Kama Walioua ni "Wasiojulikana" Then Karma, Albadir Itawahusu, ila kama ni 'Wasiojulikana', Hata Albadir Haisaidii Kitu, Wametimiza Tuu Wajibu Wao!

Kama Walioua ni "Wasiojulikana" Then Karma, Albadir Itawahusu, ila kama ni 'Wasiojulikana', Hata Albadir Haisaidii Kitu, Wametimiza Tuu Wajibu Wao!

Pascal Mayalla

Platinum Member
Joined
Sep 22, 2008
Posts
53,857
Reaction score
121,995
Wanabodi,

Najua wengi wetu wameumizwa sana na kifo cha kikatili cha Mzee Ali Mohamed Kibao, natoa tena pole kwa wote.

Watu wamekasirika hadi kuwasomea Albadir, hivyo mimi kama kawaida yangu, kama kuna kitu nakijua, huwa na share, leo naomba kushare kuwaelimisha kidogo kuhusu wauaji na utendaji kazi wa Albadir ambayo inafuata kanuni ya karma.

Je wajua kama walioua ni "wasiojulikana", then Karma, Albadir Itawahusu, ila kama ni 'wasiojulikana', then hata Albadir haiwezi kusaisaidia kitu, kwasababu wauaji hao ni walikuwa wametimiza tuu wajibu wao!.

Kama wauawaji hao ni watu "Wasiojulikana", then karma na Albadir itawahusu, na watalipwa kwa matendo yao na uovu wao, lakini kama waliofanya mauaji hayo ni watu 'wasiojulikana', then sio karma wala Albadir inaweza kuwafanya chocolate, kwasababu walikuwa wanatimiza tuu wajibu wao!.

Naomba kujitambulisha tena na tena ili kusaidia kuwaelimisha wengine kuhusu utendaji kazi wa kitu kinachoitwa "the operatives", mimi nimezaliwa na wazazi wangu wote wawili, baba na mama, wote ni waserekali.

At this juncture naomba ku declare interest, kuwa mimi Paskali Mayalla napinga mauaji ya aina yoyote na hata adhabu ya kifo iko kinyume cha katiba ya JMT, na mimi ni miongoni mwa watu tunaopinga adhabu ya kifo - Wana JF tuungane kusema NO hukumu ya kifo

Serikali zote duniani zina utaratibu wake wa kufanya kitu kinachoitwa "elimination" of dissidents. Ile mwaka 1976 kwenye ile kesi ya mauaji Mwanza, Mzee wangu alihusika na mimi kuzishuhudia baadhi ya zana za kazi baba akirudi nazo usiku mkubwa. Nawaomba mkisikia baadhi ya maofisa wa jeshi, polisi na usalama wa Taifa wanakuwa walevi wa kutupa, wasameheni tuu, kwa mambo wanayoyapitia kazini, baada ya kustaafu yanakuja kuwa hunt, sasa ili kujisahaulisha, kunapelekea most of the times wawe wako bwii!.

Hivyo kuna watu wanaajiriwa na kupewa mafunzo rasmi ya elimination. Majeshi yote yana watu hawa, wanaitwa wadunguaji, snipers, hivyo hata mimi nikiwa jeshini JKT Makutopora kwa mujibu wa sheria, kwenye somo la range, nilihit the bull 9/10, hivyo nilipomaliza tuu jkt nilipelekwa moja kwa moja JWTZ, Airwing na huko tukaanza moja deppo nyingine ya jeshi kweli sio ile ya JKT kama jeshi!.

Huko sasa nikadungua 10/10!. Mmoja wa waalimu wangu Afande Kahamba, Sstg. akatufundisha kuwa kazi ya polisi ni kulinda usalama wa raia na mali zake, kazi ya usalama wa Taifa ni kulinda Serikali iliyopo madarakani na kazi ya jeshi ni kulinda nchi. Kwa upande wa jeshi shughuli kuu ya askari jeshi ni kuua tuu, hakuna mjadala, hakuna mahojiano, ukimuona adui, mmalize kabla hajakumaliza!, nothing more nothing less, just kill!.

(Ila kumbe mtu ukiwa na shabaha ya udunguaji kwa bunduki, unakuwa na shabaha kwenye bunduki zote mbili, kwenye ile bunduki ya pili, nimeisha dungua risasi 9!, na hapo ni zile shots za direct golini, tukija mipira ya kona na me hi za ugenini, usipime!. )

Tena mkiwa mstari wa mbele mkapigwa ambush, ni mnatawanyika na hakuna tena kusubiri amri, ni unatumia tuu initiative yako kujiokoa!.

