Mkoa wa Mwanza unatarajia kuzindua Kampeni ya Msaada wa Kisheria ya Mama Samia itakayodumu kwa muda wa siku 10 kutoka Februari 18 hadi 27 mwaka huu katika Uwanja wa Furahisha jijini Mwanza.
Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Said Mtanda amesema mara baada ya kuzinduliwa, msaada wa kisheria unatarajia kuendelea katika wilaya zote nane za mkoa huo.
Mtanda amewataka wananchi kujitokeza kwa wingi katika uzinduzi wa kampeni hiyo huku akiwataka wananchi wenye changamoto za kisheria kufuatilia ratiba katika wilaya zao kujua maeneo ambayo msaada wa kisheria utakuwa unatolewa.