Kamati ya rufaa TFF yaridhia Wambura kufungiwa maisha kujihusisha na soka

Kamati ya rufaa TFF yaridhia Wambura kufungiwa maisha kujihusisha na soka

Aende CAS kwani TFF imejaa WAPUUZI,jamaa wamemuonea .Yaani kuna baadhi ya matukio hutokea Tanzani pekee yake
1.Unamuhukumu mtu bila yeye mwenyewe kuwepo kujitetea.
2.Kampuni ya JACKS ambayo wanadai wambura kafoji hizo stakabazi,hawajapewa taarifa waje kutoa ushahidi na wala wao wenyewe kuziverify hizo stakabadhi zao.
3.Yote tisa 10 TFF wao wenyewe wanaverify hizo stakabadhi,wakati kwa hapa Tanzania wenye uwezo wa verify document ni TAKUKURU pekee.
Yaani jamaa akienda CAS anashinda kabisa.
Tuko kwenye taratibu za kumpeleka takukuru na vyombo vingine vya dola
 
Soka letu halifanikiwi kwa sababu ya wapigaji, mimi shabiki kindakindaki wa simba nasema wapigaji wote hadi kina aveva funga wote haiwezekani soka letu kila siku halisongi mbele
 
Tuko kwenye taratibu za kumpeleka takukuru na vyombo vingine vya dola
Kwa nini msingeanza na TAKUKURU na JACKS alafu ndio mngeamua kumfungia na je huko mahakamani akishinda mtamrusdisha wakati mshamchagua Nyamlani ambaye naye ana tuhuma za kimaadili (Ref Shaffih Dauda).
 
Kuna haja ya TFF kuvunjwa tukae hata miaka 2 bila kuwepo tuji tathimini upya kama Tuna watu sahihi wa kuongoza soka letu..
 
Sasa ulitaka rufaa yake isikilizwe na CHANETA ,Chama cha Netiboli Tanzania??
na chombo kingine kilicho huru, hata hiyo kamati ingekuwa ni ya wizara husika ingesound kidogo, ila sijui muundo wake, kama iko hivyo basi haki haiwezi kuonekana kutendeka achilia mbali kutendeka
 
Mimi nawaambia huyu jamaa ni mbishi atapambana hadi atashinda
 
Kushinda lazima ashinde, sababu TFF walimuhukum bila kumsikiliza.
 
Back
Top Bottom