Kama umewahi kushuhudia live nguvu za giza pita hapa uweke ushuhuda wako

Hiki kisa Cha kuhadithiwa

Sasa sijui Ni nguvu za Giza au maajabu

Miaka ya nyuma kidogo,miaka ya 90's
Enzi hizo wazazi wangu Ni walimu wa shule moja katika Kijiji fulani..
Mimi nilikuwa kichanga..

Shule ilikuwa porini ,pia kulikuwa na nyumba za walimu huko huko shule.
Walimu wote waliishi huko.

Basi ilikuwa mfano j3 siku ya ukaguzi,zile ratiba zote zilizofanyika mchana ,usiku pia zinafanyika hivyo hivyo.
Walikuwa wakilala wanasikia kengele ya kuhesabu namba inagonga,Mara ya kwenda assemble..ngoma ya ukaguzi inapigwa Kama ilivyokuwa mchana..
Kama siku hiyo uliimbwa wimbo wa shule Basi usiku wimbo wa shule utaimbwa pia.

Yaani ilikuwa ni shida.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kisa kingine
Baba yangu alishawahi mwadhibu mwanafunzi kwa fimbo..yule mtoto hakufanya kazi(homework)

Alivyorudi kwao akaenda kumsemea kwa babu yake.
Babu yake aliwahi asubuhi akamwambia mwalimu utanitambua.
Mara ghafla baba mkono ulivimba.
Akaenda hospital wapi hakuna kitu..
Ulivimba ulijaa maji.

Alikuwa halali usiku kwa maumivu.
Aliombewa Sana (familia yangu ilikuwa wale wanaosali uamsho wa wakristo tz UWATA)
Baadaye baada ya maombi akarudishwa Tena hospital akatibiwa akapona.


Mama yangu pia alishawahi kuugua..baada ya maombi yule aliyemroga akaanza kuropoka maneno.
Alimroga alikuwa anataka ndoa ivunjike amuue mama ili aolewe Yeye
Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kisa kingine
Miaka ya nyuma ..
Kipindi hicho nilikuwa mdogo mdogo hivi,kijijini huko kwa Bibi.

Mwalimu fulani alikuwa ananyoshewa vidole kwamba Ni mchawi.
Nasikia kweli alikuwa mtata..wakawa wamempangia siku wamfyeke na mapanga.

Yeye alikuwa anafundisha Kijiji jirani..ila alikuwa anakuja hiki Kijiji kunywa pombe.
Sasa wakati anarudi toka kilabuni wakamvamia,wakamfyeka na mapanga,ponda kichwa Hadi wakamuua.

Kesho yake habari zinaenea mwalimu fulani ameuawa wamemtoboa Hadi macho.
Polisi wakaenda eneo la tukio (huwa nasikia mboni za jicho huwa zinaonyesha wauaji)Sasa wao walichomachoma.

Kukawa na msiba ...maiti ikapelekwa mochwari Kijiji kingine ambako ndiko wilayani kwa ajili ya kuzuia mwili kuoza na taratibu nyingine.

Huo usiku wanafamilia wanapanga taratibu za mazishi Mara wanasikia mtu (marehemu)anawaita nje

Yaani walizika yule mzee ila alikuwa anarudi nyumbani kila siku usiku anaenda kuwagongea.
Pale makaburini ukipita usiku unamkuta amekaa juu ya kaburi,akawa anafukuza watu.

Wale waliomuua waliugua MMoja baada ya mwingine,wengine walifariki...alibaki huyo MMoja yaani alikuwa anamtesa kila siku anaenda kwake.
Baadaye aliukimbia mji wake

Kuna watu walishakutana nae huko wilaya nyingine,walipishana naye njiani.
Baadaye walienda kumfunga(Mambo ya kimila zaidi mi siyajui)
Ndiyo ikawa mwisho wa usumbufu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kuna kisa kingine
Hiki kimetokea mwaka 2018

Nilienda huko Kijijini..
Kuna kijana alikuwa anasifika kwa uchawi hapo Kijijini..kijana mdogo Kwenye late 20's au early 30's.
Basi wachawi huwa wanajuana wao kwa wao.

Kuna mzee mmoja hapo kijini Ni mganga wa kienyeji,
Huyo mzee kwake kulikuwa na sherehe Kama tambiko hivi,mtoto wake mkubwa wa kiume alikuwa amenunua gari akalipeleka kwa baba yake ambaye ndiyo huyo mganga wa kienyeji ili walizindike wanasema wao kulitambulusha kwa mizimu.

Sasa kawaida ya hizo sherehe,mwenye gari ananunua pombe za kutosha,wazee wa Mila wanakunywa Hadi waridhike ndiyo wanasema mizimu imebariki.

