Dogo tulia hujui Kitu wwdigba sowey, Wewe ni muongo.
Umesema mwaka 92 ulikuwa umeshaanza kazi ya kufundisha halafu unasema tena mwaka 2009 ulikuwa unasomea ualimu, aisee hii chai yako imezidi tangawizi.
[emoji23][emoji23][emoji23] wengine wanazidisha adi tangawiziUzi umegeuka na kuwa wa chai sasa. Watu badala waeleze experience zao, wanaleta story za vjiweni
Sent using Jamii Forums mobile app
Umenikumbusha uchawi wa unyakyusa miaka ya 2004 pale Tukuyu kwenye kiwanja cha mpira karibu na Stendi, kulikuwa na mkesha wa mwenge sisi tumeroka
Tukuyu kulikuwa na watalaamu kipindi cha nyuma pale uwanja wa mpira Tukuyu Mjini kulikuwa na mbio za mwenge.
Kabla ngoma za asili au ling'oma halijapigwa mvua ilianza kunyesha dakika chache wazee wa mila wakaitana na wakazuia mvua.
Siku ya ling'oma kulikuwa na uchawi haswa maana kulikuwa kama na ligi ya ngoma kutoka sehemu mbalimbali, nakumbuka kuna ling'oma kutoka Bujesi hawa walikuwa wakipiga ngoma Tukuyu inasimama.
Siku nyingine nilikutana na kisa cha kukutana na vibwengo mimi na jamaa yangu kwenye mashamba ya chai Kyimbila. Alinishawishi tufate ling'oma Ushirika kulikuwa na Mashindano ya ngoma. Wakati wa kwenda tukapanda Hiace "Big Poppa". Usiku ikawa kasheshe saa 3 hakuna gari tukaamua tutembee kufika mashamba ya chai tunaona kibwengo kinatembea upande wetu kila tukisogelea kinaongeza spidi. Gafla kikapotea tunafika maeneo ya Kamangila Bar kuna mzee tukamwambia akacheka na kusema nyie ni wageni.
Visa ni vingi huko Sakura Pangani usiku mkali tupo na pikipiki mara raia yupo njia panda ile kusogeza pikipiki hakuna kitu.
Njia ya Mpanda-Sumbawanga tupo na Isuzu Kb pick up kuna raia anagonga body kama ana amrisha gari isimame na gari iko mwendo kipindi hicho njia mbovu.
Mimi n mtu wa maombi sana,huwa wanakujaga wenzangu home tunapiga story then tunaanza ku praise ku worship kisha tunazama kwenye maombi,unajua mnapoomba zile kelele sasa Tuna shout sana.
siku moja nimelala usiku nikaota kuna bibi mmoja nyumba ya jirani alinifata usiku akaanza kunirushia mawe anipige,ila kila akirusha mawe kuna mkono ulikua mbele yangu unayazuia yale mawe,yule bibi akawa anawambia wafuasi wake pigeni mawe huyo
amezoea kutupigia makelele usiku na wenzake,walirusha mawe sana mwisho wakasema na kesho tutakuja tena leo ni trela tu,hapo kumbuka nilikua ndotoni.
Palipokucha asubuhi nilikuta chumbani kumejaa mawe vipande vya matofali mawe ya kila aina,sikuamini macho yangu nilihisi naota,maana ni vingi vingi vingi.
Basi nikavikusanya nikaenda vitupa nnje,mchana umefika nikawa nataka kugongelea msumari mahali,nyundo sina nikasema asubuhi nilitupa mawe ngoja nikachukue kipande kimoja nije kugongea,kwenda pale nilitupa yale mawe Sijakuta hata kipande cha mchanga.
Pangani kulikuwa na mzee anaitwa Halichwi huyo alikuwa anaogopeka balaa, ilikuwa hakitaka jambo jua halikuchi hilo jambo linatokea.
Huyu alikuwa akiwa kwake jioni anatembea na majini yake kwenda kufata mahitaji.
Hapo Usagara Tanga mjini kuna mzee alikuwa mganga wa kitabu miaka ya nyuma kidogo kuna Kipindi alikuwa anayafungulia majini yanakuwa nje hapo karibu na kwake na njia hiyo ya Kwenda Coast Lodge.
mkuu umemaliza mwaka ganiNlikutana na vibwengo laivu bila chenga...nikiwa same secondary...aisee usiombe ukutane na Hawa jamaa...
