Kambi kwa Wanafunzi wa Kidato cha Pili katika Shule ya Sekondari Mkuu

Kambi kwa Wanafunzi wa Kidato cha Pili katika Shule ya Sekondari Mkuu

MrfursaTZA

Member
Joined
Jul 26, 2024
Posts
29
Reaction score
94
Natumai barua hii itakufikia salama. Mimi ni mzazi wa mwanafunzi aliye katika Kidato cha Pili katika Shule ya Sekondari Mkuu, wilayani Rombo. Nimeandika barua hii kuwasilisha maswali na malalamiko yangu kuhusu kambi inayotarajiwa kufanyika kwa wanafunzi wa Kidato cha Pili kwa gharama ya shilingi 215,000/-. Hali hii imeleta maswali mengi na wasiwasi katika familia nyingi, na kwa bahati mbaya, majaribio yangu ya kupata maelezo yanayohusiana na suala hili kutoka kwa viongozi wa shule, afisa elimu, na afisa mtendaji wa kijiji yamekosa majibu ya kuridhisha.

Haya ni maswali yangu:
1. Je, kambi hii ni lazima kwa wanafunzi? Kuna suala la kambi ya lazima, na je, mwanafunzi ambaye hatakwenda atakutana na madhara yoyote au kufukuzwa?
2. Je, gharama hii ya 215,000/- ni haki? Gharama hii ni mara tatu zaidi ya ada ya kawaida ya shule ambayo ni shilingi 79,000/-. Hii ni mzigo mzito kwa wazazi wengi, na je, hii inakubaliana na sheria au miongozo inayohusu haki za wazazi na wanafunzi?
3. Je, mwenyekiti wa bodi ya shule alikubaliana na pendekezo hili bila ushirikishwaji wa jamii? Inashangaza kwamba kambi hii ilipitishwa bila kutoa nafasi kwa wanajamii kutoa maoni yao. Wazazi wengi hawawezi kumudu gharama hii, na hii inaweza kusababisha migogoro na matatizo katika jamii, ikiwemo kuingilia mali za watu kufidia gharama hizi.
4. Je, kuna nafasi ya ushirikishwaji wa wanajamii na wazazi katika vikao vya maamuzi? Hii ni muhimu kwa ushirikishwaji wa jamii, na je, kuna uwezekano wa kutumia teknolojia kama vikundi vya WhatsApp ili kuwezesha wazazi na wanajamii kutoa maoni na kuulizwa kuhusu suala hili?

Katika juhudi yangu ya kupata majibu, nilijaribu kuwasiliana na Mkuu wa Shule, Afisa Elimu, na Afisa Mtendaji wa Kijiji, lakini walikataa kutoa maelezo na kunilazimisha nifike shuleni, licha ya kuwa mimi ni mzazi wa mtoto yatima na nipo mbali na shule. Baada ya hayo, Mkuu wa Shule, Bi. Julieth Nemes, alikata simu na kuni-block, jambo ambalo ni jambo la kushangaza na linalozua maswali kuhusu uongozi wa shule.

Ni wazi kuwa kuna hofu kubwa miongoni mwa wanakijiji kuhusu kutoa maoni kwa sababu ya hofu ya kuwa wanafunzi wao watafanyiwa visa. Hii ni hali ambayo inahitaji kushughulikiwa kwa haraka.

Natumai kuwa, kama Afisa Elimu, utaweza kuchukua hatua kuhusu suala hili ili kuhakikisha kuwa wazazi na wanajamii wanapata nafasi ya kutoa maoni na kwamba kambi hii inapitia upya ili kuhakikisha kuwa ni ya haki na inafaa kwa jamii.

Asante kwa kuzingatia masuala haya.
 
