Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Umetoa pondekezo zuri mkuu. Hata mimi nadhani Lissu na Chadema waitumie ''adhabu'' hii ya kishetani kuwafanya NEC-CCM wajute kumfungia. Zitafutwe mbinu za kumfanya ku-engage na wananchi na kijitangaza kulika hata angepiga kampeni.Dalili zote zinaonyesha movement ya Lissu ni zaidi ya Kimbunga kumbakumba, huwezi kukizuia kwa mwavuli
Polisi ipo kulinda sheria, sisi Watanzania tutabaki nyumbani kutii sheria hatuwezi kwenda kumskililiza muhubiri chuki
Lb7 Kwamba Lissu yu hai nyongo zenu milini ni kutenda sumu tu.
Mna wakati mgumu kuliko maelezo.
Wakati gani Mkuu kwa hivi vimkwara vya lissu jukwaani [emoji3][emoji3]
Mbowe hapangiwi, atafanya atakavyo. Wewe na maoni yako, anzisha chama chako..
Mkuu umewaza vema, hapo wanapima upepo'1. Ipinge na ilaani kwa nguvu zote katazo hilo na ilitangaze kuwa ni batili.'
Hii ni kupoteza muda tu maana CCM inajua zaidi ya hilo tamko hamna kitu kitafanyika.
Na hapa CCM wanapima reaction ya Chadema na wananchi,hii ikipita hivi hivi then implication ya hio ni kwamba Kwny matokeo ya uchaguzi watachakachua kama kawa wakijua wataishia tu kutoa tamko.
Lissu aendelee na ratiba zake za kampeni kama kawaida ili kuwaonyesha hata kwny matokeo ya uchaguzi mkizingua haitapita hivi hivi.
Inshort ni kwamba akikubali kutopiga kampeni then he's done.
Leo kamati kuu ya Chadema inakaa, naamini itajadili mambo mengi ikiwemo mwenendo mzima wa kampeni kuanzia uraisi hadi madiwani nchi nzima bila kusahau suala zito la kusimamishwa kufanya kampeni kwa ndugu Tundu Lissu.
Kwa minajili hiyo mimi kama mwananchi naomba kamati kuu iazimie yafuatayo
1. Ipinge na ilaani kwa nguvu zote katazo hilo na ilitangaze kuwa ni batili
Ukangalia hilo katazo dhidi ya mh Lissu, mchakato wake mzima tangu Mahera anatangazia umma kuwa wamemwandikia Lissu barua ya wito na kuifikisha kwa mhusika wakati ni uongo, mpaka siku Nyahoza anapeleka barua ya wito kwa bodaboda siku moja mbele baada ya tangazo a Mahera, Ukiangalia namna ambavyo mtuhumiwa hakuambiwa kwa maandishi Kosa lake halisi alilolifanya ili aandae utetezi juu ya kosa hilo kwa maandishi ndani ya masaa 48 kama kanuni zinavyosema, na ukiangalia kuwa Mtuhumiwa hakupewa nafasi ya kujitetea kwa kosa ambalo kimsingi halikutajwa ni nini haswa na wala hakukabidhiwa wito yeye mwenyewe. Kwa hiyo ni dhahiri maamuzi ya Kamati ya maadili ni batili na kamati kuu iutangazie umma kuwa maamuzi hayo ni batili, ya kiuonevu na iutangazie umma kuwa katazo hilo ni kinyume cha sheria na ni uonevu wa dhahiri dhidi ya mgombea wake wa uraisi
2. Kamati kuu impongeze heshimiwa Lissu na iwashukuru wananchi.
Kiukweli kabisa, Lissu kapiga kazi nzito, kuanzia wakati wa kutafuta wadhamini, mpaka wakati wa kampeni, Kanadi ilani ya chama kwa weledi mkubwa sana, kasaidia kuhuisha uhai wa chama na anaelekea kukipatia chama ushindi mnono. Chama kitoe azimio kumpongeza ndugu Lissu na kuwashukuru Watanzania kwa mwitikio mzuri na kuonyesha kukubali sera za Chadema
3. Kamati kuu impe mapumziko ndugu Lissu au Impangie majukumu mengine ya kichama ndani ya siku hizi saba
Kamati kuu kwa kutambua kazi nzito aliyofanya mheshimiwa Lissu inaweza kuamua kumpa Likizo ya mapumziko ya siku saba au ikaamua kumpa likizo ya siku tatu na ikampangia majukumu ya kujenga chama kwa siku nne. Kwenye kujenga Chama mheshimiwa Lissu atembelee ofisi za Chama na matawi yake, abadirishane mawazo na watendaji wa ofisi hizo na matawi hayo.
