Kamati ya Bunge yawataka Watumiaji wa Daraja la Nyerere, Kigamboni Kulipia Bando

Kamati ya Bunge yawataka Watumiaji wa Daraja la Nyerere, Kigamboni Kulipia Bando

Stephano Mgendanyi

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2020
Posts
2,833
Reaction score
1,301

WhatsApp Image 2024-11-13 at 16.25.05.jpeg

*Yasema matumizi ya bando ni nafuu na yanaondoa usumbufu

*Yaipongeza NSSF kwa kuweka mifumo katika Daraja hilo

Na MWANDISHI WETU,

Dar es Salaam. Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ustawi na Maendeleo ya Jamii, imeridhishwa na utaratibu wa manunuzi ya bando la tozo kwa matumizi ya Daraja la Nyerere, Kigamboni ambapo imewataka watumiaji wa daraja hilo kulipia bando kwa sababu ni nafuu, rahisi na linapunguza msongamano na kuongeza mapato.

WhatsApp Image 2024-11-13 at 16.25.05 (2).jpeg

Akizungumza wakati wa majumuisho ya ziara ya kamati hiyo, Novemba 11 2024, ilipotembelea miradi ya NSSF ukiwemo wa Daraja la Nyerere, Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Mhe. Fatma Toufiq, amepongeza kazi kubwa inayofanywa na NSSF katika Daraja hilo hususan ya kuweka matumizi ya bando.

“Tunaendelea kuipongeza Serikali na wenzetu wa NSSF kwa kazi nzuri sana ambayo imefanyika pale Daraja la Nyerere kiukweli kumewekwa mifumo mizuri ambayo licha ya kupunguza changamoto ya foleni lakini pia inapunguza mianya ya upotevu wa mapato,” amesema Mhe. Fatma.

WhatsApp Image 2024-11-13 at 16.25.08.jpeg

Amesema Kamati pia inamshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa namna anavyoleta maendeleo nchini kwa manufaa ya wananchi na kuwa wanaunga mkono juhudi zote zinazofanywa na Serikali ya awamu ya sita na kuwa wanaamini Mifuko ya Hifadhi ya Jamii ukiwemo wa NSSF utaendelea kuleta tija kwa wanachama kupitia uwekezaji unaofanywa na Mifuko hiyo.

Baadhi ya wajumbe wa kamati hiyo akiwemo Mhe. Katani Katani amepongeza mfumo wa manunuzi ya bando katika Daraja hilo na kuwataka wananchi kujiunga kwani ni mfumo rahisi na rafiki na pia unaondoa foleni.

WhatsApp Image 2024-11-13 at 16.25.04.jpeg

Naye, Mhe. Mariam Kisangi amesema mradi wa Daraja la Nyerere umechochea maendeleo ya wananchi wa Kigamboni, ambapo amewataka kuendelea kulipia tozo za kupita kwa kutumia bando kwani inapunguza usumbufu.

Kwa upande wake, Mhe. Athumani Maige amewataka wananchi kuendelea kutumia matumizi ya bando wakati wanapopita katika Daraja hilo na pia ameipongeza NSSF kwa usimamizi mzuri wa mradi huo.

Awali, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu, Mhe. Ridhiwani Kikwete, amesisitiza elimu iendelee kutolewa kwa wananchi na watumiaji wa Daraja kutumia malipo ya bando kwani ni rahisi na inapunguza usumbufu.

“Matumizi ya bando ni mazuri na yataongeza mapato, kupunguza kero kwa watumiaji wa Daraja hivyo ni muhimu wananchi kupewa elimu zaidi ili watumie bando kuondoa usumbufu,” amesema.

WhatsApp Image 2024-11-13 at 16.25.06 (1).jpeg

Mkurugenzi Mkuu wa NSSF, Bw. Masha Mshomba amesema wanaendelea kuwahamasisha watumiaji wa Daraja kulipia bando la siku, wiki au mwezi ili waweze kupita kwa urahisi hasa ukizingatia kuwa matumizi ya bando ni nafuu zaidi.

Bw. Mshomba ameipongeza kamati hiyo na kuahidi kuwa maoni, maelekezo na ushauri uliotolewa na wajumbe wa kamati hiyo wataufanyia kazi kwa ajili ya utekelezaji.
WhatsApp Image 2024-11-13 at 16.25.05 (1).jpeg


WhatsApp Image 2024-11-13 at 16.25.06 (1).jpeg
WhatsApp Image 2024-11-13 at 16.25.04.jpeg
WhatsApp Image 2024-11-13 at 16.25.05.jpeg
WhatsApp Image 2024-11-13 at 16.25.05 (1).jpeg
WhatsApp Image 2024-11-13 at 16.25.05 (2).jpeg
WhatsApp Image 2024-11-13 at 16.25.06.jpeg
WhatsApp Image 2024-11-13 at 16.25.07 (1).jpeg
WhatsApp Image 2024-11-13 at 16.25.08.jpeg
GcH2mP4XQAAY-zn.jpg
 
Mbona amsemi kuwa deni limekwisha au Bado kiasi gani?
Oh okay sawa
 
Back
Top Bottom