Mabibi na mabwana heshima kwenu na moja kwa moja kwenye mada.
Malengo ya kampeni ni kuonyesha kwa nini mgombea mmoja anafaa kuliko mwingine. Kujinadi kwa wapiga kura na hata kupigana madongo kwa wagombea ndiyo sehemu ya mchezo wenyewe.
Wagombea wote ni shuruti wawe katika uwanja sawa ili mwananchi ajichagulie mwenyewe anayemtaka bila ya shinikizo lolote.
Mlaji katika biashara hii ni mwananchi. Mwananchi ana nia ya dhati kabisa ya kujua kwa nini huyu wala siyo yule.
Mamlaka yoyote inapoingilia kati kumbeba mgombea mmoja kwa mbeleko dhidi ya wengine si sawa. Kimsingi ni kuwanyima wananchi kwa makusudi fursa yao ya kuwachagua wenye hoja na wanaowataka.
Tume ya uchaguzi - rudisheni wagombea wote walioenguliwa kwa visababu visivyo na mashiko. Visababu vya kiuhakiki ambapo nyie wenyewe mlikuwa na wajibu wa kuvitolea maelekezo visiendekezwe. Wapeni watu haki zao za kutumia sanduku la kura kufanya maamuzi yao.
Vipi kukiukwa kwa haki za wagombea kutokana na vikwazo mbalimbali visivyo kuwa na vichwa wala miguu tokea mamlaka zingine? Vipi kanuni na lugha za kienyeji kutumika majukwaani? Vipi matumizi ya pesa kununua wasanii na hata wagombea?
Polisi - hadi sasa tukiacha dosari kidogo kidogo mmejitahidi. Yale mambo ya kuwakamata baadhi ya wagombea ili wasirudishe fomu zao kwa wakati hatukuyapenda.
Tunaamini tume itatumia busara kuwarejesha wagombea wote waliokwamishwa na kadhia zisizokuwa na sababu pamoja na hizi za tokea kwa baadhi ya polisi wasiokuwa na kutambua umuhimu wa haki za watu.
Vyombo vya habari - kwa hofu zenu, kununuliwa kwenu, kujipendekeza kwenu nk, mmewanyima wananchi kuwasikia wagombea wakijinadi. Nyie hamna dhamana ya kuwaamulia watu wasikie au wasisikie nini. Si sahihi kwenu kuwanyima watu fursa ya kuwasikia wagombea katika kampeni zao.
Mamlaka zote, TCRA, TCAA, mahakama nk, ni muhimu mno mkajitathimni. Hii kushindana kwa mamlaka kumfurahisha mgombea fulani haitutendei haki sisi wananchi. Historia ni shuhuda mzuri na kila mtu ataubeba mzigo wake mwenyewe.
Kwani wagombea hawajui wananchi wanahitaji nini kiasi cha kuingiliwa kwa mchakato huu na mamlaka hizi?
Wagombea wote ni watanzania wenye haki sawa za kukamata uongozi wa juu wa nchi hii. Ubaguzi huu wa nini basi?
Tunahitaji wagombea wakidhi mahitaji yetu ya msingi tunayotarajia kwao. Kama hilo halipo, mengine yanabakia kuwa upuuzi mtupu kama huu wa kulazimishana na ahadi zenye mielekeo ya rushwa zaidi.
Mamlaka na zikatambue, haki na uhuru wetu katika zoezi zima la kampeni ni lazima kuheshimiwa.
Malengo ya kampeni ni kuonyesha kwa nini mgombea mmoja anafaa kuliko mwingine. Kujinadi kwa wapiga kura na hata kupigana madongo kwa wagombea ndiyo sehemu ya mchezo wenyewe.
Wagombea wote ni shuruti wawe katika uwanja sawa ili mwananchi ajichagulie mwenyewe anayemtaka bila ya shinikizo lolote.
Mlaji katika biashara hii ni mwananchi. Mwananchi ana nia ya dhati kabisa ya kujua kwa nini huyu wala siyo yule.
Mamlaka yoyote inapoingilia kati kumbeba mgombea mmoja kwa mbeleko dhidi ya wengine si sawa. Kimsingi ni kuwanyima wananchi kwa makusudi fursa yao ya kuwachagua wenye hoja na wanaowataka.
Tume ya uchaguzi - rudisheni wagombea wote walioenguliwa kwa visababu visivyo na mashiko. Visababu vya kiuhakiki ambapo nyie wenyewe mlikuwa na wajibu wa kuvitolea maelekezo visiendekezwe. Wapeni watu haki zao za kutumia sanduku la kura kufanya maamuzi yao.
Vipi kukiukwa kwa haki za wagombea kutokana na vikwazo mbalimbali visivyo kuwa na vichwa wala miguu tokea mamlaka zingine? Vipi kanuni na lugha za kienyeji kutumika majukwaani? Vipi matumizi ya pesa kununua wasanii na hata wagombea?
Polisi - hadi sasa tukiacha dosari kidogo kidogo mmejitahidi. Yale mambo ya kuwakamata baadhi ya wagombea ili wasirudishe fomu zao kwa wakati hatukuyapenda.
Tunaamini tume itatumia busara kuwarejesha wagombea wote waliokwamishwa na kadhia zisizokuwa na sababu pamoja na hizi za tokea kwa baadhi ya polisi wasiokuwa na kutambua umuhimu wa haki za watu.
Vyombo vya habari - kwa hofu zenu, kununuliwa kwenu, kujipendekeza kwenu nk, mmewanyima wananchi kuwasikia wagombea wakijinadi. Nyie hamna dhamana ya kuwaamulia watu wasikie au wasisikie nini. Si sahihi kwenu kuwanyima watu fursa ya kuwasikia wagombea katika kampeni zao.
Mamlaka zote, TCRA, TCAA, mahakama nk, ni muhimu mno mkajitathimni. Hii kushindana kwa mamlaka kumfurahisha mgombea fulani haitutendei haki sisi wananchi. Historia ni shuhuda mzuri na kila mtu ataubeba mzigo wake mwenyewe.
Kwani wagombea hawajui wananchi wanahitaji nini kiasi cha kuingiliwa kwa mchakato huu na mamlaka hizi?
Wagombea wote ni watanzania wenye haki sawa za kukamata uongozi wa juu wa nchi hii. Ubaguzi huu wa nini basi?
Tunahitaji wagombea wakidhi mahitaji yetu ya msingi tunayotarajia kwao. Kama hilo halipo, mengine yanabakia kuwa upuuzi mtupu kama huu wa kulazimishana na ahadi zenye mielekeo ya rushwa zaidi.
Mamlaka na zikatambue, haki na uhuru wetu katika zoezi zima la kampeni ni lazima kuheshimiwa.