Uchaguzi 2020 Kampeni za Tanzania: Badala ya Mgombea kuulizwa maswali, yeye ndiye anawauliza maswali Wananchi

Uchaguzi 2020 Kampeni za Tanzania: Badala ya Mgombea kuulizwa maswali, yeye ndiye anawauliza maswali Wananchi

CalvinKimaro

JF-Expert Member
Joined
Sep 11, 2017
Posts
245
Reaction score
314
Ni bahati mbaya mikutano ya CHADEMA na ACT wanaoulizwa maswali ni Wananchi waliokuja kuwasikiliza badala ya wananchi kuwauliza wao maswali. Kwa kuwa siku bado ningefurahi kama kuna atakayewauliza wagombea wakuu wa CHADEMA na ACT haya maswali yangu. Au tufanye mdahalo nao? Maswali yangu ni haya:

1. Nini msimamo wa CHADEMA kuhusu ushoga? Ni kweli wakipata nafasi watabadili sheria ili kila mtu awe na haki ya kutumia mwili wake atakavyo? Ni kweli ushoga ni moja ya haki za binadamu?

2. CHADEMA na ACT watuambie ni kweli wakipata nafasi wataacha kutuletea vitu na badala yake watatuletea nini?

3. CHADEMA na ACT watuambie kwa kuwa wanadai serikali imefanya makosa kuleta vitu wakipata nafasi wataving'oa au kuviharibu vitu?

4. ACT watuambie ni kweli wakipata nafasi wataruhusu wanafunzi wajawazito wachanganyike na wasio wajawazito darasa na bweni moja?

5. ACT na CHADEMA watueleze watazifanyeje ndege za ATCL? Wataziuza? Watazikodisha? Wataacha zioze? Hawatanunua tena ndege wakipata nafasi? Taifa litakuwa halina shirika la ndege chini ya utawala wao?

6. CHADEMA, ACT, CUF, NCCR watueleze watakavyounda tume mpya ya uchaguzi ambayo kwa mtazamo wao itakuwa huru 100%? Nani watakuwa wajumbe na watapatikanaje?

7. Kwa kuwa Bwawa la Nyerere (Stieglers) ni la umuhimu wa kipekee kwa Taifa na Kwa kuwa wao wanalipinga je wakishika madaraka watalivunja? Wataacha lioze?

8. CHADEMA watuthibitishie utawala wa majimbo ni suala lipo kwenye sera yao? Watagawaje hayo majimbo? Wataweka tahadhari zipi ili tusitumbukie kwenye ukabila au baadhi ya maeneo kuachwa nyuma kimaendeleo? Wataweka tahadhari zipi ili tusitumbukie kwenye mifarakano kama Nigeria?

9. Kwa kuwa CHADEMA wamediriki kufukuza chombo cha habari ambacho kwa maoni yao kilikuwa hakiwafurahisi watueleze ikiwa watapata madaraka vyombo ambavyo havitawafurahisha vitalindwa kivipi?

10. CHADEMA na ACT watueleze msimamo wao kuhusu muungano kwa kuwa wagombea wao wamejikita katika kuupinga muungano. Je muungano utakuwa salama chini ya utawala wao? Watafanya nini usivunjike?

Ikiwa watashindwa kujibu au kufafanua tumia kura yako kwa busara tarehe 28/10.
 
Mfano wa maswali

1. Mtaichagua ccm?.....wananchi hapanaaaa!!

2. CCM ni mafisadi? ......wananchi ndiooo

3. CCM imeharibu na kuchezea katiba?.......wananchi ndiooo

4. Mtamchagua Magufuli? ..... wananchi hatumtaki

5. Ndege za magfuli zina faida au hasara? .....wananchi zina hasara tupu.

Naomba tuendele na kampeni za maswali hivi hivi.


Mtakoma mwaka huu.
 
Yaani ulichoandika hapa ni Kimagufuli magufuli!

Eti "msichague upinzani maana watabomoa madaraja na kuharibu ndege!"

Wewe naye umebeba hivyo hivyo ukaleta hapa!Akili zenu tunawaambia mmebakiza za kuvukia barabara tu!Shame!
 