Lakini chama kikipenda kinaweza kumpangia mh Lissu kazi ya kunadi wagombea udiwani na Ubunge bila kujinadi yeye mwenyewe. Kufanya hivi siyo kosa kwa sababu kwanza mheshimiwa Lissu bado ni mtanzania ana haki ya kwenda popote nchini kwa mujibu wa katiba, na pili ni kiongozi halali wa Chama ana wajibu wa kuimarisha chama chake hata kama hajipigii kampeni. Nne ana haki zote za uhuru wa maoni na uhuru wa kujumuika (Freedom of association) katika kusanyiko lolote.
4. Kamati kuu imuagize Mwenyekiti ndugu Mbowe kuzunguuka sehemu mbalimbali za nchi na kuwapigia kampeni Madiwani na wabunge
Iwapo chama kitaamua Makamu Mwenyekiti (Yaani Tundu Lissu) awe kwenye mapumziko, ni wakati muafaka sasa Mwenyekiti afanye kama anavyofanya Kassim Majaliwa, yaani azunguuke sehemu mbalimbali za nchi kunadi wabunge wake na madiwani wake. Na atumie hadhara hizo kuwaeleza wananchi kwa nini Lissu hayuko kwenye kampeni, awaeleze kuwa ni sababu za uonevu tu na kutofuata sheria kwa tume.
LISSU MWENYEWE AFANYEJE
1. Kama akiamua kukaa Likizo ya siku kadhaa, basi ni muda muafaka wa kwenda kufanya Shopping kwenye masoko makubwa
Kwa mujibu wa Katiba Lissu ana haki ya kwenda popote nchini, ana haki ya kwenda masokoni kununua bidhaa, ana haki ya kwenda sokoni kariakoo kununua matunda, kwenda Soko la Tandale, Kisutu, Mwananyamala na kwenye shopping malls zote kubwa. Ana haki ya kwenda kwa shoe shines kung'arisha viatu vyake, ana haki ya kuchukua aina ya magari ya watalii na kuzunguuka mijini etc
2. Tembelea majirani zako hapo Tegeta na hani misiba
Pita kwa majirani zako, waulize habari zao katika miaka mitatu iliyopita wakati ulipokuwa haupo nchini, hani misiba yao, washukuru kwa sala zao na maombi yao.
Mtume Muhammad alifundisha kuwa Malaika Gabriel alimsisitiza sana sana kuwa vizuri mno na majirani mpaka mtume akaanza kuhisi kuwa labda hiyo ni amri mpya ya lazima kutoka kwa Mungu
3. Baada ya kukuzuia kufanya Kampeni, basi huu ndo muda wa kuendelea kuwashukuru wananchi kwa kukuchangia pale ulipopigwa risasi na pia kutoa elimu ya uraia
Watu walikuandama kuwa unaongelea sana kupigwa kwako risasi badala ya sera, Ulipoanza kumwaga sera rasmi wakapagawa mpaka sasa wamekuletea figisu. Sasa mheshimiwa Lissu hizi siku saba kwa kuwa wamekuzuia kumwaga sera, Huu ni muda wa kuzungumzia wewe kupigwa risasi, kulitaka jeshi la polisi lichunguze tukio, kuwashukuru wananchi kwa kukuchangia. Ukifanya hivi siyo kosa, ni haki yako ya kikatiba kuzungumza. Ukifanya hivi utakuwa hufanyi kampeni na hivyo siyo kosa kwa mujibu wa NEC. Pia unaweza kuendelea kutoa elimu ya uraia kwa wananchi, unaweza kuamua kufanya indoor au nje kwenye mikutano ya chama n. k
Missile of the Nation
Muhubiri chuki ni yule aliyesema Tunduma wasipomchagua Silinde hawezi kuwapelekea MajiPolisi ipo kulinda sheria, sisi Watanzania tutabaki nyumbani kutii sheria hatuwezi kwenda kumskililiza muhubiri chuki
Badala ya kuhimiza atulie na kuomba msamaha wewe unahimiza aendelee kufanya ujuaji na kiburi....wahenga walishasema mkaidi hafaidi mpaka siku ya iddi
Safi sana uko vizuriLeo kamati kuu ya Chadema inakaa, naamini itajadili mambo mengi ikiwemo mwenendo mzima wa kampeni kuanzia uraisi hadi madiwani nchi nzima bila kusahau suala zito la kusimamishwa kufanya kampeni kwa ndugu Tundu Lissu.
