Kamanda Mambosasa: Polisi hawakugawana nyama za wafanyabiashara bali ziliteketezwa na nyingine ilifukiwa ardhini, zilikuwa kilo 130 siyo 800!

Kamanda Mambosasa: Polisi hawakugawana nyama za wafanyabiashara bali ziliteketezwa na nyingine ilifukiwa ardhini, zilikuwa kilo 130 siyo 800!

johnthebaptist

JF-Expert Member
Joined
May 27, 2014
Posts
97,869
Reaction score
171,716
Kamanda wa Polisi Kanda maalumu ya Dar es salaam mh Mambosasa amesema tume iliyoundwa kuchunguza sakata la nyama ya wafanyabiashara imegundua nyama yote iliteketezwa.

Mambosasa amesema tume ilionyeshwa shimo kubwa ambamo minofu na mautumbo ilifukiwa na sehemu nyingine ambayo miguu na makongoro iliteketezwa kwa moto.

Hivyo siyo kweli kwamba askari waligawana nyama bali kuna kikundi cha watu wachache kilichodhamiria kulichafua jeshi la polisi amesema kamanda Mambosasa.

Kamanda Mambosasa amesisitiza kuwa bodi ya nyama ilikamata kilo 130 za nyama na wala siyo kilo 800 kama ilivyodaiwa na watu hao wenye nia mbaya na kwamba Jeshi la polisi halitawavumilia wazushi wenye nia mbaya kwa jeshi hilo.

Source: ITV habari

Maendeleo hayana vyama!

 
Mambosasa, waongeze mshahara vijana wako!! Kitendo cha kugawana nyama mbele ya macho ya wananchi ni aibu kubwa kwa mtumishi anayesimamia haki na mashitaka.

Waongeze mshahara. Kuna siku tutuwatega kwa sumu mwenye nyama wanakufa na familia zao kama upupu!!
 
Mambosasa, waongeze mshahara vijana wako!! Kitendo cha kugawana nyama mbele ya macho ya wananchi ni aibu kubwa kwa mtumishi anayesimamia haki na mashitaka.

Waongeze mshahara...kuna siku tutuwatega kwa sumu mwemye nyama wanakufa na familia zao kama upupu!!
Hakika huu ******
 
Tumezowea hawa kulindana. Hata traffuc tuna waona wabavyo lindana kupokea rudhwsma. Ila yana nwidho
 
Huyo Mambosasa nadhani ndio bora wasingemtumia kwenye hiyo mambo yao ya kula "nyama za watu", kwanini nyingine ichomwe na nyingine ifukiwe? au hapakuwa na petroli/mafuta taa ya kutosha?

Huko mlipofukia/kuchoma kwanini hamkwenda na vyombo vya habari wapige picha kama polisi wanavyofanya wakiteketeza mirungi au dawa nyingine za kulevya?

Nionavyo, kadri wanavyotolea maelezo hili suala ndivyo wanavyozidi kuharibu, na bahati yao mwenye nchi hajulikani alipo, angeshakula vichwa vyao.
 
Siku hizi Ubabe Ubabe tu.

Unakamatwa, unanyang'anywa nyama zako wanaenda kugawana, na ukiwapigia kelele wanakukamata wanakufungulia Kesi hata ya Uhujumu Uchumi.

Wao ndiyo wenye Nchi Bana.
 
Ataje waliokuwemo kwenye tume.
Halafu.., kwanini mwenyekiti wa tume hiyo asitoe taarifa hiyo..!? Unampaje mtuhumiwa kutangaza ALICHOCHUNGUZWA yeye..? Au alijichunguza..!?
 
Kama kawaida wale raia wanageuziwa KESI. Watawekwa ndani kwa kosa la kulichafua jeshi la polisi.


Hii ndo TANZANIA mitano Tena.

Mkurugenzi wa bodi ya nyama alidai nyama yote iliteketezwa yakabaki makongoro huyu anadai nyama nyingine ilifukiwa chini.

Mitano Tena au nasema uongo ndugu zangu?.
 
Mzee amekuja na utetezi wa zamani ajui kuwa baada ya kelele watu wananunua utumbo wa bei rahisi huko machinjioni na kutafuta sehemu ya kufukia wakija wapiga kelele wanaonyeshwa hiyo na kufukuliwa tena inanunuliwa ile iliyoharibika kabisa...utashangaa mkichukua huo utumbo waliofukia kimagumashi unazidi kilo walizochukua kwa wananchi...
 
By the way, aliyeongea kwa urefu alikuwa na mnyama yenye thamani ya Tshs 700,000/-, ambayo kwa bei ya huku mtaani kwetu ya 7,000/- kwa kilo, ni sawa na kilo 100... kwa hiyo anataka kutuambia ha walalamikaji wengine walikuwa na kilo 30 tu ili zifike hizo 130 anazozosema..!?

Tuna uwezo wa kutafakari mambo...
 
Polisiccm siku zote ni majizi hilo Watanzania wote tunalijua. Rudisheni nyama kwa mmiliki husika.,
 
Huo ndio uchumi wa kati sasa!

Maendereo hayana chama au nasema uongo ndugu zangu?
 
Walizichomea wapi? Na walizifukia wapi?

Hili jeshi linasikitisha.

Things-now naye ni walewale waliopita mule mule! Inatia kinyaa!

Everyday is Saturday............................... 😎
 
Siku hizi Ubabe Ubabe tu.

Unakamatwa, unanyang'anywa nyama zako wanaenda kugawana, na ukiwapigia kelele wanakukamata wanakufungulia Kesi hata ya Uhujumu Uchumi..

Wao ndiyo wenye Nchi Bana.
Lakini wakumbuke malipo ni hapahapa duniani.
 
Back
Top Bottom