Jibu hoja...polepole ni askari mageleza uu? Kama siyo je alikuwa kaalikwa na nani?Kwahiyo ukikamatwa umeiba utasema mbona na frani kaiba!
Mwenzenu alifuata utaratibu wa mahakama.
LIVE: Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya DSM Lazaro Mambosasa anazungumza kuhusu kilichotokea juzi Segerea wakati Freeman Mbowe akisubiriwa kutoka gerezani
=====
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
WIZARA YA MAMBO YA NDANI
JESHI LA POLISI TANZANIA
TAARIFA KWA UMMA.
KUKAMATWA KWA WAFUASI WA CHADEMA 27 KWA TUHUMA ZA KUFANYA FUJO KATIKA GEREZA LA MAHABUSU SEGEREA.
Mnamo tarehe 13.03.2020 majira ya saa 07:00 mchana Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam lilipokea taarifa kutoka kwa maofisa wa Gereza la Mahabusu Segerea kuwa kuna kundi la wafuasi wa chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) likiongozwa na wabumbe wawili ambao ni Halima James Mdee, Ester Amos Bulaya na Meya wa Ubungo Boniface Jacob limekusanyika katika geti la kuingilia gerezani hapo huku likiandamana na kufanya fujo kutaka kuingia kwa nguvu ndani ya gereza kwa lengo la kwenda kumtoa mwenyekiti wa chama chao Mhe.Freeman Mbowe.
Jeshi la Polisi Kanda Maalum baada ya kupokea taarifa hizo lilituma askari wa kikosi cha kutuliza ghasia (FFU) na askari wa kituo cha Polisi Stakishari na ambapo walipofika eneo hilo waliwakuta askari magereza wakiwa wanaendelea kuwadhibiti wanachama hao na ndipo Polisi walipowakamata watuhumiwa 27.
Baada ya watuhumiwa hao kukamatwa askari wa Jeshi la Polisi kwa kushirikiana na askari wa Jeshi la magereza waliwachukua na kuwapeleka kituo cha Polisi Stakishari kwa mahojiano na baada ya mahojiano watuhumiwa wote 27 walidhaminiwa kwa mujibu wa sheria na watafikishwa mahakamani hivi karibuni kwani upelelezi wa shauri hili umeishakamilika.
Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam linatoa onyo kali kwa kikundi chochote cha siasa,dini,au mtu yeyote kuacha kabisa kuchezea maeneo nyeti kama magereza,makambi ya Majeshi yote au maeneo yoyote ambayo ni nyeti kwa taifa.
Hivyo atakayejaribu kufanya hivyo atachukuliwa hatua kali za kisheria.
WATU 03 WAPOTEZA MAISHA KWA AJARI YA BARABARANI.
Mnamo tarehe 15.03.2020 majira ya 04:30 alfajiri huko barabara ya kawawa mataa ya veta gari namba T 530 DNW aina ya EICHER daladala linalofanya safari za Mbangara- Makumbusho likitokea Mbagala kuelekea Makumbusho liligongana na gari la kubebea nyama lenye namba T 744 DET lililokuwa likitokea Tazara kuelekea katikati ya Jiji na kusababisha vifo vya watu watatu ambao ni wanaume wawili na mwanamke moja na kusababisha majeruhi ya watu nane.
Chanzo cha ajari ni daladala kutaka kuwahi kupita kwenye taa nyekundu.
LAZARO MAMBOSAS– SACP
KAMANDA WA POLISI KANDA MAALUM
DAR ES SALAM.
15/03/2020
Tangu alipo sema risasi ilipigwa juu na kisha ikapinda mpaka Leo huyo simuaminiMarch 15, 2020
Dar es Salaam, Tanzania
Leo Machi 15, 2020 Kamanda wa kanda maalumu ya Dar es salaam, SACP Lazaro B. Mambosasa amezungumza na waandishi wa habari katika ukumbi wa mikutano wa jeshi la polisi kanda maalumu ya Dar es salaam na kutoa taarifa ya kukamatwa kwa wanachama wa CHADEMA kwa kosa la kuleta fujo katika gereza la Segerea.
Jitekenye. Msipotii sheria za nchi mtapigwa sana na hakuna lolotr mtakalofanya.Washenzi wakubwa,yaani chuki mnayojijengea ipo siku mtashangaa!
Hivi askari wakipata ajali na kufa kama 10 hivi,hilo shangwe mitandaoni naliona kama lote!
Tangu alipo sema risasi ilipigwa juu na kisha ikapinda mpaka Leo huyo simuamini
Sent using Jamii Forums mobile app
Walijipeleka wenyewe!Huyu siwezi kumuamini hata kidogo.
Kwenye hiyo kesi,wanaolengwa hapo ni Mdee na Bulaya, ila haya mambo mwisho wake ni kuwafanya viongozi wa upinzani na wafuasi wao kwa ujumla kuzoe Jela na hali hii ikitimia,basi tujiandae kwa maandamano na ghasia za kisiasa haya yakiwa ni matokeo ya watu kutoogopa jela na zaidi kuwa desperate hivyo kujiona hawana cha kupoteza kukaa/kwenda jela.
Duh, Mkuu ni heri ungejikita kukanusha kuchana hiyo sare..Kwa hiyo ukichana sare, unavunjwa mkono. Sawa sawa.
Siku zote unatakiwa kusimamia ukweli, so ukikubali kuendeshwa kwa ajili ya kulinda tumbo lako ni kitu kibaya sana kwa afya ya akili yako! [emoji41][emoji41]Tunamuonea huyuu mambosasa anapelekeshwa na wakubwa wake roho inamuuma ila afanyaje Sasa.
Another homo habilis pretending to be homosapiensUko sawa kamanda mambo sasa! Namimi nakukubari sana kamanda wangu!
Umejibu maswari yote kwa ufadaha.
Kwa ukweli
Bila chembe ya uongo.
Naamini hata mahakamani kulingana nawalichokifanya wanaenda kula mvua za ukweli ili wakirudi wakute chama kimekufa kabisa. Halima na Bulaya wanajifanya wao nividume wameenderea kufanya vitendo visivyo jadi ya watanzania sasa naona wamefika sehem wanajiona ni mwamba.
Songesha mahakamani kwa mashtaka ambayo hawaweza kuyakanusha najua hata wao watakuwa wameyaandika.
1.kwenda kumtoa mfungwa gerezani bila ridhaa ya magereza
2.kufanya funjo ndani ya eneo la magereza kwa nia ovu yakutaka wafungwa watoke.
3.kuzuia jeshi la magereza kufanya kazi zao.
Nadhani walisahau kuwa mkuu wa magereza nchini saivi ni mjeshi.
Naina miaka2 jera au faini kwa kila mmoja.