Na katika kujiokoa, au kumetolewa amri ya retreat, wakati mnarudi nyuma kujiokoa, askari mwenzako akajeruhiwa kwa risasi, hamuwezi kumbeba, wewe unatakiwa kumfariji kwa kumlambisha morphine ili kumpunguzia maumivu, halafu unatakiwa kumfanya kitu, wanaita do the needful!, kisha mnaendelea na safari.

Wale ma komandoo, huwa na vidonge kabisa vya cyanide, ukikamatwa na adui kwenye infiltration, kuliko kisubiri kuhojiwa, unajimezea kidonge na kujtendea favours, unaondoka kishujaa!, ndio maana Wahehe jeshini ni wengi!.

Nikaanza kulichukia jeshi!.

Kumbe kambi hiyo ya Airwing ndipo wanapoendeshea Mahakama ya Kijeshi Court Marshall nikashuhudia kalinye kalinye za maofisa wa jeshi wakihukumiwa Mahakama ya Kijeshi, kiukweli niliaga jeshi kwa amani nikaenda kujiunga na TSJ nikawa mwandishi wa habari na mtangazaji.

Sasa kwenye hizi eliminations ziko mbinu mbalimbali za eliminations naomba hapa nisizitaje nisije kutoa siri za kambi ila hakuna justification yoyote kumuua binadamu kwa ukatili wa kiasi kile, the professionals wana njia nyingi za eliminations, swift and clean job and left without any trail behind!, Azory Gwanda or Ben Saanane, up to date no one knows what happened to them!, ndio maana Mama Samia alisema wale wasiojulikana wa pyu pyu za Tundu Lissu ni ma amateurs, wangekuwa ni watu wa kazi zao, saa hizi tungekuwa tunazungumza mengine!.

Wenzetu wa nchi zilizoendelea hadi wanatumia technology kama polonium, mtu unaondoka taratibu...!.

Sasa kwa vile kuna watu jukumu lao ni kuua, watu hao wakitumwa kumuua yoyote, sio jukumu lao kujua amefanya nini, wao wakipewa amri halali ya eliminations, kazi yao is to eliminate, how, ni juu yao!.

Hivyo kwenye Utekelezaji wa eliminations wao wanatimiza wajibu wao, hivyo kama mlengwa was shortlisted kwenye list ya eliminations, na akawa eliminated, karma ya eliminations is upon aliyetoa amri, sio wao watekelezaji!, haiwahusu, hata msome Albadir haiwahusu kwasababu wao walikuwa wanatimiza tuu wajibu wao!.

Hata vitani bonus likipigwa linauwa wote wanaohusika hata wasio husika na mtenda dhambi sio mlipua bonus bali mtoa amri!.

Ndio maana nimesema kama waliofanya ukatili huu ni watu "wasiojulikana" then karma na Albadir itawahusu lakini kama ni wale 'wasiojulikana', karma wala Albadir haiwahusu!.

Ila ili eliminaons ifanyike kihalali, lazima CinC asaini death warrant ya hiyo operation ya eliminations.

Askari polisi, jeshi na usalama wa taifa, wanapoau kwenye kutimiza majukumu yao, sio dhambi!, hata vifo vya watu wasio na hatia, vinapotokea kwenye operations zozote, hatia ya damu isiyo na hatia sio kwa watekelezaji bali kwa waliopanga na kutoa amri ya Utekelezaji!

Kwa wasio jua tofauti kati ya "wasiojulikana" na 'wasiojulikana' karibu pande hii Shambulio la Lissu: Wajue wasiojulikana watakaojulikana na 'Wasiojulikana' ambao kamwe, hawatajulikana

Lengo la elimu hii ya eliminations sio mimi kuonyesha kuwa na support eliminations, No!, msimamo wangu uko wazi na kwenye gazeti la Mwananchi la leo, nimeandika!. Ombi kwa Rais Samia, tunakushukuru kwa mahubiri mazuri kuhusu haki, tunakuomba utende unachohubiri yasibaki kuwa maneno tuu lakini vitendo ni tofauti na pia kizungu nimeandika Mama don't preach. I think we've had enough of Preaching about law, justice & human rights. Would you Please just Practice what you Preach?

Ndio maana nikashauri TISS Ikanushe tuhuma za uvamizi, utekaji, utesaji na mauaji!. Wasijadiliwe na Bunge kwa uwazi bali wachunguzwe, wakithibitika wafumuliwe!