Elimu ni gharama.
Ongea na mwalimu ulipie kwa awamu tatu au nne.
Hapa suala sio gharama, tungetaka gharama tungewapeleka private schools, hapa ni suala la uwajibikaji, tumesikia serikali ikisema kila mara marufuku michango, je hnataka kusema serikali
Imeshindwa majukumu yake? Je unataka kusema bila kambi wanafunzi hawatafaulu? Je shula zote tanzania nzima zina mfumo huu? Je waalimu kufundisha ni hisani au
Jukumu lao la msingi?
 
Hizi kambi zipo kwa shule nyingi. Ilitakiwa shule ije na pwndekezo la gharama za kambi kwa wazazi alafu kwa pamoja mkubaliane kupunguza au kubaki hivyo hivyo. Kama hamkushirikishwa kwenye vikao vya shule hilo ni kosa na una haki ya kuhoji. Ila kama mlishirikishwa halafu wenzako wakakubali huna jinsi zaidi ya kuungana nao. Vinginevyo tafuta mbinu za kumtoa mwanao hapo kwa kipindi hicho bila kuathiri uhusiano mzuri kati yako na shule.
 
Hapa suala sio gharama, tungetaka gharama tungewapeleka private schools, hapa ni suala la uwajibikaji, tumesikia serikali ikisema kila mara marufuku michango, je hnataka kusema serikali
Imeshindwa majukumu yake? Je unataka kusema bila kambi wanafunzi hawatafaulu? Je shula zote tanzania nzima zina mfumo huu? Je waalimu kufundisha ni hisani au
Jukumu lao la msingi?
Mkuu; hebu tulia utuelezee japo kwa kifupi:
1, Lengo kuu la kuweka kambi ni nini?
2, Je, kuna uzoefu gani (learning experince) wowote wa matokeo ya kuweka kambi e.g. Matokeo ya mitihani yalikuwa mazuri kwa waliohudhuria kambi?
3. Ninavyofahamu Shule nyingi (kama sio zote) za day huweka vikao na wazazi/walezi na hapo wazazi/walezi huweza kutoa madukuduku yao. Lakini pia Yupo Diwani wa eneo hilo, Mkurugenzi au hata mbunge.
Kumbuka pia kwamba kama jambo hilo linafanyika kwa nia njema; baadhi ya faida ni mwanafunzi kupata muda mwingi wa kujisomea; kufanya mazoezi katika vikundi (group studies) mwl. anakuwa nao kwa muda mrefu tena wa ziada na kikubwa zaidi ni mtoto kubadilisha mazingira ya kujifunzia.
 
Natumai barua hii itakufikia salama. Mimi ni mzazi wa mwanafunzi aliye katika Kidato cha Pili katika Shule ya Sekondari Mkuu, wilayani Rombo. Nimeandika barua hii kuwasilisha maswali na malalamiko yangu kuhusu kambi inayotarajiwa kufanyika kwa wanafunzi wa Kidato cha Pili kwa gharama ya shilingi 215,000/-. Hali hii imeleta maswali mengi na wasiwasi katika familia nyingi, na kwa bahati mbaya, majaribio yangu ya kupata maelezo yanayohusiana na suala hili kutoka kwa viongozi wa shule, afisa elimu, na afisa mtendaji wa kijiji yamekosa majibu ya kuridhisha.

Haya ni maswali yangu:
1. Je, kambi hii ni lazima kwa wanafunzi? Kuna suala la kambi ya lazima, na je, mwanafunzi ambaye hatakwenda atakutana na madhara yoyote au kufukuzwa?
2. Je, gharama hii ya 215,000/- ni haki? Gharama hii ni mara tatu zaidi ya ada ya kawaida ya shule ambayo ni shilingi 79,000/-. Hii ni mzigo mzito kwa wazazi wengi, na je, hii inakubaliana na sheria au miongozo inayohusu haki za wazazi na wanafunzi?
3. Je, mwenyekiti wa bodi ya shule alikubaliana na pendekezo hili bila ushirikishwaji wa jamii? Inashangaza kwamba kambi hii ilipitishwa bila kutoa nafasi kwa wanajamii kutoa maoni yao. Wazazi wengi hawawezi kumudu gharama hii, na hii inaweza kusababisha migogoro na matatizo katika jamii, ikiwemo kuingilia mali za watu kufidia gharama hizi.
4. Je, kuna nafasi ya ushirikishwaji wa wanajamii na wazazi katika vikao vya maamuzi? Hii ni muhimu kwa ushirikishwaji wa jamii, na je, kuna uwezekano wa kutumia teknolojia kama vikundi vya WhatsApp ili kuwezesha wazazi na wanajamii kutoa maoni na kuulizwa kuhusu suala hili?

