#COVID19 Kamati ya Corona: Serikali itoe taarifa uwepo wa Ugonjwa wa COVID-19 na kuruhusu matumizi huru ya chanjo

Kwanini wasianze kuchanjwa watafiti kwanza.? Eti vyombo vya ulinzi ndio vianze!!, wakigandiana damu Taifa litalindwa na nani?
 
Hii TUME ILIKUA YA NINI KUNA AMBACHO HAKIJULIKANI?
Nchi haiendeshwi kwa hisia lazima tupate mahali ambapo ni official pa kuanzia., mama ilibidi aunde hiyo Tume sasa ripoti imetolewa official muacheni mama aanzie na hapo kabla ya hapo nchi ilikuwa kwenye sintofahamu, mara ugonjwa haupo mara upo lakini tuite ugongwa wa ukosefu wa kupumua mara hivi mara vile.,

Mama nampongeza sana kuanza chanjo huru atakayeona ana haja atachoma atakayeona hana haja atatulia. BigUpMama.,
Kiongozi mzanzibari ni bora mara elfu1 ata kama ni mwanamke kuliko wanaume 10 kutoka kule unyamwezini.
 
Kwenye Hilo tumeingizwa mkenge,sijajua sifa na weledi walionao walioitwa wajumbe wa hiyo tume. Rais wetu tunakupenda lkini kwa hili la chanjo hatuko na wewe kabisaaa.
Sema siko na wewe. Sisi wengine tuko nae wee vipi.
 
Nipo uingeleza na nchi inaendelea kufunguliwa.Sababu ya kufungua nchi ni kupungua kwa vifo na kupungua watu kuzidiwa na kupelekwa hospitali.Lockdown na chanjo ndo ilipelela kufikia hapa sio kingine.

Mpaka sasa zaidi ya nusu ya raia wa uingereza (na bado wanaendelea mpaka target ifike) wamepata chanjo huku wakiendelea ku monitor whole situation.

Mimi hapa nishapata chanjo na watu wengi tu nnaowajua wana chanjo.sisemi bongo waweke lockdown,ila msiwatishe wale wanaotaka kujikinga,corona haiondoki leo wala kesho,na mkiiachia sana ndo inaendelea ku mutate,sikilizeni wataalamu wenu acheni uzuzu.
 
Soon, rais ataambiwa TZ mulichelewa, kopa pesa kwa ajili ya COVID. Naanza kuona anguko letu ili wasema JPM alituponza.
wamchome yeye kwanza aliyeunda kamati then wawachome kamati nzima na familia zao then tuwasikikizie
 
Wewe unajuwa wanaokufa kwa Corona hapa Tanzania ni wangap kwa siku tofauti nan huko India?
 
Kwanza huyu ni Rais wa Katiba tu,Kama sio kubebwa na Magufuri Nani angelikubari Samia awe rais wetu,rais gani nyoronyoro hivi,aende kwao zanzibar sie Watanganyika tulisha choka,kwanza ni mvivu.anawaza misaada tu.
Hahahaa...

Hamna Rais pale.

Dhaifu mno!
 

wamefanikiwa wapi watu bado wanavaa barakoa mama kwenye hili atuache asituue kama vipi waanze na wanasiasa kwanza bungeni then wafate wakuu wa mikoa na wakuu wa wilaya na wakurugenzi
 

Nawashangaa Baadhi ya watu kuanza mijadala ya kupinga suala la chanjo kama vile serikali imelazimisha kila mtu achanjwe.

Hatuwezi kuwa na mawazo yanayolingana ndani ya nchi hii tupo tunaotaka chanjo na tuna sababu zetu kwa mfano. Biashara za kimataifa, working overseas n.k kwa sasa kama huna kinga huwezi kuingia katika nchi zingine.

Na wanaopinga chanjo nao wana sababu zao kwamfano wengine wanasema chanjo ni mpango wa mabeberu kutuua .sawa zote ni sababu.

Kimsingi naipongeza serikali kuweka Uhuru kwa kila mwananchi kuamua anaetaka sawa na asiyetaka sawa. TUSIPANGIANE.
 
Wapumbavu wanawaza kununuliwa wana ushahidi gani. Waseme tu hawataki inatosha na sio visingizio vya mabeberu na kununuliwa. Waseme tu kama corona ipo dfuniani au la.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…