Sent using Jamii Forums mobile app
Haahaaa dah umenichekesha umewaza kama mimiHiyo story ya mtoto aliyerudi n mikono mirefu mpaka magotini tafadhali nyosha mkanda je alikuwa anakula anaongea na alisema alikuwa wapi ?
Sent using Jamii Forums mobile app
au alitoka kwasa kwasa[emoji16]ulikua unatoka masandare kuangalia mademu ama
Hahaaa huyo mwanamke aliwaelewa wote watatu!2010 nipo ndani ya fuso, natokea Ifakara kwenda dsm. Kufika Maseyu mida kama saa 8 usiku dereva akapaki, akasema amechoka anapumzika kidogo. Akatuambia saa 10 tumwamshe tuanze safari.
Sijui kama ni uchawi au ni nini, tulipitiwa na usingizi mzito, na wote, tulikuwa watatu tuliota ndoto ya aina moja. TUNAPIGA MECHI. tumejipiga mabao wote, kuangali saa ni dk 20 tu zimepita. Nilichowaeleza wenzangu ndio walichoota. Mwanamke niloyeota namgonga ndio huyo huyo wenzangu walikuwa wakiota wanamgona.
Niliota vipele vya baridi kwa uoga. Tukaondoka kuendelea na safari. Tangu siku hiyo sipandi tena malori ya mzigo yanayosafiri usiku.
Sent from my SM-G570F using Tapatalk
Nimesoma kwa kuogopaaa aiseee haya mambo ni real kumbe[emoji52]Mungu wangudah nmesoma sana ngoja na mimi ntoe kisa kilichosababisha niape kuwa sitakwenda kwa mganga tena kwenye maisha yangu.
ilikuwa 2002,tunatoka dar tunakwenda mkoa wa kigoma kwa wanojua bara bara enzi hizo wanajua ni jinsi gani kulikuwa na majambazi hasa ndani ya mapori ya Tabora,bahati haikuwa yetu mida ya saa 5 usiku wakati tupo road tukakuta bara bara imewekwa bonge la gogo mzee akataka kujitahid aligeuze ghafla walitokea watu wamebeba bunduki ndo kwa mara yangu ya kwanza kuone mtu kashka bunduki huku kajizungushia mkanda wa risasi mwilini bro wangu ile kuwaona tu akakata moto tuliokuwa hatujazmia tulikuwa watatu 3 mimi mzee na bimkubwa.
Tulichezea sana vitasa mzee alidhalilika mno mwisho wa siku walichukua mpka viatu nakumbuka viatu vyangu vya kitoto vya kuwaka taa,then wakaondoka mpka na gari tulikaa pale mpka saa 11 ndo tukapata msaada tukaenda polisi but hawakuwa na msaada mzee akapiga simu kigoma ikatumwa nauli tukaenda moja kwa moja mpka kwa baba yake(means babu),sasa babu yeye kila alivyokuwa anahadithiwa alikuwa anacheka mno hasa akimuangalia bro na ujanja wake ote et kazimia,upande wa baba yeye alikuwa na hasira mno alichokuwa anataka yeye ni wale watu awashikishe adabu hata kufa wafe basi ilivyofika usiku tukaelekea sehemu fulani inaitwa ujiji kwa mzee fulani alikuwa anaitwa juma njemba.
Nadhani kwa watu wa kigoma wanaweza kuwa wanamjua,akaelezewa kila kitu akasema hicho ni kitu kidogo sana,huku na yeye anacheka kisha akasema kuwa pale kwake kuna mbuzi alimchinja sababu ya sherwhe ya mwanae hvyo itatubidi tumtafutie mbuzi mwengne amreplace ili iwe kama malipo yake baba akakubali,kilichofata akawaita wajukuu zake walete (ubumba) ni udongo fulani hivi wa mfinyanzi kisha akawa anatengeneza kimdoli kidogo cha udongo kama vile vya kitoto toto,baada ya kukitengeneza akaanza kukiandika maneno yake kisha akakisimamisha chini,then akaanza kuongea maneno yake aliongea sana baada kama ya saa 1 akasema mtu yoyote ndani ya hichi chumba haruhusiwi kukimbia wala kupiga kelele kwani kwa kufanya hivyo ndo itakuwa kifo chake.
Basi aliendele kusema maneno yake ghafla yule mdoli pole pole alianza kukua na kuwa mkubwa pole pole,baada kama ya dakika arobaini alikuwa ni mkubwa kama binadamu mwenye mwili mkubwa alikuwa anamkono na kifua kikubwa na mrefu,kwa mara ya pili bro tena akazimia kwa mara ya pili mim mkojo ulishantoka natetemeka kama nmepatwa na dege dege,mwisho yule mdoli akaambiwa shtaka letu kisha akaambiwa nenda hivi vitu vinatakiwa leo leo,theb yule mtu akafungua mlango akatoka mbio alikuwa ni mwanaume lakini yupo uchi na ni mweusi tii kama mkaa mpka macho hakuwa na ichi kiini cheupe ye alikuwa na kiini cha moja kwa moja cha weusi,alivyoondoka tukaanza kumpepea na kumwagia maji bro alivyoshtuka yule mzee akatuambia kazi imeshakwisha kesho mtayapata majibu yenu.
Ilivyofika asubuhi tukapigiwa simu nakumbuka enzi hizo kulikuwa kuna buzz siyo hii tigo na hata simu zilikuwa za mezani,tukaambiwa kuwa kuna gari imepatikana Tabora yenye namba kama tuliyoripoti pamoja na vitu vingine,tukaanza safari na treni mpka tabora kufika kule tukakuta vitu vyetu na vingne vingi tu ila mzee alisema vyote vilikuwa vyetu hela zilikuwa kama 1m lakini zilipatikana 7m polisi hawakuchukua hata cent na hata walivyopewa walikataa kata kata hakikupotea hata kifungo kisha baada ya kuchukua tukaambiwa kuwa hao majambazi waliotuibia walikutwa msituni wakiwa wameuwawa wakasema wanahisi ni wanyama wakali ndo waliwauwa maana walikuwa wanaalama za meno makali milini mwao na kucha.
lakini wakashndwa kuelewa kama ni wanyama ndo waliwashambulia ni wanyama aina gani na kwanini hawakuwapiga hata risasi moja hao wanyama na wakati walikuwa na silaha nzito?Baada ya maelezo mengi mzee akawasha gari mpka kigoma stend ya kwanza mpka kwa yule mganga tulinunua mbuzi na zawadi nyingne nying lakini mzee aligoma hakutaka chochote zaidi ya mbuzi tu,basi tukampka mbuzi wake, akasema imebaki kazi moja tu na kazi yenyewe ni kumrudisha yule kiumbe(mdoli mtu)ili asitudhuru na sisi maana ni wetu hapo mdipo ilipokuwa mtihani maana kuna msharti mengi tulikosea plus kujisahau sasa akawa anatuandama sisi atuue dah kila mmoja nyumbani anaalama ya yule kiumbe yangu ni kungatwa skio na kula kipande nikipata mda ntawamalizia kisa changu but mpka leo mimi kwenda kwa waganga ni big no,but thanks god tulitoka salama
picha ya nilipongatwa kwenye skio ambyo ni alama ambayo sitaweza isahau mpka kifo
Sent using Jamii Forums mobile app
dah!pole sana mkuu,.Mimi nilikuwa siamini hizo mambo lakn kipind cha wife ana ujauzito wa mtt wetu wa kwanza.. nikiwa mchanga kbsa kiimani,siku hio nakumbuka tumelala tukaota ndoto moja mm na wife.. ndoto ilikuwa ni mmama mmoja anasema anataka mtt alieko tumboni ili amtoe kafara,tukashtuka.. baada ya kushtuka tukasikia mipaka inalia nyuma ya nyumba kwa sauti kubwa,nilikuwa nmeshafundishwa kuomba na kukemea.. asee niliomba sana usiku huo kwa ujasiri na nguvu maana wife yeye muda huo alikuwa analalamika tumbo linamuuma na mtt alikuwa anarukaruka hatar tumboni... wakat naendelea kuomba kwa nguvu na ujasiri nkaanza kusikia sauti za paka zinaendelea kusogea mbali na nyumba lakn kitu ambacho kilikuja kunishangaza mpka sasa ni kwamba wakat naendelea kuomba nilianza kusikia vishindo kbsa kwnye bati na nyumba haikuwa na celingboard yaan vile vishindo ni kama mtu akiwa anatembea juu ya bati ikatembea alafu nkasikia hiko kishindo kimetua kama kudondoka nyuma ya chumba changu... nkapata ujasiri wa kukatisha maombi ghafla nkafungua mlango kwenda kuangalia nione hata nyayo.. bt sikuona chochote... Hata siku wife kaumwa na uchungu mida ya jioni mapaka yalilia sana siku hio.. akaenda hosptal akajifungua na alijifungulia pale amana enzi hizo na wakt anajifungua paka alitokea akabeba na kondo lake la nyuma,akatoka salama... tukaendelea kumlea mtt wetu lakn mtt alikuwa anaumwa kila siku mwisho hasa kuharisha na kutapika na tukienda hosptal ugonjwa hauonekani..so mtt alipofika mwaka na miez miwil sku hio hali ya mtt ikiwa dhoofu wazaz wakaomba tupeleke mtt akaugulie huko.. basi nkamwambia wife akapaki akapanda daladala kwenda home.. akiwa kwnye daladala mzee mmoja mwnye mapetepete mengi ya rangirangi na kanzu na kibalaghashia chake akauliza huyu mtt anaonekana anaumwa eeh wife akamjibu ndio.. akamwambia ugonjwa wake sio wa hosptalin bt hakumwelewa alimaanisha nn,kufika home kakaa siku ya kwnza siku ya pili usiku akiwa amelala akaota ndoto wamekuja mmama na kundi lake kavaa kaniki akasema mmalizieni kabiss huyo mtoto afu ndoto ikakatika...kesho yake asbh mie nko mtaani napiga mzgo wife akanipgia simu hali ya mtt imechange na kwl haikupita dk kumi wife akiwa anamnyonyesha mtt akamfia hapohapo... R.I.P katt kangu ka kike first born wangu..
Sent using Jamii Forums mobile app
HahahahNishawahi sikia kisa kinschohusishwa na uchawi
Kuna masela wawili walienda kwa mganga ili wapate utajiri
Mganga akawapa dawa akawaambia wakaoge usiku makaburini na wakitoka mlangoni kwa mganga hawatakiwi kugeuka nyuma
Basi unaambiwa safari yao iliandamwa na misukosuko yakutisha, mara wasikie muungurumo wa simba akiwa nyuma yao na vimbwenga vingi lakini walijitahidi kukaza ili kutovunja sharti la kugeuka nyuma
Sasa ulipofika usiku majira ya saa 8 ikabidi waende makaburini kuoga ili kumalizia zoezi lao la mwisho ili wawe mamilionea
Walipofika makaburini wakavua nguo wote nakubakia uchi kisha wakapanda juu ya kaburi ili waoge
si unajua ukiwa katika ile mood flani hivi unaoga halafu umefumba na macho ili maji yasiingie machoni.
wakastukia tu paap! wameshikwa makalio kwa nyuma.