Katika juhudi yangu ya kupata majibu, nilijaribu kuwasiliana na Mkuu wa Shule, Afisa Elimu, na Afisa Mtendaji wa Kijiji, lakini walikataa kutoa maelezo na kunilazimisha nifike shuleni, licha ya kuwa mimi ni mzazi wa mtoto yatima na nipo mbali na shule. Baada ya hayo, Mkuu wa Shule, Bi. Julieth Nemes, alikata simu na kuni-block, jambo ambalo ni jambo la kushangaza na linalozua maswali kuhusu uongozi wa shule.

Ni wazi kuwa kuna hofu kubwa miongoni mwa wanakijiji kuhusu kutoa maoni kwa sababu ya hofu ya kuwa wanafunzi wao watafanyiwa visa. Hii ni hali ambayo inahitaji kushughulikiwa kwa haraka.

Natumai kuwa, kama Afisa Elimu, utaweza kuchukua hatua kuhusu suala hili ili kuhakikisha kuwa wazazi na wanajamii wanapata nafasi ya kutoa maoni na kwamba kambi hii inapitia upya ili kuhakikisha kuwa ni ya haki na inafaa kwa jamii.

Asante kwa kuzingatia masuala haya.
Shule inawatoto wangapi, na Kama shule yako ni ya kata kwa maana wanafunzi wengi wa shule hiyo ni wa kata moja. Na idadi ya wanafunzi wote ni 500, Na iwapo kata yenu yaweza kuwa na watu 5000 wabaoweza kuchangia sh 1100 kwa wiki.

Je pesa munayochangishwa nu ya chakula au ya mambo gn.

Iwapo ni kwa ajili ya chakula,
Nijulishe.

Ni jukumu la wananchi kuchangia kwa kuwa wenye mamlaka pamoja na kuwa tunalipa kodi lakini wameshindwa kudeliver huduma zote za jamii nchini.

Temgeneza kamati inayohusu viongozi wa dini zote. Tutawapa wenye kukubali kutoa sadaka ya sh 1000 kila wiki ili kuwezesha watoto wote wa sekondari kulata mlo. Achili rambaldi kidato cha pili.
 
Hapa suala sio gharama, tungetaka gharama tungewapeleka private schools, hapa ni suala la uwajibikaji, tumesikia serikali ikisema kila mara marufuku michango, je hnataka kusema serikali
Imeshindwa majukumu yake? Je unataka kusema bila kambi wanafunzi hawatafaulu? Je shula zote tanzania nzima zina mfumo huu? Je waalimu kufundisha ni hisani au
Jukumu lao la msingi?
Achana na hizo story za viongozi wa serikali. Watoto wao wamewapeleka shule za mamilioni.hapo halmashauri watoto wao wanasoma ubentu Mawenzi Secondary ada million na laki sita,wengine wako shauri Tanga.
Hakuna elimu ya bure ilikufaga na MAGU.toa hela mtoto apate muda wa kucover syllabus mapema.kwenye elimu hakuna siasa. Elimu ya bure ni ya madrasa na sunday school. Watoto wa meigulu wanasoma shule ya million 10, watoto wa mkenda wanasoma shule za mamilioni.
 
