Elections 2010 Kama unaitakia mema Tanzania usimchague Mh Slaa

mpeni pole huyu mshakaji hajui analoliongea inawezekana aidha baba yake anacheo serikalini!au kashaahidiwa kitu flani,au alilamba fedha za epa maana wamepewa hadi 31/10 wawe wamezirudisha ndio itakuwa pona yao.embu muulizeni vizuri huyu jamaa
 
Tutamchagua mama yako usiwe na wasiwasi,This is another lunatic person!!!!!!!!!!
 
Huyu Lazima atakua na PEPO Mchafu,
Hajui anenalo.
 

Dadangu Zawadi, huitakii mema hii nchi. Sahau itikadi zako za kidini tuijenge Tanzania.
Chagua Dr. Slaa kwa maendeleo ya nchi yako na si Kikwete kwasababu ni mwislamu mwenzako. Wakristo hatuna tatizo na suala la dini ndo maana Kikwete alishinda kwa kishindo kwenye uchaguzi uliopita maana yake ni kwamba hata mimi mkristo nilimpa kura yangu nikitarajia kuwa ataiongoza vyema nchi hii. Lakini ameshindwa kwahiyo tunamchagua mtu mwingine aliyeonyesha nia ya kweli ya kuwakomboa watanzania toka katika lindi la umaskini ili hali nchi yao imejaa utajiri wa kila namna.
 
Tuchukulie kwamba uko sahihi; kwamba Dr. Slaa ni dikteta, sasa unatupa uchaguzi upi mbadala unaofaa? JK na CCM? Pengine (ili kuthibitisha kwamba unayo mantiki) basi angalau ungesema kwamba Watanzania safari hii hatuna pa kuponea: ni ama "dikteta" Slaa au kibaraka wa mafisadi na ufisadi JK (tena asiye na visheni yoyote zaidi ya kuwazia misaada toka nje). Udikteta vs. usanii? Kwa kifupi haujatusaidia kitu.

Kama mtu wako ni JK sijui ni mema gani unayoitakia TZ? Sisi wengine tunataka mabadiliko na Slaa anaonyesha nyota mpya. Kama ana dalili za udikteta pia unahitajika. Katika taaluma ya uongozi, kiasi fulani cha udikteta (hapa naita ujasiri) ni muhimu kudhibiti mabaradhuli. Hatuwezi kuendelea kuchekea usanii wa JK, Makamba, na skwadi la mafisi akina Kinana, EL, RA, n.k. Kama wewe ni mpiga debe wao basi ni heri uanze kusoma alama za nyakati na kutafuta mustakabali mpya. JK na CCM bila ulaghai hawauziki leo hii! :nono:
 
wewe una myopic vision
hujui ni bora uongozwe na dictator kuliko mafisadi?
kuna nchi kibao tu ambazo hazina democrasia kama China lakini wanamaendeleo makubwa tu na sasa ndio gumzo dunia nzima.
Cha mhimu ni kuwatumikia wannchi ,kwa nchi kama hii ya Tanzania ilipofikia ni lazima kuwe na kiongozi mwenye SURA MBAYA(na maanisha mkali,asiyecheka na uchafu wowote) ndio tutabadilika lasivyo mabadiliko mtaendelea tu kuyasikia.
Nchi wananchi wengi ni wazembe sana,porojo ni kubwa kuliko kazi wewe unadhani kubadilisha system ni kazi rahisi? lazima tuwe na watu kama SLAA sio Raisi wakucheka na mafisadi.

VIVA SLAA,
VIVA CHADEMA
 


Hatuwezi jibu hoja za MASHOGA hapa..
 
Unaipenda Tanzani? Msikilize tu Mh Slaa lakini kura yako mpe Kikwete.


Kwa hiyo una maana kwamba option iliyoko ni kumrudisha yule yule aliyeshidwa kungoza nchi? Wewe naona ni mtu ambaye HUNA HOJA ila una enjoy ku tease watu na kuona wanavyokasirika! Nimeshakushtukia wewe kwa hiyo NA MIMI SIPOTEZI MUDA KUKUJIBU KWA HOJA.
 
Ni kweli kabisa kumchagua Slaa ni sawa na kupotea kwenye msitu mnene wenye wanyama wakali ,jamaa ni sawa na kipofu kiutawala itambidi apapase kwelikweli ili kutoa serikali yenye kuona mbali ,alafu ukiangalia huyo mgombea mwenza ,aloo ni balaa tupu ,itabidi nae akabidhiwe shughuli za mikasi.
 
