OKW BOBAN SUNZU
Platinum Member
- Aug 24, 2011
- 53,868
- 121,001
Mhamasishaji wa Yanga SC amekubali makosa aliyofanya kwa Rais wa TFF Ndugu WALLACE KARIA na kusema alienda kumuomba msamaha nyumbani kwake huku wakinywa juice.
Baada ya kukana hadharani kwamba hakukuwa na ugomvi kati yao, hatimaye amekubali kwamba kulikuwa na ugomvi na kwamba alimtafuta kumuomba radhi kwa kumkosea adabu mbele ya halaiki.
Nimetamani hii ndiyo ingekuwa mwisho wa hata kesi ya maadili inayomkabili mhamasishaji.
Lakini sasa utaratibu ndo unazuia hili jambo kuwa limemalizika kwa kuomba msamaha. Kanuni za maadili haziombwi msamaha na ukizingatia maadili yamevunjwa kumuendea Rais TFF na sio Wallace Karia. Rais wa TFF aliyekuwa mkuu wa protokali siku hiyo kiwanjani pale Arusha.
Kiti au Mamlaka ndiyo yemekosewa maadili na sio mtu. Kwahiyo kimsingi hata kamati ya maadili sidhani kama ina kazi kubwa kutafuta ushahidi kwakuwa mwenyewe kashakubali na kuomba msamaha hadharani akikili kukosea.
Kwa ufahamu wangu kamati ya maadili ni kamati huru ambayo haiingiliwi na mtu yoyote hata Rais wa TFF ambaye anaiteua.
Kwahiyo msamaha wa Karia kwa mhamasishaji kama ameutoa hauna la kufanya na kesi yake kwenye kamati.
Kazi ya kamati ni kuhakikisha maadili yanafatwa kwa kuhukumu ipasavyo wale wanaokiuka kanuni.
Kuna wengi wamehukumiwa na kamati hii na sasa wanatumikia hukumu zao. Wengi wao hawakuwa na nafasi ya kuongea na wakubwa na kunywa nao juice wakiomba msamaha.
Kwa namna yoyote ile watakuwa wanaifatilia hii kuona nini kitaendelea baada ya msamaha. Mvuto umekuwa mkubwa zaidi baada ya mtuhumiwa kuomba radhi na kukiri hadharani makosa yake.
Kuna mtego mkubwa kwa kamati na uongozi wa TFF kwenye jambo hili. Kuna dhana ya baadhi ya watu kuwa hawagusiki kwenye mpira wetu na kuwafanya wajione wakubwa wenye haki kuliko wengine.
Hili linaweza kuleta tafsiri mbaya kwenye uongozi unaofuata taratibu kama wa TFF hii ya Rais Wallace Karia.
NB: Sikuja mjini kujuana na watu, mtu mwenyewe wa kujuana nae nani?
BIN KAZUMARI (The voice of the voiceless)
My Take
Kama msahama utaharibu maamuzi basi nyinyi na Manara wote ni watu wa hovyo na mnalea upuuzi kwenye soka
Baada ya kukana hadharani kwamba hakukuwa na ugomvi kati yao, hatimaye amekubali kwamba kulikuwa na ugomvi na kwamba alimtafuta kumuomba radhi kwa kumkosea adabu mbele ya halaiki.
Nimetamani hii ndiyo ingekuwa mwisho wa hata kesi ya maadili inayomkabili mhamasishaji.
Lakini sasa utaratibu ndo unazuia hili jambo kuwa limemalizika kwa kuomba msamaha. Kanuni za maadili haziombwi msamaha na ukizingatia maadili yamevunjwa kumuendea Rais TFF na sio Wallace Karia. Rais wa TFF aliyekuwa mkuu wa protokali siku hiyo kiwanjani pale Arusha.
Kiti au Mamlaka ndiyo yemekosewa maadili na sio mtu. Kwahiyo kimsingi hata kamati ya maadili sidhani kama ina kazi kubwa kutafuta ushahidi kwakuwa mwenyewe kashakubali na kuomba msamaha hadharani akikili kukosea.
Kwa ufahamu wangu kamati ya maadili ni kamati huru ambayo haiingiliwi na mtu yoyote hata Rais wa TFF ambaye anaiteua.
Kwahiyo msamaha wa Karia kwa mhamasishaji kama ameutoa hauna la kufanya na kesi yake kwenye kamati.
Kazi ya kamati ni kuhakikisha maadili yanafatwa kwa kuhukumu ipasavyo wale wanaokiuka kanuni.
Kuna wengi wamehukumiwa na kamati hii na sasa wanatumikia hukumu zao. Wengi wao hawakuwa na nafasi ya kuongea na wakubwa na kunywa nao juice wakiomba msamaha.
Kwa namna yoyote ile watakuwa wanaifatilia hii kuona nini kitaendelea baada ya msamaha. Mvuto umekuwa mkubwa zaidi baada ya mtuhumiwa kuomba radhi na kukiri hadharani makosa yake.
Kuna mtego mkubwa kwa kamati na uongozi wa TFF kwenye jambo hili. Kuna dhana ya baadhi ya watu kuwa hawagusiki kwenye mpira wetu na kuwafanya wajione wakubwa wenye haki kuliko wengine.
Hili linaweza kuleta tafsiri mbaya kwenye uongozi unaofuata taratibu kama wa TFF hii ya Rais Wallace Karia.
NB: Sikuja mjini kujuana na watu, mtu mwenyewe wa kujuana nae nani?
BIN KAZUMARI (The voice of the voiceless)
My Take
Kama msahama utaharibu maamuzi basi nyinyi na Manara wote ni watu wa hovyo na mnalea upuuzi kwenye soka