Kamba ya kitovu kumzunguka mtoto shingoni

Kamba ya kitovu kumzunguka mtoto shingoni

OCC Doctors

Senior Member
Joined
Jul 20, 2018
Posts
113
Reaction score
172
Kamba ya kitovu kumzunguka mtoto shingoni kabla ya kuzaliwa (nuchal cord), matatizo yanaweza kujumuisha shida ya kupumua, na kuzaa mtoto aliyekufa.

Kamba ya kitovu inaweza kumzunguka mtoto kwa ulegevu (loose), na inaweza kumzunguka mtoto kisha ikamkaza (tight), na inaweza kumzunguka mtoto mara mbili (double nuchal cord) ambapo huwa ni ngumu kwa mtoto kujinasua.

Mara nyingi kunahusishwa na hatari kubwa zaidi ikiwemo uharibifu wa ubongo wa muda mrefu au kupooza kwa ubongo kunaweza kutokea.

Insta-Reflectors.jpg

Kikawiada Kamba ya kitovu hulindwa na mafuta laini yaitwayo 'Wharton's jelly'. Husaidia kamba isijifunge fundo ili mtoto awe salama bila kujali ni kiasi gani anajikunyata na kujipindua ndani ya tumbo la mama yake.

Inapotokea kamba ya kitovu ina upungufu wa mafuta hayo laini (insufficient Wharton’s jelly), hiyo inafanya uwezekano wa kamba kujifunga fundo au kumzunguka mtoto shingoni (Nuchal Cord ).

Hivyo basi, kamba itamzunguka mtoto ikiwa ni watoto mapacha, kuwepo kwa maji mengi ya uzazi, kamba kuwa ndefu na yenye muundo duni.


View attachment 2726398
 
Hii ni Hatari sana mkuu ilimkumba mwanamke fulani hivi hadi kupelekea mtoto kufariki nayeye kuchanwa kisu alikua hajafanya ultrasound kabla so hakujua!

Wakati wa kujifungua alisikia uchungu kawaida sukuma sukuma nawewe kumbe anavozidi kusukuma ndio anamkaba mtoto ila madokta wanashangaa mbona njia imefunguka mama anasukuma vizuri ila muda unaenda mtoto hatoki ndio kumpeleka theatre masikini mtoto alikua ameshafariki so aliuguza kidonda tu!!😌

Inauma sana!
 
Hii ni Hatari sana mkuu ilimkumba mwanamke fulani hivi hadi kupelekea mtoto kufariki nayeye kuchanwa kisu alikua hajafanya ultrasound kabla so hakujua ...

Jamani nimejisikia huzuni kweli.
Kupitia kipindi cha post portum bila mtoto unaweza hata ukawa chizi bila kusali sana.

Kila kitu kinakuwa kinakukumbusha kwamba hauna mtoto. Maziwa yakianza kutoka ni huzuni maana unakumbuka hauna mtoto. Huo mshono ukiuma ni huzuni maana unakumbuka hauna mtoto.

Mungu atusaidie wanawake wote maana uzazj una changamoto zake nyingi sana.
 
Jamani nimejisikia huzuni kweli.
Kupitia kipindi cha post portum bila mtoto unaweza hata ukawa chizi bila kusali sana.

Kila kitu kinakuwa kinakukumbusha kwamba hauna mtoto. Maziwa yakianza kutoka ni huzuni maana unakumbuka hauna mtoto. Huo mshono ukiuma ni huzuni maana unakumbuka hauna mtoto.

Mungu atusaidie wanawake wote maana uzazj una changamoto zake nyingi sana.
Yaniii ni maumivu yasiyo na mfano!!
Afu serikalini Hospitali wao wanawaweka hodi moja ya waliojifungua kwa oparie so tukienda kumuona vile tunavoona vitanda vya pembeni yao kila mmama kakumbatia kachanga kake au anakaangalia na kukaweka sawa kachanga kake huku yeye anauguza kidonda tu na kuumia kifua kwa kujaa kwa maziwa bila katoto ka kuyanyonya tunaumiaaaa sanaa sasa hapo ni sie tuloenda kumuona je yeye majonzi na maumivu yake??!!!!!
Usiku wodini vichanga vya wenzie ni ng'aaa ng'aaaa ng'aaa yeye bilabila dahhh!!
Nesi akipita kwake ni kuishia kuangalia hali ya kidonda tu Huku wenzie anaangalia na hali za vichanga!!

