Kamati ya Bunge - Nishati: Mgawo wa Umeme mwisho Aprili 2024

BARD AI

JF-Expert Member
Joined
Jul 24, 2018
Posts
3,591
Reaction score
8,826
Your browser is not able to display this video.
Hadi kufikia Mwezi April mwaka 2024 Watanzania hawatakuwa na tatizo la mgao wa umeme kufuatia kukamilika kwa vituo vya kuzalisha umeme sambamba na kuanza kwa uzalishaji wa bwawa la umeme la Mwalimu Nyerere.

Kauli hiyo imetolewa na David Mathayo mwenyekiti wa kamati ya kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini, katika ziara yao ya kutembelea vituo vya kuzalisha umeme mkoani Tanga, ambapo amewahakikishia watanzania kuwa hakutakuwa na mgao wa umeme ifikapo mwezi April 2024.

Naye mwenyekiti wa bodi ya Wakurugenzi TANESCO, Balozi Meja Jenerali, Paul Kisesa Simuli amewataka wawekezaji kujipanga kuzalisha bidhaa kwa wingi utokana na serikali kujidhatiti kuhakikisha suala la mgao wa umeme linabaki kuwa historia.
 
Ni mwezi wa nne kumbe! Maana rais alisema mwezi wa tatu ndio mwisho?
Kwa hiyo tuna miezi mitano mbele ya mgao!
 
Hainabtofauti na hii habri Mwendokasi kuanza kazi mwishoni mwa mwaka 2022...
 
Ni mwezi wa nne kumbe! Maana rais alisema mwezi wa tatu ndio mwisho?
Kwa hiyo tuna miezi mitano mbele ya mgao!
Yaani wanasubiria bwawa la Mwl Nyerere, hii nchi ni kizungumkuti
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…