Kama unaingia Mkataba ulipwe Mshahara kidunchu unategemea nchi yako ifanyeje?

Kama unaingia Mkataba ulipwe Mshahara kidunchu unategemea nchi yako ifanyeje?

Robert Heriel Mtibeli

JF-Expert Member
Joined
Mar 24, 2018
Posts
28,297
Reaction score
68,017
Habari Wakuu!

Mambo yetu yanasikitisha mno. Yanahuzunisha Sana.

Tumezoea kulalamika.
Tumezoea kulaumu wengine huku Sisi tukifanya yaleyale.

Taikon sitaki kumlaumu yeyote. Siku zote nitakuwa msema ukweli hata Kama unaumiza.
Ukweli ndio dawa pekee ya kuikomboa nchi.

Hakunaga maendeleo pasipo kujitoa kafara!
Hakunaga Amani pasipo ncha ya Upanga.

Wananchi masikini tumekuwa tukilalamikia viongozi wetu kuwa wanaingia mikataba mibovu ya kinyonyaji isiyoinufaisha nchi. Lakini sisi nasi tunaingia mikataba hiyohiyo katika level zetu za maisha kuajiriwa na kupewa mishahara kidunchu.

Ukiona nchi au taifa lolote watu wake wanaogopa Kifo na wapo tayari kuuza utu na haki zao ili angalau waweze kuishi, taifa hilo kamwe haliwezi kuendelea Ng'oo. Taikon ndio nimeshasema baada ya kupeleleza Kwa muda mrefu.

Mtu atasema; Bora nifanye hiki kibarua ilimradi maisha yasonge hata Kama ananyonywa haki zake.

Viongozi wa nchi wataendelea kuingia katika mikataba ya kinyonyaji Kama vile wananchi wake tunavyoingia mikataba ya kinyonyaji katika vibarua vyetu.

Nchi inajengwa kuanzia ngazi ya familia.
Ikiwa familia nyingi watu wake wapo Radhi waingie mkataba wowote hata kama wakinyonyaji ili Familia zao zipate Kula unafikiri Kwa level ya kitaifa ambayo ni viongozi watafanya nini zaidi ya wao nao kuingia mkataba wowote ilimradi familia zao na kidogo nchi Yao ipate chochote.

Ikiwa Wafanyakazi wao kila siku ni kulalamika wanalipwa Mishahara midogo na wanashindwa kujitetea unafikiri wananchi haohao siku wakija kuwa viongozi wakawa wanalipwa angalau mishahara mikubwa watapigania haki za wananchi? Jibu ni hapana.

Kama mtu kashindwa kutetea haki zake iweje aweze kutetea haki za watu wengine?

Kama tunahitaji kuibadilisha jamii yetu itatupasa kila mmoja wetu aache Ubinafsi.
Jamii yetu imejawa na watu Wabinafsi kuanzia masikini Kabisa mpaka Tajiri Kule juu.

Nipumzike sasa!
 
Nimesoma kichwa cha habari tu bila shaka umeandika upopoma

Ungeijua njaa na umaskini ungekaa kimya.
 
Unajua shida wewe?
Unaijua njaa wewe?
Kama umebarikiwa kula na kusaza mshukuru Mungu,na kama unalipwa mshahara mnono pia shukuru,kuna familia wanaishi kwa mshahara wa 120,000/=na bado kuna mamia ya watu wanaitaka hiyohiyo kazi tena kwa kuomba na kupiga magoti.
 
Ukiona nchi au taifa lolote watu wake wanaogopa Kifo na wapo tayari kuuza utu na haki zao ili angalau waweze kuishi, taifa hilo kamwe haliwezi kuendelea Ng'oo. Taikon ndio nimeshasema baada ya kupeleleza Kwa muda mrefu.
Kweli mleta mada una hoja. Kule Ukraine mpk wabunge wanapanga foleni kwenda ili kugawiwa silaha wakapiganie nchi yao.

Ingekuwa hapa bongo Kuna mwananchi ama mbunge angepanga foleni kwenda kupewa silaha ili aende vitani.

Ili kufanikisha manunuzi kwa wabunge na madiwani wa chadema, ccm wakati wa awamu ya tano waliwatishia kwa kuwanyang'anya mali zao, kuwaua na kuwazushia kesi. Wabunge na madiwani wa chadema wakaufyata na kuamua kuunga juhudi.

Nchi hii Ina watu wa ajabu sana
 
Kweli mleta mada una hoja. Kule Ukraine mpk wabunge wanapanga foleni kwenda ili kugawiwa silaha wakapiganie nchi yao.

Ingekuwa hapa bongo Kuna mwananchi ama mbunge angepanga foleni kwenda kupewa silaha ili aende vitani.

Ili kufanikisha manunuzi kwa wabunge na madiwani wa chadema, ccm wakati wa awamu ya tano waliwatishia kwa kuwanyang'anya mali zao, kuwaua na kuwazushia kesi. Wabunge na madiwani wa chadema wakaufyata na kuamua kuunga juhudi.

Nchi hii Ina watu wa ajabu sana


Ubinafsi ni kitu kibaya Mno.

Kama nchi yetu ingekuwa haina ubinafsi masuala ya utekaji wala usingeyasikia.
Angetekwa mmoja alafu wengine wangeandamana mpaka serikali iwajibike.

Lakini anatekwa wakwanza, kimya, wananchi kimya, serikali kimya.
Wapili, kimya
Watatu, kimya.
Huo Kama sio ubinafsi ni nini?

Mtu ananilaumu kiongozi kuingia mkataba mbovu wakati naye kaingia mkataba mbovu wa kulipwa laki na 20. Huoni huo ni upuuzi.