Mungu atusaidie sana wanawake mambo ya uzazi 🙌!
 
Hali hii huwa inasababishwa na nini
Wakati wa ujauzito, watoto huelea kwenye mfuko wenye maji ya uzazi.
Mfuko huu huwaruhusu watoto wazunguke, wacheze pamoja na kuhama kutoka sehemu moja kwenda nyingine wakiwa ndani yake.
Pia hizi zinaweza zikawa sababu:-
  1. Kuwa na kitovu kirefu sana
  2. Mfuko wa uzazi kuwa na maji mengi sana
  3. Kuwa na ujauzito wa mtoto zaidi ya mmoja (3, 4, 5)
 
Wakati wa ujauzito, watoto huelea kwenye mfuko wenye maji ya uzazi.
Mfuko huu huwaruhusu watoto wazunguke, wacheze pamoja na kuhama kutoka sehemu moja kwenda nyingine wakiwa ndani yake.
Pia hizi zinaweza zikawa sababu:-
  1. Kuwa na kitovu kirefu sana
  2. Mfuko wa uzazi kuwa na maji mengi sana
  3. Kuwa na ujauzito wa mtoto zaidi ya mmoja (3, 4, 5)
Santrooo sana dokta!!
 
Yaniii ni maumivu yasiyo na mfano!!
Afu serikalini Hospitali wao wanawaweka hodi moja ya waliojifungua kwa oparie so tukienda kumuona vile tunavoona vitanda vya pembeni yao kila mmama kakumbatia kachanga kake au anakaangalia na kukaweka sawa kachanga kake huku yeye anauguza kidonda tu na kuumia kifua kwa kujaa kwa maziwa bila katoto ka kuyanyonya tunaumiaaaa sanaa sasa hapo ni sie tuloenda kumuona je yeye majonzi na maumivu yake??!!!!!
Usiku wodini vichanga vya wenzie ni ng'aaa ng'aaaa ng'aaa yeye bilabila dahhh!!
Nesi akipita kwake ni kuishia kuangalia hali ya kidonda tu Huku wenzie anaangalia na hali za vichanga!!

Mungu atusaidie sana wanawake mambo ya uzazi [emoji119]!

Zamani nilikuwa najua ukisha beba mimba tu ndio habari imeisha usubiri kubeba mtoto tu!

Khaaa kumbe changamoto hadi umpakate huyo mtoto ni za kutosha hapo katikati. Miscarriages na stillbirth za kutosha.

Yaani ukiona mtu kajifungua salama na ana mtoto wake apewe tu maua yake maana si mchezo.
 
Zamani nilikuwa najua ukisha beba mimba tu ndio habari imeisha usubiri kubeba mtoto tu!

Khaaa kumbe changamoto hadi umpakate huyo mtoto ni za kutosha hapo katikati. Miscarriages na stillbirth za kutosha.

Yaani ukiona mtu kajifungua salama na ana mtoto wake apewe tu maua yake maana si mchezo.
Kwakweli tupewe tu maua yetu!!
 
Kikawiada Kamba ya kitovu hulindwa na mafuta laini yaitwayo 'Wharton's jelly'. Husaidia kamba isijifunge fundo ili mtoto awe salama bila kujali ni kiasi gani anajikunyata na kujipindua ndani ya tumbo la mama yake.

Inapotokea kamba ya kitovu ina upungufu wa mafuta hayo laini (insufficient Wharton’s jelly), hiyo inafanya uwezekano wa kamba kujifunga fundo au kumzunguka mtoto shingoni (Nuchal Cord ).

Hivyo basi, kamba itamzunguka mtoto ikiwa ni watoto mapacha, kuwepo kwa maji mengi ya uzazi, kamba kuwa ndefu na yenye muundo duni.


Nuchal-Cord-Bubble-Thumbnail-transformed.jpeg
 
Hii ni Hatari sana mkuu ilimkumba mwanamke fulani hivi hadi kupelekea mtoto kufariki nayeye kuchanwa kisu alikua hajafanya ultrasound kabla so hakujua!

Wakati wa kujifungua alisikia uchungu kawaida sukuma sukuma nawewe kumbe anavozidi kusukuma ndio anamkaba mtoto ila madokta wanashangaa mbona njia imefunguka mama anasukuma vizuri ila muda unaenda mtoto hatoki ndio kumpeleka theatre masikini mtoto alikua ameshafariki so aliuguza kidonda tu!!😌

Inauma sana!
Pain 😩 😩
 
Back
Top Bottom