Kamisaa kashtuka sana Namungo kukosa penati

Mimi mwanayanga. Penalty hatujaonewa kabisa.. ni clear penalty maana bakari hakugusa mpira kabisa ila aliugusa mguu wa kichuya na kumuangusha...

Timu yetu mbovu safu ya ushambuliaji..

Sarpong anatumia nguvu kuliko akili... natamani hata molinga angekuwepo..

Carinho, feisal wanalazimika kupiga mashuti na kwenda kutafuta magoli mbele maana sarpong hafungiii magoli na hajui kujiposition kama mshambuliaji

Natamani ntibanzonkinza aje haraka
 
Tatizo utopolo wengi ni mateja.

Mwamuzi kawabeba sana jana la sivyo wangeshapigwa zaidi ya mbili,ila cha ajabu mateja wanavyolalamika,utashangaa hadi msemaji wao atawaunga mkono
Nimeona video ya mashabiki wa Yanga wakilalamika waamuzi kusikitika namungo kukosa penati ,hii imekaaje au walijua kinachojiri .mhh haya twendeni tutajafika tu
 
Kiukweli nyinyi mashabiki wa utopolo ni tofauti sana na mashabiki wa Mtibwa , Prison , Simba n.k na hapo ndio mnathibitisha yale maneno ya kocha wenu luc.

Mashabiki wa hizo timu nilizotaja pindi timu zao zinapopoteza mechi au kutoa draw huwa wanajikita kuchambua timu zao kuwa zimecheza chini ya kiwango na kulaumu benchi la ufundi kitu ambacho kinaleta faida kwa timu.

Sasa nyinyi badala hata ya kuongelea bao la kwanza la namungo jinsi beki zenu zilivyogeuzwa kiutopolo ili zijirekebishe, mnatafuta sababu kwamba ilipangwa mfungwe.

Ile ni clear penat na Kama umeangalia mechi yanga ndio walibebwa maana hata goli lenu mlifunga namungo wakiwa pungufu kwa mchezaji mmoja kukataliwa kuingia kwa muda mrefu mpaka mkafunga goli.
 
Mkuu ni kweli endapo Charles Edward Manyama angekuwepo uwanjani lile goli lisingefungwa. Ukiangalia hata ile krosi ilitokea upande wa kushoto ambapo yeye alikuwa yupo nje
 
Mkuu ni kweli endapo Charles Edward Manyama angekuwepo uwanjani lile goli lisingefungwa. Ukiangalia hata ile krosi ilitokea upande wa kushoto ambapo yeye alikuwa yupo nje
Mchezaji hawezi ruhusiwa kurudi uwanjani wakati mpira unaendelea hadi usimame,
 
Ingekuwa manguruwe, leo hii Haji angebeba screen kuonyesha kwamba Bakari Nondo hakumgusa tapeli Kichuya.

La pili, waamuzi walikuwa na "mzigo" wangefanikisha Yanga kufungwa. Ule mshangao wa kukosa hela.
Hili la mzigo mbona wazi kabisa
 
hii ndio maana halisi ya utopolo. nimeongea na mwamuzi anasema alikuwa anajutia makosa ya refa wake. kipa alitoka kabla ya penati kupigwa
Pia, kuna mchezaji mmoja wa Yanga, aliingia ndani kabla ya hiyo penati kupigwa. Bila hata ya kosa la kipa kutoka golini kabla ya kupigwa hiyo penati, hilo kosa la huyo mchezaji, lilistahili kufanya hiyo penati irudiwe!
 
Nikajua peke yangu nililiona ilo, nilishangazwa na refa kutomruhusu muda wote ule
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…