Kisa kingine cha Kaka yangu mtoto wa Mama yangu mdogo.
Yeye kipindi hicho alikuwa amemaliza chuo akarudi Kijijini nyumbani kwao.
Huko akawa na mahusiano na binti fulani,baada ya muda alipata kazi akaja huku mjini..Mambo yakakaa sawa akataka kumuacha yule mwanamke, yaani alirogwa mdomo ulipinda .. Sasa Kuna siku alikuja nyumbani kwetu(kwa mamkubwa wake) kusalimia nikawa namshangaa mdomo upo pembeni kabisa ila haumwi chochote.
Kumuuliza mama ndiyo akanihadithia kwamba huko kwao familia ya binti ilimroga.
Ilibidi aendelee na yule mwanamke,baadaye akamuoa..tukafunga safari Hadi huko Kijijini tukacheza harusi.
Akamchukua mkewe wakaenda kuishi mjini.Yule dada alikuwa mrembo jamani huwezi amini Kama ni mchawi.
Mkewe akapata ujauzito,wanaendelea kuishi na mimba ilikuwa kubwa tu Kama miez 6-7.
Kumbe usiku wakilala yule dada alikuwa anaondoka kimazingara anaenda anakoenda asubuhi anarudi.
Wachawi wao kanuni yao akiondoka usiku ,mwili unabaki pale kitandani na inabidi usimuamshe.
Sasa yule Kaka alistuka usiku akamstua akaona mtu hatikisiki.
Yule dada aliondoka akaenda Kwenye anga ya sumbawanga huko na mama yake ,wameenda kuwanga huko wakazidiwa nguvu.(haya yalikuwa maelezo ya mama ya huyo dada)..huku Kaka alivyozidi kumuamsha ndipo alipoharibu Mambo.
Amsha dada haamki,kuita majirani amsha mtu haamki,kumpeleka hospital kumpima amekufa yeye na mtoto tumboni.
Mama wa huyu dada msibani alilia Sana,akaanza kumlaumu huyu Kaka kwanini alimuamsha mwanawe,alivyoona Mara ya kwanza hajatikisika angemuacha na asingeita watu.
Yule dada akawa amekufa hivyo,mtoto akatolewa tumboni ..wakazika.
Huyo binti ndiye alikuwa anaenda naye safari zake zote.
Baadaye mama mtu anamwambia yule Kaka kwamba ampe binti yake mwingine aliyebakia..
Huyo Kaka aligoma kabisa.
Hicho Kijiji hakijaendelea bado.. yaani Kuna wachawi hatari.
Sent using
Jamii Forums mobile app