Mara wanaanza kunywa pombe zikawa na dosari,zimechacha zote.
Yule mzee(mganga)akaenda ndani ofisini kwake.. kuangalia Kwenye kioo akamuona huyo kijana yuko pale(niliyesoma pale juu kwamba kijana mdogo mchawi)
Sasa sijui alikuwa ameenda na dawa chache ,,yule mzee aksmzidi nguvu yule kijana.
Akamtungua..

Asubuhi tunasikia msiba unatangazwa,vijijini huko huwa wanapiga ngoma...Mara yule kijana amefariki.
Homa ilimbana usiku ,akaanza kugaragara chini kupelekwa hospital dk akawaambia mbkna hii Ni maiti tayari.

Hiyo siku amekufa,Jana yake alikuja pale nyumbani nilipokuwa,Kuna Kaka alikuwa anaishi pale alikuja kumuulizia,
Alivyonikuta hakunisemesha kitu nilikuwa nimetoka kusali,sijui kwanini alinipita hata salamu hakunipa,akaondoka

Basi msiba ukapita,kijana akawa ameenda.
Mara usiku wanamuona kwake anazunguka nje.
Mke wake alisema kwamba alikuwa anamgongea usiku.
Aliwatokea marafiki zake..
Nikawa namtania yule kijana wa pale nyumbani kwamba wewe hajakutokea!?
Maana ile siku anakufa mchana alikuja hapa,akasema hapana..ila nimemuota usiku.

Basi haukupita mwezi,mtoto wa yule mzee mganga aliyepeleka Lile gari nyumbani kwao ,,(alikuwa mwanajeshi) akafariki.
Yaani hakuugua chochote alikufa ghafla.

Yule mzee alilia,akasema Bora wangemchukua huyu mdogo.
Alilia Sana yule mzee.

Kuna kiss kingine Cha huyo mzee na mjukuu wake(yaani mtoto wa huyo mtoto wake mwanajeshi)
Nimechoka kuandika.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Daaah so sad.

Umesema vyema; nuru na giza havichangamani kabisa. Na wengi wetu huwa tunamjua na kumuamini Mungu when things are ok; lakini inapotokea shida tu; huwa hatukimbilii kwa Mungu tunayemnena kwa watu kila siku; tunakimbilia kwa waganga. Unfortunately waganga watapoozesha tatizo lako kwa muda au litaisha kabisa; but in the process kuna maagano ya chale (damu) na sadaka ambazo zitakurudisha tu kwenye madhabau za kipepo; utakuwa mtumwa wa shetani daima. Wengine ndo katika tiba unapewa na jini la kukulinda; siku ukilichoka ukataka uachane nalo ndo utaelewa shoo.

Kwa Mungu ni kana kwamba mara nyingi anajibu kwa kukawia (though kwake hakuna kukawia wala kuwahi; He does everything in His own perfect time). Lakini akishakujibu ndo umefunguliwa mazima and the good thing is atakachokupa Mungu (baraka yake) hakitakupa huzuni/majuto. When wengi tunashindwa kumwamini Mungu na kuwa na uvumilivu wakati tunasubiri atutendee
 


Pole sana mamy. ...
kweli ndoto mbaya kama hizo ni za kufunga na kuomba sema ulikua mdogo hukuelewa kiivo



Cc Smart911
 
Pole sana. Nakazia hapa kwa huu mstari.

Ayubu 33:14-15

14 Kwa kuwa Mungu hunena mara moja, Naam, hata mara ya pili, ajapokuwa mtu hajali.
15 Katika ndoto, katika maono ya usiku, Usingizi mzito uwajiliapo watu, Katika usingizi kitandani.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
pole sana dear,
kabisa ndoto ni taharifa kabla ya jambo kutokea,
nakumbuka mwaka jana kuna usiku mmoja mimi,dada yangu,na mdogo wangu wa kiume tuliota msiba mkubwa sana nyumbani na ulikua ni usiku mmoja na mida ile ile wote kwa pamoja tukaota ndoto io,
Tuliamka na kukemea sana roho ya mauti, asubuhi ya io siku mama aliamka anaumwa sana lakini maombi yetu yaliepusha ile roho ya umauti iliozengea,

ndoto ni taharifa ni ya kuchukulia kwa umakini na kutokuipuuzia.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
pamoja Mkuu.
 
hiyo namba moja umeigonga vile vile, mtu lazima upataje utapokuwa, sasa kimjini mjini tuna tabia ya kuficha tulipo tusipigwe mizinga ndio tatizo linapoanzia!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nilishawahi kuota pia mama yangu yangu amepata tatizo.
Nimeamka sikujua Ni tatizo gani ila yale mawazo yakawa yananijia Tena na Tena,
Nikawa napata kengele kichwani kwamba Kuna kitu lakini nikapuuzia sikufanya lolote..nadhani ujinga wangu pia ulichangia

Ule mwaka mama yangu alipata matatizo,yaani siji kusahau.
Ni Mungu tu alitenda.

