Kama umewahi kushuhudia live nguvu za giza pita hapa uweke ushuhuda wako

Kama mtakimbuka ile mvua ya mawe kahama march 2015 ngoja niwape kisa chake.

Mvua zilikuwa adimu sana basi wananzengo wakamfuata mganga mmoja alokuwa ana tuhma za kuzuia mvua
Basi watu wakamuhoji akakataa tuhuma hizo. Jamaa hawajaelewa wakampiga hadi kumuua.
Wakati anakufa alisema nakuta lkn mtaona.
Waloelewa walianza kuhama walokaza shingo wakakomaa .....
Mvua ilipoanza wakasema tumemuua yule alikuwa anazuia mvua....lkn ikaja kuzidi....na mawe juu. Iliua watu na mifugo na uharibifu mkubwa ulotokea.

Kiranga usi comment hapa
 
Mie ningekiambia kaniletee madini!! wewe mtu mfupi...
 
huyu hatakiwi kujibiwa,siku moja nature yenyewe itajipambanua machoni pake kwa sura yoyote tu.

halafu swala la kujua ameona nini litabaki kichwani kwake[emoji23][emoji23][emoji23]
 

Ukitaka kunijibu kwa tija zaidi, naomba unitag au uninukuu ili nipate kuona maandishi yako, vinginevyo unaweza kunipinga kwa hoja halafu hata nisione uli hiandika, nikakosa nafasi ya kukujibu.

Kuhusu kujibu kwa maswali, mimi natumia Socratic method.

Kama hujui Socratic method ni nini, sishangai hunielewi. Google that.

Na watu wengi kukubali kitu hakukifanyi hicho kitu kiwe kweli.

Kuna kipindi watu wengi walikubali jua linazunguka dunia.

Je, hilo lilifanya jua liwe linaizunguka dunia?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Thibitisha kuwa dunia inalizunguka jua. Kwanza hata wanasayansi wanakiri wameongeza chumvi (orbit) kwenye mfumo wa jua. Btw naomba tusibishane.
 
Ukiniambia nisi comment, ndiyo umenialika ku comment.

Nasoma kitabu cha histoeria ya Rais Mstaafu Benjamin William Mkapa. "My Life, My Purpose: A Tanzanian President Remembers".

Rais Mkapa anaelezea jinsi familia yao ilivyoonewa wivu na majirani, mpaka wakazushiwa kwamba wamezuia mvua, mama yake na bibi yake Rais Mkapa akateswa sana, mpaka bibi yake Rais Mkapa akafariki kutokana na mateso hayo.

Watu wenyewe familia ya Mkapa walikuwa Wakatoliki wazuri, baba yake rais Mkapa alikuwa m Katekista na mwalimu. Majirani zao waliojiita "Wakristo" waliwaonea wivu na kuwazushia kwamba wamezuia mvua.

Hizi imani za uchawi na kuzuia mvua zimeua watu wengi sana wasio na hatia.

Hao watu wa zamani tunaweza kusema walikuwa hawana elimu ya kujua mvua inaanzaje.

Leo hii karibu kila mtu anatembea na internet yenye usomi wote wa kuelezea mambo haya.

Bado mnaamini mambo ya watu kutengeneza mvua kwa uchawi tu?
 
Thibitisha kuwa dunia inalizunguka jua. Kwanza hata wanasayansi wanakiri wameongeza chumvi (orbit) kwenye mfumo wa jua. Btw naomba tusibishane.
Kuthibitisha unakokutaka unataka kukidhi vigezo gani?

Maana naweza kuthibitisha usikubali uthibitisho wangu kwa vigezo vyako.

Nipe vigezo vyako unavyotaka nivitumie kuthibitisha, ili nijue uthibitisho wangu unakidhi vigezo.
 
Sikulazimishi ukubali ila nikwambia jambo moja tu ndugu, kwenye maji kuna vimbwanga hujawahi kufikiriaa. Hii alinihadithia mama yangu kipindi wanakwenda Bukoba miaka ya themanini ambapo meli ya Mv Bukoba ilikuwa ikifanya safari zake mchana.

Kuna pahali walifika wakawaona watu kila mtu na shughuli zake, wengine wakawa wanacheza tenis mixer tenis inagonga mpaka meli, wengine wanashughuli nyingine.
 
Uongo. Mwaka gani huo?

 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…