Kwa minajili hiyo mimi kama mwananchi naomba kamati kuu iazimie yafuatayo
1. Ipinge na ilaani kwa nguvu zote katazo hilo na ilitangaze kuwa ni batili
Ukangalia hilo katazo dhidi ya mh Lissu, mchakato wake mzima tangu Mahera anatangazia umma kuwa wamemwandikia Lissu barua ya wito na kuifikisha kwa mhusika wakati ni uongo, mpaka siku Nyahoza anapeleka barua ya wito kwa bodaboda siku moja mbele baada ya tangazo a Mahera, Ukiangalia namna ambavyo mtuhumiwa hakuambiwa kwa maandishi Kosa lake halisi alilolifanya ili aandae utetezi juu ya kosa hilo kwa maandishi ndani ya masaa 48 kama kanuni zinavyosema, na ukiangalia kuwa Mtuhumiwa hakupewa nafasi ya kujitetea kwa kosa ambalo kimsingi halikutajwa ni nini haswa na wala hakukabidhiwa wito yeye mwenyewe. Kwa hiyo ni dhahiri maamuzi ya Kamati ya maadili ni batili na kamati kuu iutangazie umma kuwa maamuzi hayo ni batili, ya kiuonevu na iutangazie umma kuwa katazo hilo ni kinyume cha sheria na ni uonevu wa dhahiri dhidi ya mgombea wake wa uraisi
2. Kamati kuu impongeze heshimiwa Lissu na iwashukuru wananchi.
Kiukweli kabisa, Lissu kapiga kazi nzito, kuanzia wakati wa kutafuta wadhamini, mpaka wakati wa kampeni, Kanadi ilani ya chama kwa weledi mkubwa sana, kasaidia kuhuisha uhai wa chama na anaelekea kukipatia chama ushindi mnono. Chama kitoe azimio kumpongeza ndugu Lissu na kuwashukuru Watanzania kwa mwitikio mzuri na kuonyesha kukubali sera za Chadema
3. Kamati kuu impe mapumziko ndugu Lissu au Impangie majukumu mengine ya kichama ndani ya siku hizi saba
Kamati kuu kwa kutambua kazi nzito aliyofanya mheshimiwa Lissu inaweza kuamua kumpa Likizo ya mapumziko ya siku saba au ikaamua kumpa likizo ya siku tatu na ikampangia majukumu ya kujenga chama kwa siku nne. Kwenye kujenga Chama mheshimiwa Lissu atembelee ofisi za Chama na matawi yake, abadirishane mawazo na watendaji wa ofisi hizo na matawi hayo.
Lakini chama kikipenda kinaweza kumpangia mh Lissu kazi ya kunadi wagombea udiwani na Ubunge bila kujinadi yeye mwenyewe. Kufanya hivi siyo kosa kwa sababu kwanza mheshimiwa Lissu bado ni mtanzania ana haki ya kwenda popote nchini kwa mujibu wa katiba, na pili ni kiongozi halali wa Chama ana wajibu wa kuimarisha chama chake hata kama hajipigii kampeni. Nne ana haki zote za uhuru wa maoni na uhuru wa kujumuika (Freedom of association) katika kusanyiko lolote.
4. Kamati kuu imuagize Mwenyekiti ndugu Mbowe kuzunguuka sehemu mbalimbali za nchi na kuwapigia kampeni Madiwani na wabunge
Iwapo chama kitaamua Makamu Mwenyekiti (Yaani Tundu Lissu) awe kwenye mapumziko, ni wakati muafaka sasa Mwenyekiti afanye kama anavyofanya Kassim Majaliwa, yaani azunguuke sehemu mbalimbali za nchi kunadi wabunge wake na madiwani wake. Na atumie hadhara hizo kuwaeleza wananchi kwa nini Lissu hayuko kwenye kampeni, awaeleze kuwa ni sababu za uonevu tu na kutofuata sheria kwa tume.
