Kamala hatokwenda kwenye mkutano wake Chuo Kikuu cha Howard

Damaso

JF-Expert Member
Joined
Jul 18, 2018
Posts
3,978
Reaction score
6,739
Tarehe 30 Oktoba 2024 kituo cha habari cha NPR, kiliweka wazi kuwa Harris atatumia usiku wa uchaguzi katika Chuo Kikuu cha Howard, HBCU ambayo ni mahali palipo na mchango mkubwa katika kumtengeneza kuwa kiongozi.


Makamu wa Rais Harris atatumia usiku wa uchaguzi katika chuo kikuu cha Howard, chuo kikuu cha watu Weusi huko Washington ambacho amesema kilikuwa na mchango kubwa kwa utambulisho wake na hamu yake ya kuwa wakili. Harris ndiye makamu wa kwanza wa rais kuwa mhitimu wa HBCU, na angeweka historia kama rais wa kwanza kuhitimu ikiwa atashinda.


Ila masaa mawili yaliyopita imetangazwa kuwa Kamala Harris hatazungumza huku wafuasi wakitokwa na machozi wakiondoka kwenye sherehe za ushindi wakiwa chuoni hapo Howard.


Makamu wa Rais Kamala Harris hatazungumza wakati usiku wa uchaguzi ulipoingia Jumatano asubuhi, kulingana na mwenyekiti mwenza wa Harris Campaign Cedric Richmond ambaye alipanda jukwaani kwenye tafrija ya kutazama Makamu wa Rais Harris katika Chuo Kikuu cha Howard.

Trump shikamoo umemfanya Kamala aone moto aisee! Mambo ni fire kunaki Marekani!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…