Kamari imekua zaidi ya cocaine!

Iko strateg ya kula hela ila ukubali ku stick na option moja huku ukidouble stake..odds iwe angalau 3...
 
.
90% ya sumu ya panya ni chakula... Sidhani kama umenielewa. Namaanisha 10% inayobaki ndio sumu ya kumuua panya. Kwanini wanaweka kiasi kidogo sana cha sumu na kiasi kingi cha chakula? Simple, kumvutia panya ale.
.
Ina uhusiano gani na kamari? Siku hizi wachezesha kamari wameshtuka, wakibutua hela za wateja wao bila kuwapa ushindi wa hapa na pale, watu wanakata tamaa wanaacha kucheza kabisa.
.
So wamekuja na mbinu mpya ya kurudisha kiasi kikubwa cha hela kwa wachezaji. Siku hizi ukiwa mcheza kamari kwa muda fulani, uwezekano wa kupiga hela ni mkubwa na ndio maana wacheza kamari wanaongezeka kila kukicha.
.
In the lon run kuna mambo 2 yanatokea;

1. Wanakupiga hela kidogo kidogo, unakula unaliwa unakula unaliwa ila overall unaliwa pakubwa lakini mpaka uje kushtuka sio leo.

2. Wanakufanya kuwa na uraibu wa kamari kitu ambacho ndio lengo kuu. Ukishafikia stage hii, huchomoki. Hapo wao ni kuvuna tu hela zako mpaka utakapofilisika.
 
Yaani machalii yamesoma yana nguvu nikukaa kuanzia asubuhi mpaka jioni kubahatisha yaani mpaka wazee!!
Mi kwa Sasa Niko hapa soko la kilombero wamama wanauza nyanya wakipata mia mbili mbili wanadumbukiza kwenye zile mashine za kichina![emoji2827]


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Achana na Hilo mashine mkuu

Huku mtaani tunaliita Dubwi sio poa yaani vijana wa Boda hawapeleki hesabu wamama nao linawapelekesha hadi kodi ya meza Dubwi anakwala sio poa
Kuna jamaa waliliwaaaaa ikafika sehemu wakasema haiwezekani hili dude linatoboka kwanini tusitoboe tuchukue Pesa zetu ilivyofika asubuhi dude linakutwa limetobolewa na Pesa zote zimechukuliwa

Sema sasa hivi wote marehemu wamekufa kwa kupigwa risasi
 
Haya mambo ni kuwa na kiasi tu, binafsi ni muumini wa kubashiri, nime-base sana kwenye mpira wa miguu, kiukweli nampiga sana mhindi, nyumbani hawajui kama nabeti na pia huwa wanashangaa huwa natoa wapi pesa, kwa week huwa nabet mara moja tu na hiyo ni mara baada ya kufanyia utafiti timu ntakazozibetia kisha natia mzigo, kiufupi ukienda kwa mahesabu na kiasi huwezi ona athari .
 
imagine unakopa uanzishe mladi wa ufugaji wa kuku wa kisasa au kilimo cha nyanya na matikiti na unawasakama wanaobeti[emoji28][emoji28][emoji28].

moja ya mpango amabo shetani kafanikiwa kuhusu sisi binaadam,ni kututawanya kwa uwezo wa kufikiria.

huna tofauti na benki za kiislam zinazosema hazitozi riba kama benki nyingine,ila zinakuuzia bidhaa sio pesa,akili mtu wangu.
 
Achana na Hilo mashine mkuu

Huku mtaani tunaliita Dubwi sio poa yaani vijana wa Boda hawapeleki hesabu wamama nao linawapelekesha hadi kodi ya meza Dubwi anakwala sio poa
Kuna sehemu yeye anawakopesha pesa za kucheza hilo dude kwa return ya 1000 kwa kila 10000
Anasema kwa siku anapata faida ya 20000 kwa kukopesha tu
 
Ukifikiri kwa makini maisha yote ni kamari tu nashangaa wanaodai kamari ni haramu.
Watu hawaelewi hilo kwamba kununua mzigo na kuusubiri ufike, ukauuze kwa bei fulani ni kamari.

Kusomesha mtoto ukitegemea awe hivi anakuwa vile
 
waache watu watumie pesa zao wew unaumia nin?
 
Ila usiifananishe na Cocaine

Cocaine inakufanya uwe High

Betting ifananishe na Heroine
 
Kamari kama cocaine, ni uraibu!
 
Watu hawaelewi hilo kwamba kununua mzigo na kuusubiri ufike, ukauuze kwa bei fulani ni kamari.

Kusomesha mtoto ukitegemea awe hivi anakuwa vile
Kabisa mkuu ata imani imekaa kikamari tu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…