#COVID19 Kamati ya Corona: Serikali itoe taarifa uwepo wa Ugonjwa wa COVID-19 na kuruhusu matumizi huru ya chanjo

Ngoja tuone mkuu
 
Kwakuwa waTz wameishi na kike kinachoitwa Corona kwa miaka miwili sasa na hakuna imoact ueyote tuliyoiona, mi nadhani huo wote ni utopolo tu, hakai mtu lockdown, na hizo pesa za kodi wanazotaka kuchezea kwenye chanjo watazitapika!!
Cool bana, hakuna aliyetangaza lockdown. Wananchi walikaririshwa kipindi kile kuwa mabeberu wanataka muweke lockdown- ulikuwa uongo mtupu.
Na chanjo itakuwa hiari,, so endelea kurelax.
 
Hofu inalazimishwa ili tu kuonyesha kuwa hatua zinazochukuliwa sasa si sahihi kwasababu za ajabuajabu sana.
Mbona kikitokea kipindupindu tunaelezana njia za kukiepuka na wala hatuonyani kuhusu hofu?? Wala hatusemi haya masharti ya kipindupindu yataleta hofu hivyo watu watakufa sana.
Watanzania mlikuwa brainwashed na wansiasa wachumia tumbo hakika.
Lakini cha kujiuliza ,,tumeishi kwa kutegemea hii sayansi kwa muda mrefu sana, kwanini sasa??
Lakini pamoja na hayo ,magonjwa yote yakitokea tunaikimbilia sayansi,,, kwanini corona pekee??

Je ni kweli mzungu anashindwa kukuua wewe mbongo ikiwa kweli anataka kukuua mpaka aisubiri corona??

Hebu fikiria wakiamua kuwaua kwa kupitia AC za magari mnayonunua kwao watashindwa??

Amka mbongo ,,fikiria logically.
 

Niombe serikali kutoa agizo la ABIRIA wote kukaa viti kwenye daladala au magari ya biashara ya usafiri wa abiria; kwa kuzingatia idadi ya viti vya abiria katika gari husika, kama kweli imeanza kupambana na covid-19 kama tulivyojitahidi mwaka uliopita !
 
Korona ipo haipo? Watu wanakufa hawafi? Mnaogopa kuambiwa ukweli au? Ina maana timu ya wataalamu imetudanganya?

Lini watu waliacha kufa? Chanjo ya Malaria iko ima haiko?. Kwa nini maendeleo ya sayansi na technologia yaliyo wezesha upatikanaji wa chanjo ya corona kwa kasi ya voda fasta yasiwezeshe na chanjo ya malaria? Maana wako wataalamu wanasema upatikanaji wa chanjo ya corona ndani ya kipindi kifupi umesababishwa na maendeleo ya technologia.

Unaposema unachanja watumishi wa vyombo vya ulinzi na usalama kuna uhiari tena hapo au ni mwendo wa amri na ndio afande, timamu. Tusidanganyane wako watu wamedhamiria kuwa madalali wa chanjo na vifaa tiba.

Wengine hatuko tayari kuwa nguruwe guinea/panya weupe wa majaribio kwa hii chanjo ya korona.

'Nguto' kwa kikojani ni 'tiger.'
 
Cool bana, hakuna aliyetangaza lockdown. Wananchi walikaririshwa kipindi kile kuwa mabeberu wanataka muweke lockdown- ulikuwa uongo mtupu.
Na chanjo itakuwa hiari,, so endelea kurelax.
Hiari hilo liko wazi, suala ni pesa zitakazotumika kuagiza, ni kodi zetu au ni zao binafsi?
 
Tangu Corona imeanza na watu wamekaa kwa kubanana hivyo, kuna chochote kimetokea?
 
Hiari hilo liko wazi, suala ni pesa zitakazotumika kuagiza, ni kodi zetu au ni zao binafsi?
Hayo ndiyo matumizi sahihi ya kodi za wananchi.
Watu walitaka kulazimishia kijiji kiwe jiji tuliona poa tukasema ni sehem ya Tanzania, halafu eti tuone ni dhambi serikali kulinda wananchi wake dhidi ya magonjwa.
 
