Jay456watt
JF-Expert Member
- Aug 23, 2016
- 10,356
- 7,992
umemjibu vyema kabisa...jamaa kanishangaza sana...kwani hakuna waknya wanaoweza kuandika Kiswahili sanifu? sasa ushakuwa mtanzania sababu ya mwandiko wako? jamaa hana akili kabisaUnapindisha mandhari ya mada, Kiswahili ni lugha ya taifa Kenya na pia ni lugha ya asili ya baadhi ya jamii zetu za Pwani, walihusika kwenye kukibuni.
Turudi kwenye mada....
hawa watakuwa small fish and middle-sized fishes....tunataka sasa the big fish baada ya hawa kukamatwa...tumechoshwa sana...finance minister, CBK governor na bank managers wana maswali yakujibu pia...
Maze corruption Africa ni cancer. Mr Magufuli recently has received his Party assets audit report, my friend I hope no action will be taken coz am sure if he acts the party will shakePaspoti zitwaliwe, kila aliyetajwa kwa namna moja au nyingine anafaa kubaki ndani nyumbani mwake akisubiri makachero kubisha hodi wakati wowote, nchi yote ijawe taharuki, tumbo joto kwa kila mmoja, we want blood...
Unazeeka vibaya, hao mawaziri walifungwa miaka minane jela na wametukia kifungo chao zaidi ya nusu. Kutokana na uzee na afya zao wakabadilishiwa kuwa kifungi cha kijamii. Hebu tuonyeshe kiongozi gani mwenyewe hadhi ya baraza la mawaziri amehukumiwa kwa ufisadi nchini Kenya. Hili swala Kenya hamliwezi mtake msitake, kuanzia Jomo Kenyatta, Moi, Uhuru Kenyatta, Ruto hata huyo Matiagi wote ni mafisadi. Wote wamejilimbikizia mali ambayo ukiwauliza vizuri hawawezi kujibu wameipata vipi. Mnapenda kuona sinema eti fulani kakamatwa, kuna watu waiokuwa na nafasi kubwa makatibu wakuu nk wateseka hivi sasa kujibu maswali magumu na akauti zao zimewekwa stop.Hilo la kesi kuendelea mahakamani ni jambo la kawaida hata huku tuna zaidi ya kesi 400 mahakamani kwa ajili ya watuhumiwa wa ufisadi, mimi nilitaka unionyeshe kipi mumefaulu cha zaidi, kama vile kutaifisha mali, unaishia kuniambia watu walipewa kifungo cha kufanya kazi za jamii, community service, like seriously mtu ameiba mabilioni unampa adhabu ya kufagia, a slap on the wrist, halafu unakuja kujisifia hapa eti mnapigana na mafisadi.
Hii awamu mlianza kwa mbwembwe nyingi sana, nimejaribu kutafuta nini mlifanikisha tofauti na ilivyokua hapo awali sijakiona, zaidi ya PR za kuzunguka na wana habari mkishtukiza. Juzi hapa tuliona ukuaji wa uchumi wenu umeshuka zaidi ya hatamu na awamu zote, ukaishia kubwabwaja eti ni kwa sababu mumewaondoa wawekezaji hewa.
Unazeeka vibaya, hao mawaziri walifungwa miaka minane jela na wametukia kifungo chao zaidi ya nusu. Kutokana na uzee na afya zao wakabadilishiwa kuwa kifungi cha kijamii. Hebu tuonyeshe kiongozi gani mwenyewe hadhi ya baraza la mawaziri amehukumiwa kwa ufisadi nchini Kenya. Hili swala Kenya hamliwezi mtake msitake, kuanzia Jomo Kenyatta, Moi, Uhuru Kenyatta, Ruto hata huyo Matiagi wote ni mafisadi. Wote wamejilimbikizia mali ambayo ukiwauliza vizuri hawawezi kujibu wameipata vipi. Mnapenda kuona sinema eti fulani kakamatwa, kuna watu waiokuwa na nafasi kubwa makatibu wakuu nk wateseka hivi sasa kujibu maswali magumu na akauti zao zimewekwa stop.
Kifungo ni kifungo, kupotelewa kwa heshima ya mtu tena ukiwa ni mtu mkubwa na mwenyewe madaraka ina umiza kuliko kifungo cha kukaa jela. Unafikiri watu kama Bill Cosby na Harvey Weinstein wanaumizwa kiu gani, kupotea pesa au kupoteza heshima yao mbele ya jamii?Nimetafuta kwenye Googla na kukuta hao walifungwa kipindi cha Kikwete, kifungo chaa miaka mitatu na wakaachiwa kwenye utawala wa hii awamu ili wakafagie. Lakini mali zao hazikutaifishwa, hivyo bado issue iko pale pale, a slap on the wrist baada ya kukwapua mabilioni.