LISSU MWENYEWE AFANYEJE
1. Kama akiamua kukaa Likizo ya siku kadhaa, basi ni muda muafaka wa kwenda kufanya Shopping kwenye masoko makubwa
Kwa mujibu wa Katiba Lissu ana haki ya kwenda popote nchini, ana haki ya kwenda masokoni kununua bidhaa, ana haki ya kwenda sokoni kariakoo kununua matunda, kwenda Soko la Tandale, Kisutu, Mwananyamala na kwenye shopping malls zote kubwa. Ana haki ya kwenda kwa shoe shines kung'arisha viatu vyake, ana haki ya kuchukua aina ya magari ya watalii na kuzunguuka mijini etc
2. Tembelea majirani zako hapo Tegeta na hani misiba
Pita kwa majirani zako, waulize habari zao katika miaka mitatu iliyopita wakati ulipokuwa haupo nchini, hani misiba yao, washukuru kwa sala zao na maombi yao.
Mtume Muhammad alifundisha kuwa Malaika Gabriel alimsisitiza sana sana kuwa vizuri mno na majirani mpaka mtume akaanza kuhisi kuwa labda hiyo ni amri mpya ya lazima kutoka kwa Mungu
3. Baada ya kukuzuia kufanya Kampeni, basi huu ndo muda wa kuendelea kuwashukuru wananchi kwa kukuchangia pale ulipopigwa risasi na pia kutoa elimu ya uraia
Watu walikuandama kuwa unaongelea sana kupigwa kwako risasi badala ya sera, Ulipoanza kumwaga sera rasmi wakapagawa mpaka sasa wamekuletea figisu. Sasa mheshimiwa Lissu hizi siku saba kwa kuwa wamekuzuia kumwaga sera, Huu ni muda wa kuzungumzia wewe kupigwa risasi, kulitaka jeshi la polisi lichunguze tukio, kuwashukuru wananchi kwa kukuchangia. Ukifanya hivi siyo kosa, ni haki yako ya kikatiba kuzungumza. Ukifanya hivi utakuwa hufanyi kampeni na hivyo siyo kosa kwa mujibu wa NEC. Pia unaweza kuendelea kutoa elimu ya uraia kwa wananchi, unaweza kuamua kufanya indoor au nje kwenye mikutano ya chama n. k
Missile of the Nation
Umeona mbali na mawazo yako yanafungamana na yangu. Aendelee kuchanja mbuga tu.'1. Ipinge na ilaani kwa nguvu zote katazo hilo na ilitangaze kuwa ni batili.'
Hii ni kupoteza muda tu maana CCM inajua zaidi ya hilo tamko hamna kitu kitafanyika.
Na hapa CCM wanapima reaction ya Chadema na wananchi,hii ikipita hivi hivi then implication ya hio ni kwamba Kwny matokeo ya uchaguzi watachakachua kama kawa wakijua wataishia tu kutoa tamko.
Lissu aendelee na ratiba zake za kampeni kama kawaida ili kuwaonyesha hata kwny matokeo ya uchaguzi mkizingua haitapita hivi hivi.
Inshort ni kwamba akikubali kutopiga kampeni then he's done.
Akili ya bangiOngezea aanze kuaga mapema kwani tarehe kama ya leo atakuwa Ubelgiji
Kama vile ulikuwa kwenye akili yangu, kampeni sawa Ila Kuna mambo nje ya kampeni Ni muhimu zaidi,Nashauri TL na kamati yake watumie muda huu wa kusimamishwa kwa kampeni zao kuandaa mikakati ya kupata mawakala wasomi, wenye nguvu, waaminifu,na wahakikishe kila kituo kinakuwa na mawakala zaidi ya mmoja kwa kutumia uwakilishi wa vyama rafiki hasa ACT wazalendo.
Kumbuka kivumbi, patashika nguo kuchanika, figisu, vitimbwi, mazingaombwe, vituko na kila aina ya mihemko, kura kupotea, mabox kunyakuliwa, mawakala kushambuliwa na kunyimwa nakala za matokeo, kunyimwa fomu za malalamiko, kukataa kusaini matokeo, kubadili matokeo kwa maana ya kura za A kumpa B na za B kumpa A, yote hayo muda wake ni kuanzia saa1 jioni ya tarehe 28/10/2020.
Uzoefu wangu unanionyesha kuwa hicho ndio kitakachokuwa kipindi kigumu na cha kutisha sana huenda kuliko nyakati nyingine zote katika historia ya uchaguzi wa nchi hii.
Ndio kipindi pekee cha kuhakikisha chungwa linabaki kuwa chungwa, au kwa nguvu ya ajabu, chungwa litabadilishwa kuwa limau.
Ndio kipindi cha kuamua hatima ya amani ya nchi hii.
Polisi ipo kulinda sheria, sisi Watanzania tutabaki nyumbani kutii sheria hatuwezi kwenda kumskililiza muhubiri chuki