Kama umewahi kushuhudia live nguvu za giza pita hapa uweke ushuhuda wako

Kama umewahi kushuhudia live nguvu za giza pita hapa uweke ushuhuda wako

Wale waliosoma boarding mnamkumbuka miss corridor sjui nyie mlimwiitaje in short huyu ni jini huwa anatembea ukumbuni kwenye mabweni mashuleni au makambini au maholi tulitunga hilo jina sababu akitembea unaskia "ko, ko, ko " ile sauti kama ya viatu vya kike vyenye visigini virefu ukienda angalia huoni mtu ukibahatika unamuona mwanamke ana nywele ndefu kakupa mgongo anamalizia kukata kona

Sent using Jamii Forums mobile app
haukumla kisusio mimi ningemfuata nikamshika tako kiaina.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Aliona kichwa chake nn..... ????
Alikuwepo mfanya biashara mmoja huko(alikuwa anafanya biashara za magendo) basi kila alipokuwa anapita na pikipiki yake akawa anasumbuliwa na askari mmoja wa barabarani ikabidi awe anatoa hongo ili asikamatwe ilifika time akachoka kutoa hongo.

Siku mmoja akapita kama kawa akasimamishwa na yuleyule askari. Alikuwa na ndoo amefunga kwenye pikipiki yule askari akaenda kukagua haaa akakutana na kichwa cha mtu kinatoa damu mbichi kana kwamba kimekatwa muda huohuo.

Askari aliruka kwa mshtuko maana hakutarajia kuona kitu kama hicho wenzake kufika pale kwenye ndoo hawaoni kitu.

Unaambiwa alitoka pale moja kwa moja kuomba uhamisho kurudi kwao.

Sent using Jamii Forums mobile app

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mwaka fulani nikiwa katika mafunzo ya JKT katika kambi moja wapo hapo Kigoma,
Kuna ServiceMan mwenzetu alimua kapangiwa lindo huko ndichi mashamani, mchana akiwa lindoni akakutana na bibi kabeba mkungu wa ndizi za jeshi, Basi Service akachukua ndizi na bibi akarushwa sana kichura, mwendo wa bata na kupiga push za kutosha kisha akaachiwa andoke zake.

Jioni jamaa anarudi Hangani(Dom) baada ya kukabidhi silaha akaanza kuumwa sana mpaka asubu ni mahututi, hospitali wanadai hawaoni ugonjwa basi Nyumbani kwao wakamuomba akaenda kutibiwa na akapona, Siku anarudi kambini ile hali inaanza upya, akitoka nje ya kambi mzima ila akiingia kambini hoi. Mpaka Utawala wakamumisha Kambi.

Shkmaooo Kigoma.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hivi visa kusoma usiku unatisha...ngoja niende kwa walaji matunda kimasihara nisije kuota vitu vya ajab ajabu
Unanikumbusha dada yangu alinikuta natizama movie ya Matrix usiku. Kunikuta akaunga tela. Usiku mnene alivyolala ghafla akawa anapiga makelele. Wazazi kuja mbio mbio kumuuliza nini akanitaja mimi. Mama akanijia akaanza; umemfanyaje dada yako (?) Unaangalia madude yako huko unamtisha mwenzako. Sitaki kabisa uangalie madude yako na mwenzako akiwepo!

Nikabaki hee! Movie ya Matrix anaota! 😂😂😂 miaka ya nyuma hiyo!
 
Duh, mimi nimeshuhudia uchawi wa kutisha kwenye nchi moja inaitwa Tanzania.
Kuna li Chama inaitwa CCM, tangu mwaka 1961 hadi leo 2029 watu wanalala kwenye nyumba Kama mabanda ya nguruwe na kula yao ni taabu lakini wanavumilia tu badala ya kutumia nguvu kuyatoa ma CCM, ama kweli uchawi upo

Sent using Jamii Forums mobile app
Dah, CCM tuna taabu sana mwaka huu
 
Hii iliwahi mtokea mmshkikaji mmoja bwenini. Yaan jamaa alitoka mara nne nje ndani ya saa moja, nioashangaa jamaa mmoja mlokole anaanza kukemea pepo, ndipo yule jamaa akaa cha kujiskia mkojo. Ila ile hali Haikuwahi kujirudia tena pale bwenini
Nimekumbuka hiki kisa,

Mbeya mjini nilikutana na kisanga cha kubebeshwa mkojo na wazee wanacheza drafti, bao na kunywa kahawa,
Unakuta wanacheza wewe unaenda shangaa pale (mimi nilikua nasubiri coaster za usiku za dar) nimeshangaa wee baada ya dk 20 hivi nkabanwa mkojo nkarudi kwa mwenyeji nkamuomba anielekeze pa kujisaidia, nimerudi kujisaidia naenda kushangaa na kuskiliza stori zao, yaani ndani ya lisaa nilienda chooni mara 3, nkawa najisemea mapema yote hii hata maji sijanywa mkojo mwingi hivi?
Kwa sababu nilikua na safari niliogopa kunywa maji japo nilikua na kiu sana kwa hofu ya kusumbua gari njiani kuchimba dawa,

Gari ilivyokuja nkaanza pakia carolight zangu nkamaliza nilipotaka kurudi pale kuendelea kushangaa mwenyeji wangu akaniambia twende huku (hapo tunasubiri gari ijae abiria) tukakaa mahali tunapiga stori za hapa na pale ndio akaniambia nimekuona unabebeshwa mikojo tu hata huelewi, nkabaki namshangaa...
Ndio akaniambia ukienda shangaa pale kama hauko vizuri wale wazee wakiskia mkojo wanakubebesha wewe unaenda kuukojoa badala yao, yaani wanaweza kukaa asubuhi hadi jioni hata chooni wasiende ila wee kila mda unapiga ruti tu..
Hiyo ilikua mwaka 2010 pale uyole.

Sent using Jamii Forums mobile app

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Sasa wewe unanijibu swali kwa swali halafu hapo hapo unanisema nina maswali?

Sayansi imethibitishwa kwa mantiki isiyokanushika katika majaribio yanayoweza kurudiwa na wengine kwa uthibitisho zaidi.

Wewe uchawi unauthibitishaje huu ni uchawi na si kitu kingine usichokijua?
Tusibishane Sana Wakati Kuna obvious solution
Hicho kitu tusichokifahamu ndio tumekipa Jin la 'Uchawi:
 
Wale waliosoma boarding mnamkumbuka miss corridor sjui nyie mlimwiitaje in short huyu ni jini huwa anatembea ukumbuni kwenye mabweni mashuleni au makambini au maholi tulitunga hilo jina sababu akitembea unaskia "ko, ko, ko " ile sauti kama ya viatu vya kike vyenye visigini virefu ukienda angalia huoni mtu ukibahatika unamuona mwanamke ana nywele ndefu kakupa mgongo anamalizia kukata kona

Sent using Jamii Forums mobile app
inasemekana kwa mabinti girls walikuwa wanafuata kulamba damu za hedhi,kwa wanaume wanafuata mkuyenge(ndio pale kwenye ndoto nyevu).

kimbembe kuwe na mmoja wenu ana mapepo humo ndani[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23].
 
Gamboshi ipi?je ni ile ya kuonekana au isiyoonekana?

Sent using Jamii Forums mobile app
Aseee, nilikuwa nasearch Gamboshi hapo Google map na haya ndo majibu:

Screenshot_20200105-114553.jpeg


I moved your cheese!
 
Back
Top Bottom