Crocodiletooth
JF-Expert Member
- Oct 28, 2012
- 20,561
- 24,428
Some how littly i believe you, hasa wale wanaopata comma,ikaunganika na faint hapa huwa viungo vinafanya kazi in a very low heart pulse huwa na interval ndefu,hapa daktari akiwa na papara unapigwa kwenye freezer dadek....😛Kiranga, acha kujishusha hata kama mtu, amezikwa akiwa mzima, kuna uwezekano wa kujitoa yeye mwenyewe, kaburini. Kwa dongo lile linawekwa pale, kwa Wakristo mtu huzikwa ndani ya jeneza.
Sent using Jamii Forums mobile app
Pekee yangu chumbaniMweh mweh. Unalala peke yako mu chumba au ni bwenini?
Nishawahi sikia kisa kinschohusishwa na uchawi
Kuna masela wawili walienda kwa mganga ili wapate utajiri
Mganga akawapa dawa akawaambia wakaoge usiku makaburini na wakitoka mlangoni kwa mganga hawatakiwi kugeuka nyuma
Basi unaambiwa safari yao iliandamwa na misukosuko yakutisha, mara wasikie muungurumo wa simba akiwa nyuma yao na vimbwenga vingi lakini walijitahidi kukaza ili kutovunja sharti la kugeuka nyuma
Sasa ulipofika usiku majira ya saa 8 ikabidi waende makaburini kuoga ili kumalizia zoezi lao la mwisho ili wawe mamilionea
Walipofika makaburini wakavua nguo wote nakubakia uchi kisha wakapanda juu ya kaburi ili waoge
si unajua ukiwa katika ile mood flani hivi unaoga halafu umefumba na macho ili maji yasiingie machoni.
wakastukia tu paap! wameshikwa makalio kwa nyuma.
Aaah unaambiwa wote ilibidi wageuke nyuma kwa haraka huku wanakimbia na kupiga makelele
Kesho yake kijiweni wakaanza kulaumiana "aaah wewe ndiye ulizingua, we ungekausha bila kupiga mikelele mi nisingechochora kwani kushikwa tako kitu gani bwana" yani leo nisingekua nakunywa kahawa hapa ningekua nimejikoki huko kwenye hotel zinazotambulika na dunia"
Mwaka 1989 nilikwenda kijiji cha jirani nikanywa pombe sana.Nilipokuwa narudi nikapita sehemu ambayo inasifika kwa mauza uza nikawa mbishi vile nimelewa siogopi.
Nikafika kichaka flani nikasikia nywele zimesimama nikahisi joto kali sana nikasikia harufu ya marashi mara ukawaka mwanga mkali pombe yote ikaisha.
Kesho yake nikamuhadithia bibi yangu akaniambia bahati yako pale kulikuwa na jini lipenda dini liivyoona unanuka pombe likaona ngoja huyu mchafu aende zake.
Sent using Jamii Forums mobile app
Uzi una wakongwe huu..
Kuna vijana wawili walipiga paka wa ostadhi mmoja hivi..mwenye paka akapata taarifa akawaambia waombe msamaha..kijana mmoja alikubali mmoja akagoma..yule aliyegoma alianza kutokwa na majipu mwilini wazazi wake wakamsihi akaombe msamaha lakini bado aligoma..kilichomkuta ni kupoteza maisha...yule mzee ni mchawi akikutaka uwe mpenzi wake ni dk 0 tu..
Tukio lingine Kuna kijana alijisaidia kubwa nyuma ya nyumba ya huyo mzee ostadhi alivyofika kwake akakuta ile kubwa ipo kitandani kwake.
Sent using Jamii Forums mobile app
Hili tatizo hata mimi nikiwa mdogo nilikuwa nalo, nilikuwa na miaka 6-7. Kilikuwa kinaanza usiku wa manane kuelekea alfajiri yaani kilikuwa kinauma balaa. Ila kiliacha chenyewe sijui kama wakubwa walifanya kituSalange, Mimi kwenyewe nimewahi kusumbuliwa na kuumwa sana na kichwa nikiwa na umri baina ya miaka 14-16. Kichwa kilikuwa kinauma mpaka napoteza faham. Nikipelekwa hospital hawagundui tatizo. Siku moja mshua akanipeleka kwa MZEE mmoja(mtaalam). Yule MZEE akacheki vipimo,akachukua pembe ya Ng'ombe. Akawa ananichanja chale maeneo mbalimbali ya kichwa,baadae akawa anaibana na pembe ya Ng'ombe kila chale mithili ya MTU anayebana kizibo cha bic kwenye ulimi.
Baadae pembe inaachia taratibu kisha inadondoka. Kila ikidondoka kinatolewa kijiwe cheupe mithili ya goroli. Vilitolewa vijiwe 4, tangu siku hiyo mpaka Leo hii,sijawahi sumbuliwa na kichwa. Uchawi upo,asiyeamini amuombe Mungu aendelee kumpa uhai. Maana ukiwa hujafa,hujaumbika.
Sent using Jamii Forums mobile app
Pyepyepye, Nimekusoma vizuri sana hapo kwenye mbunga aka soka. Achana kabisa na hizo mambo. Wazee wa mirambo watakuwa wanelewa hizo mambo.
Nakumbuka moja nikiwa golini jamaa walinibebesha mizizi,mingine nikatafuna aisee
Ile game ilikuwa balaa,timu yetu ilikuwa mbovu lakini tulichomoka kwa ushindi wa mbinde.
Sent using Jamii Forums mobile app
Me kuna kipindi naweza kulala nimevaa boxer nikiamka asubuhi niko uchi.
Mpaka sasa bado cjaelewa kitu, je ni nini hiyo?
