Kamati ya Bunge itakayomuhoji Gwajima ijiandae kukutana na majibu yatakayowaacha wakiangaliana

Vipi, ikitokea Rais mjinga Kama kibwetere!??
Akatufungia ndani Ili atuchomee moto ndani?!
Tuendelee kutii tu!!! Hizo directions za kiongozi wetu.

Mh!?
Ukijibiwa kuwa wewe ni mpumbavu usije chukia,miezi michache tu imepita ulikua umebanwa na Rais kibwetere na hukuongea chochote,sasa kidogo freedom of press ipo nchini na wewe unajifanya shujaa!tuendeleee kulalama humu .
 
Mbona ku sign hospital huwa ni kawaida ka unafanyiwa operation so acheni ushamba wakusema ku sign hyo consent form ya chanjo kuwa dawa ina madhara
 
Hii ni drama tu.
Wote ni wapigaji.

Watasutana na kuishia 'onyo'
Serikali yenyewe imekosa msimamo kwa kusema eti chanjo ni hiari wakati kitaalamu sio hiari. Kwasababu usipochanja ukiupata ugonjwa huenda utaambukiza wengine ambao wanaweza kufa; pamoja na wewe mwenyewe!
Ni sawa na kusema "tii sheria bila shuruti" wakati wewe mwenyewe huheshimu katiba na sheria!


Sent from my G80 using JamiiForums mobile app
 
RAISI was Tanzania hashitakiki popote
 
RAISI was Tanzania hashitakiki popote
Ndio maana wewe middle class unaendelea kulalama humu na no actions unaweza chukua kisa woga wako na njaa ya tumbo,KATIBA mpya ni muhimu ambayo ita keep on check madaraka ya no 1,....next time take your time kujibu hoja maana ulichokiandika hapo hakisomeki vema ,spelling errors nyingi mno
 
Na kisheria sijui kosa lake ni lipi.

Anashutumiwa kuhimiza watu kutochanjwa na kusema ana taarifa za kisayansi kuwa chanjo si salama. Serikali ina taarifa kuwa chanjo ni salama na inahimiza watu wakachanjwe kwa uamuzi wao binafsi.

Wakati serikali ikitaka watu watumie hiari yao kuamua kama wanachanjwa au la - Gwajima anaonekana kuwa na kundi analolilamisha kuamua kutochanjwa. Mwanzoni ilionekana kama ni yeye na familia yake, lakini anajisahau na kuonesha kama ni kanisa lake zima halitachanjwa.

Hatuna utamaduni wa kuvumiliana hasa inapokuwa anayepaswa kuvumilia ni taasisi yenye mamlaka. Waliitwa dhaifu wakapiga kelele ila wao wakiita wenzao “wa hovyo” inakuwa sawa.

Gwajima atashutumiwa kwa kukwamisha shughuli za serikali. Enzi za kodi ya kichwa, niliwahi kushitakiwa mahakama ya mwanzo kuizuia serikali kukusanya mapato nilipokataa kulipa kodi katika kata ninayoishi lakini nimelipa kata nyingine katika halmashauri hiyo hiyo moja!! Kesi ilichukua dakika 10 nikaachiwa huru. Hata Gwajima hatashutumiwa lakini tutegemee kutosikia akizungumzia kutochanjwa tena! Ninahisi Spika katumiwa tu, Gwajiboy amelengwa na mamlaka za juu zaidi!
 
Kwa kupata kwako hizo jabs sisi tumepona
 
Watanzania mnavyojua kudaka misamiati ya kibeberu hamjambo. Eti go get a "jab", nadhani baada ya hiyo utaenda pia kupata "booster shot".
Brainwashed hao wasikuchanganye wasubiri booster zao zipo njiani
 
Nakumbuka yule mwanamke msinzi alipoletewa mbele ya Yesu, alinena"ambae hana kosa awe wa kwanza kumrushia jiwe" walitokomea na kumuacha Yesu na mwanamke.
 
Sasa hoja zake azilete ushahidi wa ki science na mabara aliyo chunguza, tafiti hupingwa kwa tafiti za ki science sio kuongea ongea kuhadaa wajinga wenzake
Maswali ya Gwajima ndyo Yale Yale aliyoongea mollel labda aanze Kwanza kututhibitishia huyo naibu waziri
 
Mku nafikiri shida sio chanjo lakini watu wanajiuliza, ile fomu ya kuweka sahihi yako kwamba kwa lolote litakalotokea baada ya mtu kupata chanjo, asimulaumu mtu yoyote nafikiri ndo inawapa wasiwasi. Unajua kwamba mwananchi wa kawaida hana uwezo kujua na kuhakiki usalama wa chanjo. Serikali yetu ndo ina watalamu/machineries na Govt Depts kama TBS etc. Hapo ndo wanabaki njia panda.
 
Jibu mojawapo tayari kalitoa ambalo lina ushahidi wa sauti na maneno ya waziri wa afya na naibu wake. Wakati wa JPM waliwaaminisha wananchi kuwa chanjo hazifai na ni hao tena wakati wa Suluhu wanasema chanjo ni nzuri, watu wakachanje. Ni vigumu kuwaamini watu walewale waliokataa chanjo na sasa wanawaaminisha wananchi kuwa chanjo ni nzuri. Tayari amesema kuwa ilifaa waondolewe, wawekwe wengine kwa kuwa inakuwa katika logic ya kawaida UWONGO(FALSE) na UKWELI(TRUE) haiwezi kuwa ni KWELI na ikiwa umesemwa na mtu yule yule. Kuaminika kwake ni vigumu!!!.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…