Mwaka Jana december pia nimelala nikawa naota nyumbani, naona km Kuna kitu kibaya kitatokea na kitamuathiri mama.
Asubuhi nilivyoamka Yale mawazo yakawa yananijia Tena...nikasali.
Baadaye nikatulia kusikiliza mawazo yatakayonijia baada ya maombi.
Kuna mstari ukaja akilini nikashika Bible nikafunngua palepale ulipo ilikuwa habakuki nadhani.
Nikamtumia mama message nikamwambia asali, nikamwambia simama kwa miguu yako..usisubiri mtu akusalie.
Kweli haikupita wiki Kuna mtu mbaya alienda nyumbani..lakini lilipita.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nimekuja kujua hili baadaye Sana.
Na kumbe nilianza kupewa vitu zamani..nahisi umri pia unachangia.
At least siku hizi miaka imesogea najitambua

Unakuta Jambo limetokea nakumbuka kabisa hili mbna Kama si jipya nilishawahi kuona..nakumbuka kumbe nilishawahi kuota kitambo.

Siku hizi nimekuwa makini Sana kusikiliza.
Ni Hadi katika maisha yangu ya kawaida,Roho mtakatifu ukikaa naye vizuri anakufundisha na kukwambia kila kitu..
Bahati mbaya Sana wengi wetu hatujui mumsikiliza,au tunasikia na kupuuza.

Wiki iliyopita kupuuzia kumenigharimu.
Ilikuwa nna ratiba kwenda sehemu,Basi nimeamka nikatulia kwa Muda..nikasikia wazo linanijia kwamba wakati wa kwenda kule usisahau kitu fulani,nimemaliza kujiandaa nikaona Muda umeenda..icho kitu kilikuwa kabatini,nikaona hapa nikianza kufungua Tena nitachelewa..wazo linanijia kuwa lakini mbna unaacha Ni Cha muhimu,Mimi huyo nikaondoka.
Dah..nimefika kule nilikoenda nilijuta kwanini sikubeba.

Hii Hali ilikuwa inanikuta Hadi Kwenye masomo.
Siku za mitihani nikilala mawazo yananijia kwamba pitia hapa na hapa,nikiamka hivyohivyo yanakuja kwanini usipitie hapa..
Kuna siku nilipuuza..kufika Kwenye mtihani nikayakuta Mambo na Mimi sikupitia.

Linaweza likaja wazo kamuombee mtu fulani au nenda kaongee naye Jambo fulani.
Nikiwaza na nilivyokuwa mdhaifu wa kuongea nitawezea wapi!?
Nilishawahi mpoteza rafiki yangu tuliyecheza pamoja ..baadaye wazo likanijia kwamba hukumwambia hiki,mbona hukumuombea.

Tangu hapo nikisikia maelekezo ya kuongea na mtu au kusema kitu huwa sipuuzi.


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mimi kuna mtoto wa ndugu yangu.kuna siku alinikwaza kweli kweli.
Yaani alinikwaza kweli yaani...mpaka machozi yalinitoka siku hiyo.
Na kuna jambo ambalo alikuwa anasubiria majibu.
Kwa hasira nilivyokwazika siku ile nilinena maneno mabaya juu yake na nilisema akose hilo jambo analolisubiria...
asee baada ya siku kupita na hasira tu zilivyoisha nikasahau yoteee mimi huwa nimtu wa kuchukia hapo hapo tu ila ni mwepesi kusahau..
Huwezi anini lile jambo nililonena kwake akose alikosa kweli....
Niliumia sana japo hakuna mtu yoyote ambae nilimwambia kwamba nilimnenea vile zidi ya leo naandika hapo...
Niliumia sana pasipo kujua jinsi gani ya kufanya yale maneno yasiendelee kuleta madhara kwake.
Kwani nilimsamehe na kumuomba MUNGU ayatengue...
Na nikaapa sitarudia tena kumnenea mtu mabaya.... @Da'Vinci

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wakiwa wanafanya kazi huko shambani wanaonekana? Kama hawaonekani majirani watasemaje pindi wanapoona shamba limelimwa asubuhi na jana mpaka jioni lilikuwa halijalimwa?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…