Albinoomweusi
JF-Expert Member
- Oct 28, 2016
- 3,433
- 8,585
Ngoja niwe mkweli, kamati ya hadhi ya wachezaji haiwezi kuamua kesi ya Fei Toto, nimesikiliza interviews za Mwenyekiti Mzee Said Sudy namna anavyoongea unajua kabisa hakuna wanachoweza kuamua.
Kamati inataka kusawazisha ubao, inataka kuibeba Yanga, inataka kujisafisha mbele ya Yanga kutokana na mahusiano yao kuanzia kesi ya Morrison na sakata la “Bingwa la Kufeli”.
Hakuna mkataba wa kazi duniani hauvunjiki na hakuna namna ya mkataba wa Feisal umeelekeza kwamba hawezi kuuvunja akaondoka. Wanaoimba Busara wanataka Fei aingie upepo na arudi Yanga kutumikia mkataba asoupenda.
Waandishi na watu wenye nguvu mitandaoni wanatumika kupotosha hili sakata makusudi ili kutisha wachezaji wazawa waendelee kucheza kwa huruma. Lakini ukweli ni kwamba FEISAL keshaondoka Yanga na sasa au mwisho wa msimu atacheza sehemu nyingine.
GENDAEKA wengi wanapiga kelele ili kuifunika Kamati ya hadhi ya wachezaji ambayo kimsingi ni kamati dhaifu. Kwangu mimi hii kesi Feisal anakwenda kushinda CAS au mamlaka za kinchi lakini hawezi kucheza Yanga. Yanga wakubali tu kwamba Feisal ana uwezo wa kununua mkataba wake na akaendelea na maisha mengine.
Hili litakua funzo kwa idara za Sheria pamoja na wanaosajili wachezaji na wanaosimamia wachezaji. Niwakumbushe tu, hakuna mkataba usofunjika Duniani kote. Kama Simba walivyovunja mkataba kwa Akpan na Okwa na kama Yanga kwa Kambole.
Che Guevara🫡
NB:
Vicent Aboubakary baada ya kutakiwa na Man United ameamua kuvunja mkataba na Al Nasry.
Kamati inataka kusawazisha ubao, inataka kuibeba Yanga, inataka kujisafisha mbele ya Yanga kutokana na mahusiano yao kuanzia kesi ya Morrison na sakata la “Bingwa la Kufeli”.
Hakuna mkataba wa kazi duniani hauvunjiki na hakuna namna ya mkataba wa Feisal umeelekeza kwamba hawezi kuuvunja akaondoka. Wanaoimba Busara wanataka Fei aingie upepo na arudi Yanga kutumikia mkataba asoupenda.
Waandishi na watu wenye nguvu mitandaoni wanatumika kupotosha hili sakata makusudi ili kutisha wachezaji wazawa waendelee kucheza kwa huruma. Lakini ukweli ni kwamba FEISAL keshaondoka Yanga na sasa au mwisho wa msimu atacheza sehemu nyingine.
GENDAEKA wengi wanapiga kelele ili kuifunika Kamati ya hadhi ya wachezaji ambayo kimsingi ni kamati dhaifu. Kwangu mimi hii kesi Feisal anakwenda kushinda CAS au mamlaka za kinchi lakini hawezi kucheza Yanga. Yanga wakubali tu kwamba Feisal ana uwezo wa kununua mkataba wake na akaendelea na maisha mengine.
Hili litakua funzo kwa idara za Sheria pamoja na wanaosajili wachezaji na wanaosimamia wachezaji. Niwakumbushe tu, hakuna mkataba usofunjika Duniani kote. Kama Simba walivyovunja mkataba kwa Akpan na Okwa na kama Yanga kwa Kambole.
Che Guevara🫡
NB:
Vicent Aboubakary baada ya kutakiwa na Man United ameamua kuvunja mkataba na Al Nasry.