Hapa suala sio gharama, tungetaka gharama tungewapeleka private schools, hapa ni suala la uwajibikaji, tumesikia serikali ikisema kila mara marufuku michango, je hnataka kusema serikali
Imeshindwa majukumu yake? Je unataka kusema bila kambi wanafunzi hawatafaulu? Je shula zote tanzania nzima zina mfumo huu? Je waalimu kufundisha ni hisani au
Jukumu lao la msingi?
Walimu hawatoshi wanaoletwa na serikali. Kinachofanywa na mwalimu mkuu wa mkuu sec ni kuajiri walimu wa kujitolea. Hao walimu walipwe na nani kama siyo wazazi?
Ukiendekeza ubinafsi kwenye elimu ya mtoto unamharibia tu future yake. Elimu ni gharama sana hata walimu wa Government watoto wao wanawapeleeka private school.kwa sababu ya uchache wa motisha.
 
Mkuu; hebu tulia utuelezee japo kwa kifupi:
1, Lengo kuu la kuweka kambi ni nini?
2, Je, kuna uzoefu gani (learning experince) wowote wa matokeo ya kuweka kambi e.g. Matokeo ya mitihani yalikuwa mazuri kwa waliohudhuria kambi?
3. Ninavyofahamu Shule nyingi (kama sio zote) za day huweka vikao na wazazi/walezi na hapo wazazi/walezi huweza kutoa madukuduku yao. Lakini pia Yupo Diwani wa eneo hilo, Mkurugenzi au hata mbunge.
Kumbuka pia kwamba kama jambo hilo linafanyika kwa nia njema; baadhi ya faida ni mwanafunzi kupata muda mwingi wa kujisomea; kufanya mazoezi katika vikundi (group studies) mwl. anakuwa nao kwa muda mrefu tena wa ziada na kikubwa zaidi ni mtoto kubadilisha mazingira ya kujifunzia.
Kwahiyo walimu hawawezi kufundisha topics zote ndani ya muda uliopangwa na serikali?

Hivi elimu ni vita enhe? Yaani mtoto hana muda wa kujumuika na wazazi wake akapata kujifunza na stadi za maisha ambazo mzazi ana wajibu huo wa malezi?

Yaani walimu wana njaa hadi inaleta kinyaa.

Hayo maisha magumu wanayopitia walimu tena wakiwa na mshahara, basi wafahamu kwamba wazazi wengi hawana vyanzo vya mapato vya kueleweka hivyo kuwabebesha gharama za ziada ni kumwangushia shida zako.
 
Wewe sema tu huna Cha kutoa, ila suala la mikakati ya kuwafaulisha watoto ipo shule nyingi. Elimu ni gharama Bwashee
 
Elimu ni burudani ya akili Kama mpira na/au challenge yoyote ambayo akili itahitaji kutoa temporary solution, sio kitu Cha kukomaa nacho... watoto wangu hawaendi tuition jumamosi... mitihani ya jumamosi Wala kambi na wanafaulu kwa Kiwango Cha 75+ percentile hiyo inatosha kwangu.
 
Kwahiyo walimu hawawezi kufundisha topics zote ndani ya muda uliopangwa na serikali?

Hivi elimu ni vita enhe? Yaani mtoto hana muda wa kujumuika na wazazi wake akapata kujifunza na stadi za maisha ambazo mzazi ana wajibu huo wa malezi?

Yaani walimu wana njaa hadi inaleta kinyaa.

Hayo maisha magumu wanayopitia walimu tena wakiwa na mshahara, basi wafahamu kwamba wazazi wengi hawana vyanzo vya mapato vya kueleweka hivyo kuwabebesha gharama za ziada ni kumwangushia shida zako.
Hakuna uwezekano wa mwalimu kumaliza syllabus ndani ya mwaka mmoja kama iddi ya walimu haitoshi.
Ili shule ifanye vizuri inatakiwa mwezi wa sita wacover syllabus then waanze review na kupitia mitihani ya kutosha.
 
Back
Top Bottom