Kama unataka kujua meli zinazoingia Bandarini Dar na Bandari shindani, angalia website hii

Unaweza kuangalia idadi ya meli zinazoingia Bandalini Dsm na Bandali Jirani ambazo ni shindani. Hii itonyesha kama kweli sisi hatupati meli au tunasema tu bila kuwangalia

http://www.marinetraffic.com/en/ais/index/ports
Hatujasema hatupati na hakuna aliesema hivyo, Ila kinachozungumzwa ni mizigo kupungua! Usibadilishe mada, huo ndio msingi wa hoja!!
 
Kwa nini watu wanashindwa kuelewa ukweli mwepesi?
1. Meli zilzokuwa zinaleta mizingo ya kiujanjajanja na kukwepa kodi haziji tena bandari ya Dar. Zimehamia kwingine.

2. Kwa hiyo meli zinazokuja Dar zimepungua maana zimebaki zile tu za mizigo halali zisizokwepa kodi ya serikali.

3. Makusanyo ya kodi kwenye bandari ya Dar imeongezeka mara dufu.

4. Sasa tatizo ni lipi? Unataka tu mameli yajazane pale bandarini yakipiga dili sisi hatupati kitu, ndiyo ufurahi? Au sisi tunachotaka si ni pesa?
 
Mkuu hapo namba tatu jipange upya
 
Ukiangalia idadi ya Meli zilizopo bandarini kwa sasa Dar ni (12), Tanga (0), Mtwara (2) na Mombasa ni (29). Kwa leo hii, Bandari ya Mombasa wametuzidi sana.
ukijumlisha na expected mombasa wana 65 sie 34

halafu hzo 34 zina mizigo kiduchu ya wafanyabiashara wasio na mali za maana!
tunaambiwa zimeingia tani elfu 1 badala ya elfu 40

kodi yetu imepanda sana tena mara mbili ndo mana watu wamepotea!
kodi ingekuwa ni ile ile tungekuwa tunacheza na 1.5 trilion na ushee


beira na maputo pana meli 100

yan mpaka najiskia kulia
 
Hatujasema hatupati na hakuna aliesema hivyo, Ila kinachozungumzwa ni mizigo kupungua! Usibadilishe mada, huo ndio msingi wa hoja!!
Kateleza huyoo
 
Haina neno hata kama zimepungua hizo meli tunafidia kwenye VAT kwetu sisi wananchi. Tutakamuana wenyewe kwa wenyewe mpaka mhame nchi.
 
Unaweza kuangalia idadi ya meli zinazoingia Bandalini Dsm na Bandali Jirani ambazo ni shindani. Hii itonyesha kama kweli sisi hatupati meli au tunasema tu bila kuwangalia

http://www.marinetraffic.com/en/ais/index/ports
Nimefungua haifunguki. Lkn jana niliangalia tv1 habari, makampuni ya kusafirisha mizigo kwa njia ya bahari yako hoi. Kuna moja limetangaza hasara ya usd 5 billion ndani ya wiki moja. Hivyo hali ni tete kwa wote
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…