasi ya kwamba mwanamke alishaanza kufungasha mizigo yake aondoke,jamaa alichofanya alimpgia mtalaam wake simu aisee,baada ya masaa 5 mwanamke amesahau kila kitu,hali ikawa shwari


Sent from my iPhone using JamiiForums

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom