Kama umewahi kushuhudia live nguvu za giza pita hapa uweke ushuhuda wako

Kama umewahi kushuhudia live nguvu za giza pita hapa uweke ushuhuda wako

Hahahahaha

Umenikumbusha mbezi beach makonde Kuna mjengo wa maana ukilipa kodi hulali..unakutana na vimbwanga hatari..Mara usiku vyombo vinaangushwa ukiamka asubuhi unakuta na nyayo zilizokanyaga maji kuanzia jikoni hadi sebuleni..

Kuna rafiki wa dada angu alipangiwa na mzungu wake ..akawa anamwambia nyumba ina mauza uza mzungu haamini..siku aliyolala pale aliyoyaona mbona aliondoka na mwanamke wake usiku uleule hata Kodi hakudai..

Sent using Jamii Forums mobile app
Sio ya jogoo io kweli,anyway znaweza kua different ila same story.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Duuh lete Visa kadhaa vya kuverify hili
Kuna kipindi hapo hapo nilipopanga na yule mama wa kigoma, alikua ananitoa nje kimazingara na alikua ananitesa kweli

Basi siku moja nilala chakushangaza nikawa najiona nimetoka sijui wapi kule tena nilikua nimechoka sana nikawa naelekea kwenye chumba changu

Cha ajabu ile nakata kona nikamuona yule mama wa kiha kasima mlangoni tuanpoingilia akiwa amevaa nguo za kaniki(nyeusi) na kiremba cheusi theni akaninyooshea mkono huku anaongea maneno ya kichawi ghafla nikashitka

Ingawa badae nilipo lala nikajiona nipo ndani tena hata kuona vzuri siwezi nikiwa napapasa kitanda kilipo

Hiii inamaana gani
Yaani manaake yule mama alinichukua kimazingara usiku nakwenda kunibebesha magunia ya njegere alizokua anauza pale ilala.....

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hii niliambiwa na jamaa yangu na ilimtokea Dar miaka ya hivi karibuni.

Jamaa waliitwa kwenye interview ya driving! Wakapita, wakaitwa kwenye second interview ambayo ndio angepatikana dereva sasa!

Jamaa akawapoteza wenzie yaani siku ya interview kaenda alone, wenzie hawajaja! Jamaa akapata kazi

Sent using Jamii Forums mobile app

🤣🤣🤣
 
nilipanga nyumba,chumba cha uani...sasa ikawa daily night Kali lazima mapaka yajae na kupiga kelele za kutosha juu ya bati...na mengine yanagonga dirishani..

kelele zikaendelea lakini nikishaamka na kuwasha UDI na kushtua Bob Marley, hayo makelele yanakata..na mbaya zaidi ni juu ya bati langu tu..

jirani yangu ticha nikimuuliza kuhusu hizo kelele anakataa hajawahi kuzisikia...na hata nilipomuuliza aliyeniachia chumba juu yaa mapaka,naye alikataa

ajabu nilipomuuliza baba mwenye nyumba juu ya makelele ya kutosha ya hao paka,naye alikataa kuwasikia.!

na kuanzia siku namuuliza hizo kelele zilikoma kabisaa..sijui alikuwa na uhusiano gani na hayo makelele ya mapaka.!!


Sent using Jamii Forums mobile app
 
dah nmesoma sana ngoja na mimi ntoe kisa kilichosababisha niape kuwa sitakwenda kwa mganga tena kwenye maisha yangu.

ilikuwa 2002,tunatoka dar tunakwenda mkoa wa kigoma kwa wanojua bara bara enzi hizo wanajua ni jinsi gani kulikuwa na majambazi hasa ndani ya mapori ya Tabora,bahati haikuwa yetu mida ya saa 5 usiku wakati tupo road tukakuta bara bara imewekwa bonge la gogo mzee akataka kujitahid aligeuze ghafla walitokea watu wamebeba bunduki ndo kwa mara yangu ya kwanza kuone mtu kashka bunduki huku kajizungushia mkanda wa risasi mwilini bro wangu ile kuwaona tu akakata moto tuliokuwa hatujazmia tulikuwa watatu 3 mimi mzee na bimkubwa.

Tulichezea sana vitasa mzee alidhalilika mno mwisho wa siku walichukua mpka viatu nakumbuka viatu vyangu vya kitoto vya kuwaka taa,then wakaondoka mpka na gari tulikaa pale mpka saa 11 ndo tukapata msaada tukaenda polisi but hawakuwa na msaada mzee akapiga simu kigoma ikatumwa nauli tukaenda moja kwa moja mpka kwa baba yake(means babu),sasa babu yeye kila alivyokuwa anahadithiwa alikuwa anacheka mno hasa akimuangalia bro na ujanja wake ote et kazimia,upande wa baba yeye alikuwa na hasira mno alichokuwa anataka yeye ni wale watu awashikishe adabu hata kufa wafe basi ilivyofika usiku tukaelekea sehemu fulani inaitwa ujiji kwa mzee fulani alikuwa anaitwa juma njemba.

Nadhani kwa watu wa kigoma wanaweza kuwa wanamjua,akaelezewa kila kitu akasema hicho ni kitu kidogo sana,huku na yeye anacheka kisha akasema kuwa pale kwake kuna mbuzi alimchinja sababu ya sherwhe ya mwanae hvyo itatubidi tumtafutie mbuzi mwengne amreplace ili iwe kama malipo yake baba akakubali,kilichofata akawaita wajukuu zake walete (ubumba) ni udongo fulani hivi wa mfinyanzi kisha akawa anatengeneza kimdoli kidogo cha udongo kama vile vya kitoto toto,baada ya kukitengeneza akaanza kukiandika maneno yake kisha akakisimamisha chini,then akaanza kuongea maneno yake aliongea sana baada kama ya saa 1 akasema mtu yoyote ndani ya hichi chumba haruhusiwi kukimbia wala kupiga kelele kwani kwa kufanya hivyo ndo itakuwa kifo chake.

Basi aliendele kusema maneno yake ghafla yule mdoli pole pole alianza kukua na kuwa mkubwa pole pole,baada kama ya dakika arobaini alikuwa ni mkubwa kama binadamu mwenye mwili mkubwa alikuwa anamkono na kifua kikubwa na mrefu,kwa mara ya pili bro tena akazimia kwa mara ya pili mim mkojo ulishantoka natetemeka kama nmepatwa na dege dege,mwisho yule mdoli akaambiwa shtaka letu kisha akaambiwa nenda hivi vitu vinatakiwa leo leo,theb yule mtu akafungua mlango akatoka mbio alikuwa ni mwanaume lakini yupo uchi na ni mweusi tii kama mkaa mpka macho hakuwa na ichi kiini cheupe ye alikuwa na kiini cha moja kwa moja cha weusi,alivyoondoka tukaanza kumpepea na kumwagia maji bro alivyoshtuka yule mzee akatuambia kazi imeshakwisha kesho mtayapata majibu yenu.


Ilivyofika asubuhi tukapigiwa simu nakumbuka enzi hizo kulikuwa kuna buzz siyo hii tigo na hata simu zilikuwa za mezani,tukaambiwa kuwa kuna gari imepatikana Tabora yenye namba kama tuliyoripoti pamoja na vitu vingine,tukaanza safari na treni mpka tabora kufika kule tukakuta vitu vyetu na vingne vingi tu ila mzee alisema vyote vilikuwa vyetu hela zilikuwa kama 1m lakini zilipatikana 7m polisi hawakuchukua hata cent na hata walivyopewa walikataa kata kata hakikupotea hata kifungo kisha baada ya kuchukua tukaambiwa kuwa hao majambazi waliotuibia walikutwa msituni wakiwa wameuwawa wakasema wanahisi ni wanyama wakali ndo waliwauwa maana walikuwa wanaalama za meno makali milini mwao na kucha.

lakini wakashndwa kuelewa kama ni wanyama ndo waliwashambulia ni wanyama aina gani na kwanini hawakuwapiga hata risasi moja hao wanyama na wakati walikuwa na silaha nzito?Baada ya maelezo mengi mzee akawasha gari mpka kigoma stend ya kwanza mpka kwa yule mganga tulinunua mbuzi na zawadi nyingne nying lakini mzee aligoma hakutaka chochote zaidi ya mbuzi tu,basi tukampka mbuzi wake, akasema imebaki kazi moja tu na kazi yenyewe ni kumrudisha yule kiumbe(mdoli mtu)ili asitudhuru na sisi maana ni wetu hapo mdipo ilipokuwa mtihani maana kuna msharti mengi tulikosea plus kujisahau sasa akawa anatuandama sisi atuue dah kila mmoja nyumbani anaalama ya yule kiumbe yangu ni kungatwa skio na kula kipande nikipata mda ntawamalizia kisa changu but mpka leo mimi kwenda kwa waganga ni big no,but thanks god tulitoka salama


picha ya nilipongatwa kwenye skio ambyo ni alama ambayo sitaweza isahau mpka kifo

Sent using Jamii Forums mobile app
Uliposema na umri wako mdogo uliruhusiwa kuingia kwenye nyumba mganga nikajua kwamba hii ni chaiiiiii
 
Jana nimevunjiwa home sasa kuna jamaa akanimabia twende kwa mzee hivyo vitu vitarudi kwaiyo nataka nikajionee kama kweli haya mambo yapo au sound tu.nitaleta mrejesho
20191230_105627.jpg


tatizo lugha
 
Miaka kadhaa nyuma, bibi yangu mzaa mama, katika umri wake wa makamo, mrembo na mwenye kinywa kilichosheheni meno imara na meupeeee, aliamka asubuhi moja tusiyoisahau mpaka leo, kinywani akiwa hana jino hata moja. Alikuwa kibogoyo kabisa kama alizaliwa na kukua bila meno.

Wakati ukoo mzima tumetunduwaa kwa mshangao, jamii ilitutuliza kwa kutuambia kuwa tuwe wapole na habari ndiyo ilikuwa imekwisha hivyo. Kuwa bibi yangu eti alifanya uzembe wa kuamka na kupiga kelele akidai meno yake hayamo kinywani.

Kumbe ilimpasa, baada ya kuona kinywa chake kitupu, angerudi kimya kimya kulala. Meno yake yangerejeshwa na walioyaazima kwenda kutafunia nyama na bisi!! Ni juzi tu tumemzika bibi yetu akiwa kibogoyo kwa miaka kibao, kwani meno hakurejeshewa tena. Uchawi wa migombani Unyakyusa huu!!

Sent using Jamii Forums mobile app
Umenikumbusha uchawi wa unyakyusa miaka ya 2004 pale Tukuyu kwenye kiwanja cha mpira karibu na Stendi, kulikuwa na mkesha wa mwenge sisi tumeroka
Mfijinja dah!!

Sent using Jamii Forums mobile app
Tukuyu kulikuwa na watalaamu kipindi cha nyuma pale uwanja wa mpira Tukuyu Mjini kulikuwa na mbio za mwenge.
Kabla ngoma za asili au ling'oma halijapigwa mvua ilianza kunyesha dakika chache wazee wa mila wakaitana na wakazuia mvua.

Siku ya ling'oma kulikuwa na uchawi haswa maana kulikuwa kama na ligi ya ngoma kutoka sehemu mbalimbali, nakumbuka kuna ling'oma kutoka Bujesi hawa walikuwa wakipiga ngoma Tukuyu inasimama.

Siku nyingine nilikutana na kisa cha kukutana na vibwengo mimi na jamaa yangu kwenye mashamba ya chai Kyimbila. Alinishawishi tufate ling'oma Ushirika kulikuwa na Mashindano ya ngoma. Wakati wa kwenda tukapanda Hiace "Big Poppa". Usiku ikawa kasheshe saa 3 hakuna gari tukaamua tutembee kufika mashamba ya chai tunaona kibwengo kinatembea upande wetu kila tukisogelea kinaongeza spidi. Gafla kikapotea tunafika maeneo ya Kamangila Bar kuna mzee tukamwambia akacheka na kusema nyie ni wageni.

Visa ni vingi huko Sakura Pangani usiku mkali tupo na pikipiki mara raia yupo njia panda ile kusogeza pikipiki hakuna kitu.

Njia ya Mpanda-Sumbawanga tupo na Isuzu Kb pick up kuna raia anagonga body kama ana amrisha gari isimame na gari iko mwendo kipindi hicho njia mbovu.
 
Pangani kulikuwa na mzee anaitwa Halichwi huyo alikuwa anaogopeka balaa, ilikuwa hakitaka jambo jua halikuchi hilo jambo linatokea.

Huyu alikuwa akiwa kwake jioni anatembea na majini yake kwenda kufata mahitaji.

Hapo Usagara Tanga mjini kuna mzee alikuwa mganga wa kitabu miaka ya nyuma kidogo kuna Kipindi alikuwa anayafungulia majini yanakuwa nje hapo karibu na kwake na njia hiyo ya Kwenda Coast Lodge.
 
Kuna mzungu mmoja alikua kakaa sana Afrika(si unajua kasha adapt tabia za kibongo mpaka katuzidi wenyeji),Yuko na kijikampuni chake ametupatia Ajira ya masimango sana.Mtaliano yule alikua ana tabia ya kumtukana kila staff bila kuangalia umri wala cheo.Siku akiamka fresh mnapiga stori..

Kuna mzee ni msafishaji wa bustani.Anajiheshimu sana na watu wote tunamweshimu.Iko siku sikujua walipishana nini kiswahili na Mtaliana.Mzee alitukanwa sana.Matusi yote.

Mzee alishukuru kwa matusi akaondoka.Ila alimwambia nakupa week moja majibu utayapata.

Baada ya week Mzungu akivuka tu geti la kuingilia kazini anapata homa kali sana.Akipelekwa hospital mzima wa afya.Akipelekwa nyumbani mzima wa afya.Kosa ni kugusa maeneo ya kazini....

Sent using Jamii Forums mobile app
Hii hata Kule Amboni Estate imewahi kutokea kulikuwa na mzungu kazoea Tanzania akawa ananyanyasa sana wabongo kwenye kampuni.

Wakampiga juju kila akienda Pangani anaumwa sana, akiwa Ulaya anakuwa vizuri.
Mzungu akaona isiwe tabu akaondoka mazima Tanzania.
 
Tanga miaka ya 82. Kuna jama alifanya mapenzi na mke wa mtu. Ghafla alipomaliza kitu kikakatikia ndani lkn damu haimwagiki. Alikuja kwa mganga pale Gatundu. Mtu mwingine ukimuangalia mashine unaiona imetulia. Yeye binafsi haioni na hata akipeleka mkono anakuta hamna kitu.
...........,..................

Jamaa mwingine tena alitembea na mke wa mtu. Wakamaliza fresh kila mtu akachukua hamsini zake. Jamaa alikua anakakaa nyumba isiyo na ceiling board. Ghafla wakati amepumzika chumbani kwake ametulia kitandani baada ya kumshuhhulikia mke wa bwege akaona panya amebeba dhakari na pum*** anakatiza nayo kwenye mbao juu
 
Back
Top Bottom