Kamaradi Gabriel Zacharia

Amavubi

JF-Expert Member
Joined
Dec 9, 2010
Posts
30,156
Reaction score
13,258
Nimekuwa nafuatilia sana vipindi mbalimbali hasa vya mahojiano katika TBC ONE/TAIFA, kwa mijadala mbalimbali ya siha, kwa kufanya hivi nimebahatika pia kufanya uchambuzi wa watangazaji mbalimbali na wengi kuvutiwa nao na wengine kuona kuna maeneo wanayohitaji maboresho kidogo. Wenzetu huwa wanaangalia sana hasa vipindi vya mahojiano kumpeleka mtu mwenye taaluma husika kufanya mahojiano na mlengwa wake

Hata hivyo bado sijavutiwa sana na kamaradi Gabriel Zacharia, ninaona muda mwingi akiwa kama muoga hivi anapowahoji walengwa mbalimbali na hujikita sana kwenye maswali aliyoandaa, aidha mara nyingi simuoni akiwa na umakini kwenye swali alilouliza yaani akishauliza anasubiri mjibu swali amalize ili amuulize swali linalofuata bila kufanya analysis ya majibu (kuuliza alimradi maswali yaishe) sidhani kama ni nidhamu ya woga iliyojengeka kwa TBC sasa au la....

Nadhani Kamaradi Gabriel bado anayo nafasi ya kuonyesha zaidi ya taaluma akiwa kwenye anga zake (kipaji)........moja ya sifa kuu zinazowabeba watangazaji wengi kama Larry King etc ni kuonesha vipaji vyao halisi wanapopewa rungu (smartness upstairs)
Nakutakia kila la heri unapotafakari haya....
 
thats true mkuuu,
sometym anakua na kitete sana .. .... na anaonesha kama ana dalili za kutokwa na machozi hivi kwa woga! huwa nashindwa kumsoma fresh then nachenj channel!
 
kwa mazingira na kiwango cha utangazaji wa ndani ya nchi yetu, mimi naona gabriel zakaria ana kiwango cha kuridhisha na hasa ikizingatiwa kuwa hapa kwetu hatujafikia kiwango cha kuwa na specialists bali tunao generalists katika utangazaji.Huyu Gabriel Zakaria ni generalist wa kiwango cha juu kwani anajitahidi kufanya home work ya issues ambazo atawahoji wazungumzaji tofauti na watangazaji au waandishi wengi wa habari hapa Tanzania.
 
namuona anakuwaga na hasira pale mitambo ya tbc inapokataa kuleta habari na kumbakisha yeye kwenye screen kwa muda asijue afanyeje
 
kuna siku alikuwa anamhoji lissu kuna tym ilimbidi amkatishe maana alihisi kibarua kingeota nyasi jinsi lissu alivyomwaga sumu kuhusu mkapa.
 
Ninachokiona mimi ni always kuwa not impartial anapohoji watu contrary na taluma yake. Hasa ukiwa anakuhoji kitu kinachonekana ni dhidi ya gvt. Ye ni mfano wa golori juu ya meza ikiwa tenge, upande wa chini kunako rangi mbili afu mgeni akaa upande wa juu. Lazima itiririkie kuleeee!!
 
hajiamini kabisa..hajui kutangaza...anakosea kosea sana...ukiangalia newscasters wakali dunian kama Amanpour CNN,Christie lu stout CNN na Fauziah Ibrahin AJE...hutatamani kumsikiliza huyu Gabriel...
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…