Sent using Jamii Forums mobile app
Wewe hujawahi kuona maruwe ruwe?
Mzee baba uko siriaz au unatania? maana hata mie nilikuwaga siamini mambo ya kusikia, Nakumbuka siku moja nipo chuo nakula msuli kimbweta jamaa alinifata akidai hajala tangu usiku wa siku moja kabla ya jana( nimekutana nae jumatano mchana halafu akasema hajala tangu alipokula usiku wa jumatatu), nikaona kama ananipanga tu nikampa buku 2 akasepa. Ila nilikuja kufulia kuna kipindi nikawa nakoroga uji tu geto nakunywa asubuhi afu navunga mpaka usiku tena, ilifikia kipindi nikawa tena sioni haja ya uji navunga tu tangu asubuhi mpaka usiku napiga maji tu ya dawasco, ndo nikajua hakuna jipya chini ya jua.Uwongo tu na stories,pangine umevuta bangi Kama kweli uchawi unafanya kazi mlogeni Kiranga awe chizi mkiweza nilogeni na Mimi
Hayo ni mawenge tu!
Yule mzee eti kaniambia kakutana na mtu mweusi mwenye mkino mingi ya chuma upuuzi
Hakunaga uchawi shetani Wala mungu
Naami hivyo
Duuuh! ndo kali yaoHii ilimtokea Mshiakaji wangu dereva wa lori
Anatoka zake Zambia akavuka Tunduma boda, alipoona yupo Bongo akaenda kuna mahali wanalalaga madereva basi usiku mnene akasikia kama watu wanapita nje akachungulia dirishani akaona kikosi cha WANGA wanawake wako msururu, ile bado anaangalia akamuona mzee mmoja yuko kwa nyuma ndo kama anawa command, basi kufika usawa wa dirisha yule mzee akawa kama kastuka hivi akageuka upande aliko jamaa(jamaa yupo ndani) akaanza kupiga hatua akilifata dirisha, jamaa kuona hivyo akaegesha kama amelala akiskilizia nini kinafuata, Ebana yule mzee alifika akaingiza kichwa kuchungulia ndani bila kufungua dirisha huku mwili wake ukiwa nje na kichwa mpaka usawa wa mabega kaingia ndani, jamaa akakausha mzee akawacheki akaona kama wote wamelala akazepa zake.
Ukisema habari ya njombe unantisha,mwanangu anasoma hukoNipo Njombe huku!! Kuna mwanafunzi alikuwa anafanya mtihani kabla hajamaliza mkono ukaanza kuvimba ghafla hivyo ikashindikana kumalizia mtihani huo! Ikabidi tuwasiliane na Mzazi wake akasema tusimpeleke popote anakuja mwenyewe basi wakaja hapo shuleni na mchungaji baada ya maombi kama dakika 5 tu mkono ulijirudi na kuweza kuandika vizuuuuuuri! Daaa Kweli uchawi upo!! TUMWOMBE MUNGU DAIMA!!
Sent using Jamii Forums mobile app
Suala la kushikwa tako ni jingineNishawahi sikia kisa kinschohusishwa na uchawi
Kuna masela wawili walienda kwa mganga ili wapate utajiri
Mganga akawapa dawa akawaambia wakaoge usiku makaburini na wakitoka mlangoni kwa mganga hawatakiwi kugeuka nyuma
Basi unaambiwa safari yao iliandamwa na misukosuko yakutisha, mara wasikie muungurumo wa simba akiwa nyuma yao na vimbwenga vingi lakini walijitahidi kukaza ili kutovunja sharti la kugeuka nyuma
Sasa ulipofika usiku majira ya saa 8 ikabidi waende makaburini kuoga ili kumalizia zoezi lao la mwisho ili wawe mamilionea
Walipofika makaburini wakavua nguo wote nakubakia uchi kisha wakapanda juu ya kaburi ili waoge
si unajua ukiwa katika ile mood flani hivi unaoga halafu umefumba na macho ili maji yasiingie machoni.
wakastukia tu paap! wameshikwa makalio kwa nyuma.
Aaah unaambiwa wote ilibidi wageuke nyuma kwa haraka huku wanakimbia na kupiga makelele
Kesho yake kijiweni wakaanza kulaumiana "aaah wewe ndiye ulizingua, we ungekausha bila kupiga mikelele mi nisingechochora kwani kushikwa tako kitu gani bwana" yani leo nisingekua nakunywa kahawa hapa ningekua nimejikoki huko kwenye hotel zinazotambulika na dunia"
Duuu naokoka na ujambz naachaKisa kingine nilikisikia kilitokea maeneo ya sumbawanga
Kuna mzee wamakamo alikua ni tajiri sana, pesa zake haweki benk na hata akienda kufanya manunuzi hua haweki kwenye wallet kuzistiri zisionekane yeye hua anazishikilia tu kama wanafunzi wanavyoshika vitini vyao mikononi
Siku moja kuna kosi la majambazi lilijipanga kwenda kumvamia
Walimkuta yuko nyumbani kwake ameshikilia pesa akipata upepo kwenye garden yake
Wakamnyooshea bastola na kumwambia atulie kimya kisha atoe kila kitu alichonacho
Yule mzee akachukua zile pesa akazibana kwenye kwapa lake huku akitetemeka kwa woga
majambazi wakamsisitiza kua anyanyue mikono juu, mzee akatii amri kwa kunyanyua mikono juu kisha pesa alizozibana kwapani zikaanguka chini majambazi wakaziokota
Wakamwambia tena "toa kila kitu ulichonacho"
Round hii unaambiwa mzee alichomoa kichwa chake akakishika mkononi halafu kile kichwa kikiwa mkononi kikatoa sauti ikisema "sina chochote jamani nina kichwa tu hapa"