Wasalaam
Jumatano Njema.
Paskali
Mada nyingine za mtoa mada kuhusu mambo ya kinteligensia
 
Mtu akikutesa akakuua, maombi hayafanyi kazi pigana mwenyewe. Ingekuwa hizo albadir zinafanya kazi basi Hamas wasingekuwa frontline kupoteza maisha Israel na akina Nyau wangekuwa washaanguka kitambo.
 
Duh

Huu Uzi ni dhahiri kisomo Cha Tanga kimeanza kufanya KAZI

Kama si kuuwawa Ally Mohamed Kibao Elimu hii nyeti yenye ushuhuda wa " dingi" tungeipata Wapi?

Mungu wa mbinguni ana njia zake za kuleta habari

Mungu wa mbinguni mbariki Pascal Mayalla 🌹
 
Mtu akikutesa akakuua, maombi hayafanyi kazi pigana mwenyewe. ingekuwa hizo albadir zinafanya kazi basi Hamas wasingekuwa frontline kupoteza maisha Israel na akina Nyau wangekuwa washaanguka kitambo.
True.

Hata maandiko matakatifu kutoka kwenye vitabu vitakatifu yanasema kwamba "Jilinde nami nitakulinda."
 
Wanabodi,

Najua wengi wetu wameumizwa sana na kifo cha kikatili cha Mzee Ali Mohamed Kibao, natoa tena pole kwa wote.


Jumatano Njema.
Paskali
Nafikiri Bw. Paskali umechanganya mambo, hususani kwenye suala hili la kuua Watu kiholela kunakofanywa na vyombo vya Usalama.

Jaribu kutofautisha kati ya haya mambo mawili:-
1. 'Killing People' and
2."Elimination of Threats.'

Very clear line must be drawn to separate these two things. Unless otherwise, it will cause a total chaos and the serious grave human right violations.
 
Nani kakuambia kwamba watekaji, watesaji na wauaji ni Watu wasiojulikana?
Naomba unitofautishie hizo "wasiojulikana" mbili kwenye heading.

Samahani kaka. Just help me to understand

Jambo la pili
Albadir ni kisomo cha Islam walio safi ingawa wapo wanaoitumia kama ushirikina. Je how do you know karma and not karma ya Albadir? Je wahusika wanahitaji psychological healinĝ yet?
 
Wanabodi,

Najua wengi wetu wameumizwa sana na kifo cha kikatili cha Mzee Ali Mohamed Kibao, natoa tena pole kwa wote.

W

N
Jumatano Njema.
Paskali
Nakuheshimu sana Pasco.
Ngoja nikwambie kitu
Albadir ni dua ambayo unamshatikia Allah. Hii kusomwa unatakiwa utoe taarifa kwamba tunasoma dua hii.
Kama mwizi ajitokeze arudishe, kama Kaiba ndani ya familia ajitokeze ili isisomwe.
Na hii jinsi unavyonuia.
Kama umeniua aliehusika au kutoa amri ya kuibiwa hicho kitu aende na maji basi watakwenda. Ni msururu wa watu wanaeza kwenda na maji. Swala utajuaje kama wameenda na water kutokana halbadiri?
Sasa sijui wasumaji wa dua watanunia vipi
Unamuua au kuamrisha mwenzio auwawe wakati weye mwenyewe utaondoka ktk dunia hii.
 
Mtu akikutesa akakuua, maombi hayafanyi kazi pigana mwenyewe. Ingekuwa hizo albadir zinafanya kazi basi Hamas wasingekuwa frontline kupoteza maisha Israel na akina Nyau wangekuwa washaanguka kitambo.
Na kukumbusha tu ndugu yangu hapa duniani kuna aina mbalimbali za uchawi na tumeambiwa Ktk vitabu vya dini kwamba HAKUNA UCHAWI JUU YA ISRAEL hivyo hakuna ombi, ulozi, uchawi, utaalam wa nyota, au ushirikina wa aina yoyote ya kumuua mu Israel, sasa sijajua huu uwezo ni wa Ki Mungu au kuna mzizi gani hawa jamaa walikula na wana roho ngumu, mbaya, mkatili, kama una bomu au mshale au jiwe unawabamiza vizuri tu lakini uchawi wowote jamaa hawafi wala kuumwa.

Lakini matabaka yaliyobaki hapa duniani yanalogeka.
 
Back
Top Bottom