Aaah unaambiwa wote ilibidi wageuke nyuma kwa haraka huku wanakimbia na kupiga makelele
Kesho yake kijiweni wakaanza kulaumiana "aaah wewe ndiye ulizingua, we ungekausha bila kupiga mikelele mi nisingechochora kwani kushikwa tako kitu gani bwana" yani leo nisingekua nakunywa kahawa hapa ningekua nimejikoki huko kwenye hotel zinazotambulika na dunia"
[emoji23]Kisa kingine nilikisikia kilitokea maeneo ya sumbawanga
Kuna mzee wamakamo alikua ni tajiri sana, pesa zake haweki benk na hata akienda kufanya manunuzi hua haweki kwenye wallet kuzistiri zisionekane yeye hua anazishikilia tu kama wanafunzi wanavyoshika vitini vyao mikononi
Siku moja kuna kosi la majambazi lilijipanga kwenda kumvamia
Walimkuta yuko nyumbani kwake ameshikilia pesa akipata upepo kwenye garden yake
Wakamnyooshea bastola na kumwambia atulie kimya kisha atoe kila kitu alichonacho
Yule mzee akachukua zile pesa akazibana kwenye kwapa lake huku akitetemeka kwa woga
majambazi wakamsisitiza kua anyanyue mikono juu, mzee akatii amri kwa kunyanyua mikono juu kisha pesa alizozibana kwapani zikaanguka chini majambazi wakaziokota
Wakamwambia tena "toa kila kitu ulichonacho"
Round hii unaambiwa mzee alichomoa kichwa chake akakishika mkononi halafu kile kichwa kikiwa mkononi kikatoa sauti ikisema "sina chochote jamani nina kichwa tu hapa"
Kwahiyo baadae mdoli alirudi kwa mganga?alama nlobaki nayo mpka leo ya yule dubwana
inshort wengi humu wanasema sjui hakuna uchawi huwa nawaangalia tu but kwa yaliyonikuta nikikuhis hata unatembea na hiriz mfkoni hata kama ndgu yngu hutoniona tena maishan mwakoView attachment 1303100
Sent using Jamii Forums mobile app
Huyu kijana naye mwanga sana,nyumbani kweke ni masheikh tu wanapigana vikumbo mara nazi zivunjwe usiku basi tabu tupu,naona ndio staili ya life ya bongo.mwenye nafasi au tajiri,MWANGA.Nasikia Diamond huko Kigoma zaidi ya kupokelewa na umati wa kihistoria lakini pia kapokelewa na kundi kubwa la popo angani [emoji1787][emoji1787][emoji1787]. Anayebisha tembelea IG page ya babutale.
Sent using Jamii Forums mobile app
Wacha na Mimi niwape mkasa niliyoshuhudia katika mahakama moja miongoni mwa wilaya za Tanga.
Nikiwa katika harakati za kutekeleza majukumu ya kikazi nilipanga nyumba moja hivi iko vizuri tu.wapangaji tulikuwa watatu tu, baba mwenye nyumba Ni kijana mwenzetu ana mishe zake. Sasa bhana huyu baba mwenye nyumba kwenye biashara zake akafanya magumashi yaliyompelekea kushatakiwa na kufunguliwa kesi mahakamani. Kesi ilikuwa kubwa ya kumfunga kifungo kirefu tu. Kwa kuwa huyu baba mwenye nyumba tulikuwa tukielewana stori kwa Sana akanambia nimsindikize mahali kwa mganga. Tukaenda aisee tulipofika mganga akatueleza shida tuliyoendea kesi jinsi ilivyo na imebaki shahidi tu kuja kutoa ushahidi siku ya kesi jamaa ahukumiwe kwa namna yoyote jamaa hachomoki. Mganga akasema kanileteeni Nazi moja tu na si kitu kingine duh tukasema hapa hamna mganga. Tukaenda nunua Nazi tukampelekea, mganga akaandika maneno ya kiarabu kwenye ile Nazi kwa juu ikiwa haijapasuliwa ( maandishi yalikuwa ya rangi nyekundu). Kisha akasema saa 8 usiku ile Nazi ikapasuliwe njia panda ya kuelekea mahakamani.
Tuliporudi home tukawa tunasema mganga mzinguwaji kesi kubwa yy anatufanyia mzaha, basi saa nane usiku tukaenda njia panda ya kuelekea mahakamani jamaa jamaa akajifunga kaniki nyeusi Kisha akaipasua kama alivyoelekeza mganga.
Siku ya kesi ikafika ndipo nilipojuwa kuwa dunia no Zaidi ya tunavyoiona. Jamaa kafikishwa kizimbani kasomewa mashtaka kakataa akaitwa shahidi wa Kwanza, hakimu Kila swali akimuuliza shahidi anasema kasahau hakumbuki kitu, shahidi wa pili ndiye was muhimu Sana aisee jamaa alivyopanda kutoa ushahidi alikuwa bubu seriousky kudadeki acheni tu Kila akiulizwa anashindwa kuongea anabaki baaaa...baaaa...mmmm. Hakimu alidata akaahurisha kesi.
Siku tajwa ya kesi kufika hakuna shihidi alokuja Tena na Tena. Hakimu akafuta kesi na jamaa akawa huru.
Hivi vitu vipo aisee Ni mpaka ushuhudie ndiyo utaamini.
Sent using Jamii Forums mobile app