Sababu watakuambia Mimi napigania hela ya Kula, kiongozi naye atakuambia vivyo hivyo
 
Unajua shida wewe?
Unaijua njaa wewe?
Kama umebarikiwa kula na kusaza mshukuru Mungu,na kama unalipwa mshahara mnono pia shukuru,kuna familia wanaishi kwa mshahara wa 120,000/=na bado kuna mamia ya watu wanaitaka hiyohiyo kazi tena kwa kuomba na kupiga magoti.

Shida hazilingani Mkuu Acha hasira 😀😀

Wakati wewe ukikosa chakula cha ugali mlenda na inakupasua kichwa.
Kuna mwenzako anapasuka kichwa na anashida ya kwenda Kula Paris na anakonda na kuona maisha magumu.

Kwenye maisha kila mtu anaurefu WA kamba yake.

Usije ukadhani shida yako ya kukosa Kodi ya elfu 50 wewe ndio unateseka pekeako, wapo wanateseka Kama unavyoteseka wewe Kwa kuishi jumba kubwa ambalo halijabadilishwa samani za Ndani Kwa miaka mitatu.

Muhimu watu waache Ubinafsi.
Ubinafsi ni pamoja na kujiona unateseka wewe kuliko wenzako kisa unawaona wanauafadhali.

Umasikini na shida ni jinsi ulivyo iseti akili yako(set of mind)
 
Kweli mleta mada una hoja. Kule Ukraine mpk wabunge wanapanga foleni kwenda ili kugawiwa silaha wakapiganie nchi yao.

Ingekuwa hapa bongo Kuna mwananchi ama mbunge angepanga foleni kwenda kupewa silaha ili aende vitani.

Ili kufanikisha manunuzi kwa wabunge na madiwani wa chadema, ccm wakati wa awamu ya tano waliwatishia kwa kuwanyang'anya mali zao, kuwaua na kuwazushia kesi. Wabunge na madiwani wa chadema wakaufyata na kuamua kuunga juhudi.

Nchi hii Ina watu wa ajabu sana

Rwanda hapo Waziri ama balozi ni wanapanda economy. Ni sheria. Na hospitali wote mnapanga mstari kumsubiri daktari unless waone aibu wahusika kumrukisha kiaina. Ukraaine mbali sana huko mkuu kulinganishia.
 
Habari Wakuu!

Mambo yetu yanasikitisha mno. Yanahuzunisha Sana.

Tumezoea kulalamika.
Tumezoea kulaumu wengine huku Sisi tukifanya yaleyale.

Taikon sitaki kumlaumu yeyote. Siku zote nitakuwa msema ukweli hata Kama unaumiza.
Ukweli ndio dawa pekee ya kuikomboa nchi.

Hakunaga maendeleo pasipo kujitoa kafara!
Hakunaga Amani pasipo ncha ya Upanga.

Wananchi masikini tumekuwa tukilalamikia viongozi wetu kuwa wanaingia mikataba mibovu ya kinyonyaji isiyoinufaisha nchi. Lakini sisi nasi tunaingia mikataba hiyohiyo katika level zetu za maisha kuajiriwa na kupewa mishahara kidunchu.

Ukiona nchi au taifa lolote watu wake wanaogopa Kifo na wapo tayari kuuza utu na haki zao ili angalau waweze kuishi, taifa hilo kamwe haliwezi kuendelea Ng'oo. Taikon ndio nimeshasema baada ya kupeleleza Kwa muda mrefu.

Mtu atasema; Bora nifanye hiki kibarua ilimradi maisha yasonge hata Kama ananyonywa haki zake.

Viongozi wa nchi wataendelea kuingia katika mikataba ya kinyonyaji Kama vile wananchi wake tunavyoingia mikataba ya kinyonyaji katika vibarua vyetu.

Nchi inajengwa kuanzia ngazi ya familia.
Ikiwa familia nyingi watu wake wapo Radhi waingie mkataba wowote hata kama wakinyonyaji ili Familia zao zipate Kula unafikiri Kwa level ya kitaifa ambayo ni viongozi watafanya nini zaidi ya wao nao kuingia mkataba wowote ilimradi familia zao na kidogo nchi Yao ipate chochote.

Ikiwa Wafanyakazi wao kila siku ni kulalamika wanalipwa Mishahara midogo na wanashindwa kujitetea unafikiri wananchi haohao siku wakija kuwa viongozi wakawa wanalipwa angalau mishahara mikubwa watapigania haki za wananchi? Jibu ni hapana.

Kama mtu kashindwa kutetea haki zake iweje aweze kutetea haki za watu wengine?

Kama tunahitaji kuibadilisha jamii yetu itatupasa kila mmoja wetu aache Ubinafsi.
Jamii yetu imejawa na watu Wabinafsi kuanzia masikini Kabisa mpaka Tajiri Kule juu.

Nipumzike sasa!
Umegonga mule mule. Waafrika tunauza Utu wetu sana. Wa Waajiri walishaona Watu wengi wapo Mtaani kwahiyo wanakuwa na Viburi pia katika Kuajiri. Maana Ukiacha Wewe anatamba Acha Ajira niwaajiri wengine
 
Umegonga mule mule. Waafrika tunauza Utu wetu sana. Wa Waajiri walishaona Watu wengi wapo Mtaani kwahiyo wanakuwa na Viburi pia katika Kuajiri. Maana Ukiacha Wewe anatamba Acha Ajira niwaajiri wengine

Niliwahi andika Makala hii


Hata viwanda vijengwe nchi nzima bado Kwa akili za Watanzania bado watateseka tuu.
Ubinafsi
 
Watanzania ukitoa Mbowe, Lissu, Maria Sarungi na Fatuma Karume wengine wote ni wanafiki wakubwa

 
Back
Top Bottom