Finaly we are here, wanaotaka chanjo wasinyimwe haki yao, na wasiotaka pia waheshimiwe, sijui mwendazake angekua macho angesemaje
Mimi sina imani nao hao watu wa Laboratory tangu Hayati Dr Magufuli kuwapa Vipimo vya Mbuzi ,Damu ya kwale,mafuta ya dizeli na mafenisi yote hayo walipima hao Wana-Sayansi wa Laboratory. Na Wakakuta Vipo Positive Covid19?
Leo Mheshimiwa Rais Mama Suluhu amewapa hao hao Wana -Sayansi wa Laboratory kupima Chanjo ya Corona Virus? Unafikiri watasema haifai kuchanjwa? Au si Salama? Sisi Waafrika Akili zetu kitu kikitoka kwa Mzungu tuna imani kipo salama. Kumbe kina madhara makubwa sana.

 
Tanzania Hakuna Wataalam Wazuri ni watu kuiga atakacho kisema mtu Mweupe M-Taaalam wa Tanzania hawezi kukipinga. tuna Wana-Sayansi feki Tanzania.
 
Mkuu sio kwamba watu wanapingana na sayansi ila uhalisia ndio unaopingana na hiyo mnayoita sayansi, kwa jinsi ambavyo bongo tulivyojiachia kwa kutozingatia taratibu za kujikinga na corona basi ilitakiwa tuone athari zake kwa kiwango kikubwa kabisa na hali hiyo ingeelezeka kisayansi kama inavyoelezeka huko India, lakini uhalisia unaeleza tofauti na hiyo sayansi mnayoizungumzia. Bongo tumekuwa ndio kwanza tunaogopa kuletewa corona kutoka nchi za nje kama huko India au Afrika kusini.
 
Kwanza hatuweki record yoyote hivyo situation chini kwetu ni ya kuhisia tu.
Kwanini India iko vile: Ni vizuri pia kutafiti hizo sababu,, mpaka sasa zipo ambazo hazijathibitika.

Mfano mzuri kwako ni Rwanda.
 
Kwanza hatuweki record yoyote hivyo situation chini kwetu ni ya kuhisia tu.
Kwanini India iko vile: Ni vizuri pia kutafiti hizo sababu,, mpaka sasa zipo ambazo hazijathibitika.

Mfano mzuri kwako ni Rwanda.
Record zingetueleza tumeathirika kwa kiasi gani lakini wakati huo athari tunaziona, yani ilitakiwa tuone hospitali kuzidiwa kuelemewa kwa wagonjwa wenye kuhitaji mashine za kusaidia kupumua na hali ya mazishi kuongezeka kama ambavyo tumesikia wenzetu sehemu za kuhifadhi maiti zilijaa na huko India tunasikia hadi kuni za kuchomana zimeisha. Sasa hizo ni athari ambazo tungeziona na hapo ndio record zingetuambia kiwango cha maambukizi,wagongwa waliyopo na vifo. Sasa huwezi kusema hatuoni hayo kwa sababu hatuweki record.
 
Sasa tumeamua tutafute data ili tujue nguvu ya adui wetu na kisha tujue tunamtokomeza kiasi gani,- lina ubaya hilo?
Dunia inairate kila nchi kulingana na situation yake, Tanzania imekuwa siku zote ni unknown , hata tu jinsi ya kujieleza ni aibu tupu.
 
Mwendazake alitupoteza sana, kusema chanjo ya Corona ina matatizo wakati chanjo nyingine za wazungu tunazitumia miaka mingi hakuwa sawa, hasa alipodai wazungu hawatupendi it was such a very primitive mentality.
Alichokisahau yeye na waliomuunga mkono ni kuwa vingi vya mabeberu tunavyovitumia kv: "mionzi ya simu, magari, ndege zifushazo moshi angani zinapokatiza anga letu... vifaa tiba toka hukohuko kwa wazungu" walijiridhisha kuwa havina athari???
 
umieni Chanjo kutoka China ambayo hadi sasa haijapatikana na kasoro za kuhatarisha maisha kama chanjo zinazoka kwa wazungu .
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…