Fafanua neno hili tafadhali "USICHAGUE CHAMA, CHAGUA MTU" Mbona mnajibu hewa, na ktk uongoizi ndio mtakuwa hivyo hivyo. tumewagundua!

CCM wenyewe walishachagua mtu badala ya chama. Ndiyo maana Makamba alisema wazi JK ni maarufu kuliko chama na vileviel ndiyo sanbabu kampeni zinafanywa na Baba, Mama na Mwana na siyo chama!!!

Kwa hiyo ushauri wa bure, kama unachagua Chama chagua CHEDEMA kama unachagua mtu au familia chagua JK!!!
 
Great Thinker in the making............CCM ni sawa na samaki aliyeharibika, labda kichaa peke yake ndo anayeweza kumla.
 

"To hell"....RIP( Z.N+MWIBA)...Let us live!..it's a new world,you don't know what time it is?
 

Kwa hiyo Tanzania tutakuwa na Madictactor Wawili kama Slaa akishinda, Nyerere wa kwanza, wa pili Slaa.
Nimesikiliza sana hotuba zake na nimegundua huyu jamaa Dr. Slaa hana UWEZO wa kuwa rais.
 
Kwa hiyo Tanzania tutakuwa na Madictactor Wawili kama Slaa akishinda, Nyerere wa kwanza, wa pili Slaa.
Nimesikiliza sana hotuba zake na nimegundua huyu jamaa Dr. Slaa hana UWEZO wa kuwa rais.

Ili kuonesha kwamba una UWEZO wa kuwa Rais wa Tanzania (your definition), unatakiwa kusema nini?
 
Fafanua neno hili tafadhali "USICHAGUE CHAMA, CHAGUA MTU" Mbona mnajibu hewa, na ktk uongoizi ndio mtakuwa hivyo hivyo. tumewagundua!

Sijaona neno la kufafanua hapo.

Umegundua kuwa hatufuati upepo eeh?
 
Zawadi Mdogo wangu (i'm sure your are under 18)

haukatazwi kumpigia unaemtaka kura kwa kuwa ndio wanaowaweka mjini, si unajua kodi zetu zote anatumia kuwahonga wazazi wako, na hivyo mna'kaunafuu wa maisha hivyo unaona anafaa na unataka aendelee kuwepo hapo ili nyinyi wachache muendelee kuneemeka. But for Us, hatuwerzi kumpigia kura mtu ambaye amesababisha gharama za maisha kupanda, wakati pato letu halijapanda.

bAHATI MBAYA HAUTOWEZA KUPIGA KURA, SO TELL WAZAZI WAKO WAMCHAGUE TU HUYO FISADI BUT HATOPITA KWA KUWA WENGI TUTAPEWA AMBAO NI DR. SLAA (CHADEMA)

Usiku mwema katotoo
 

Hoja yako No 1 nimeielewa una maana nini, kwa hiyo tegemeo la Mh Slaa ni kwamba muhimili wa Bunge hatauhitaji? Kwa vile ataendesha mambo yake huku Bunge likimpigia magoti, na kuwa Bunge la Bendera.

Tuache utani wewe binafsi unaunga mkono hili. Je kuna Demokrasia hapo? Na kama hakuna Demokrasia basi nu UDIKITETA ndio utaotawala.

Katika hoja yako hii, unafanya makosa makubwa sana, tena ni makubwa sana. Bunge la Tanzania la leo kwa jinsi lilivyozoea uhuru lililopewa na JK, HALIWEZI kurudi nyuma na kuwa kama hivyo usemavyo.

Kitu usichokielewa ni kwamba, mambo yalikuwa rahisi kwa CCM kwa sababu walikuwa na wabunge tosha kupitisha hoja, kitu ambacho panga pangua CHADEMA hawawezi kupata. Sasa huyo Mh wenu akiwa na nadharia hizo ulizo nazo wewe ataipeleka nchi pabaya.

Mimi napenda wapinzani washike nchi, lakini sipendi wajaribu kushika nchi. Kwa umasikini tulio nao hatuna muda wa kujaribu!
Na uchaguzi si lelemama, tusifanye utani jamani, CHONDE CHONDE!

Hoja yako ya pili sina haja ya kuijibu, ukweli nimechoshwa na uchochezi wa Udini, au na wale waombao kura kupitia nyumba za ibada. Sina la kujibu.

Ujumbe wa leo: Ni rahisi kuharibu amani, lakini ni vigumu kuirudisha amani. Ukitaka kuharibu amani, mpe kura yako Mh Slaa.
 

YouTube - Nyerere Rushwa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…