Maswali yote ni valid na muhimu! Ninasubiri majibu yasiyo ya ubabaishaji hapa.
 
Yaani ulichoandika hapa n....!
Eti "msichague upinzani maana watabomoa madaraja na kuharibu ndege!"
Wewe naye umebeba hivyo hivyo ukaleta hapa!Akili zenu tunawaambia mmebakiza za kuvukia barabara....
Leta majibu ya maswali hapa, acha ya "tatarika ya bisi kwenye kikaangio"
 
Magufuli aulizwe maswali haya:
1. Kwann anateka watu?
2. Kwann anauwa watu?
3. Kwann anapora fedha za wafanyabiashara?
 
Kama haya ndo maswali ya kuuliza kuna mawili unapofushwa na uchama au uwezo wa kuelewa ndo umepungua ndugu na kama huna majibu ya haya maswali kuna mtoto wa darasa la saba B niko nae nitamwambia akujibu
 
Kama haya ndo maswali ya kuuliza kuna mawili unapofushwa na uchama au uwezo wa kuelewa ndo umepungua ndugu na kama huna majibu ya haya maswali kuna mtoto wa darasa la saba B niko nae nitamwambia akujibu
Ninachojua Ni kwamba jamaa anataka msimamo wa hivyo vyama kuhusu hayo maswal yake.
 
Bila kuiba mwaka huu ni ngumu sana ...washauri wake aliowakumbatia walimdanganya hakuna hata haja ya kampeni anapita tu anapungia anashinda imekuwa tofauti.....ndio maana hakuna uchaguzi tangu tuingie vyama vingi ccm imfanya maandalizi mabovu ya ndani kama huuu , walijua watapitisha wabunge bila kupingwa wamekutana na upinzani mkali imebidi wasimamishe ......, wana ccm mashinani hawajapelekewa vifaa wale pesa za kampeni .....pesa zote amehodhi yeye , kibaya ni kuwa kutokana na mapendekezo ya Bashiru hata pesa za miradi midogo midogo zote wamechukua na wanashindwa kuwaletea huku chini pesa za kampeni ...

Maandalizi upande wa vyombo vya dola ni hatari zaidi , huu ni uchaguzi pekee hadi sasa huoni Polisi kuwa na magari mapya na vifaaa kama huko zamani , acha zile posho zao za uchaguzi ....hata bendera ziko moja moja ..maana fuko la pesa za kampeni za ccm anadhibiti mdogo wake kabisa pamoja na mtoto wake .

Ni kuomba Mungu tu watu wasiingie barabarani kwani hivyo vifaa vya kudhibiti vurugu na hata morali haipo kwa askari ....usishangae wakizidiwa wakavua uniforms!

Kuna hoja nyepesi kama vitambulisho vya wamashinga zinaibua maswali kwakua hapakuwa na risiti zilizotolewa na haijulikani pesa zimeenda wapi.

KUNA ZILE PESA ZA DPP ZINAZOITWA ZA MAFISADI WALIKUWA WANALIPISHWA ONLY IN CASH .....NA MWISHONI LAPTOPS ZIKAIBIWA NA VIDEO ZILI LEAK ....NASHANGAA HADI SASA LISSU HAJAMPIGA KWENYE HILI MAANA NALO NI BOMU LA NYUKLIA.

PESA TASLIMU ALIZOKUWA AKIPOKEA DPP MAGANGA ALIKUWA ANAMPA NANI ...KWANINI HAZIKUWA ZINAENDA BANK? NA BAADA YA WATU KULALAMIKA NANI WALE WALIENDA KUIBA LAPTOPS KUFICHA USHAHIDI?
 
Hakuna atakayeweza kujibu hayo maswali vizuri humu jukwaani wala uko uraiani ,jazba ndo zimetawala tu
 
Hakuna atakayeweza kujibu hayo maswali vizuri humu jukwaani wala uko uraiani ,jazba ndo zimetawala tu

Mtoa mada ana iwaza Sana Chadema... Achuke kadi na yy awe mwanachama.

Pia angeongelea ilani na sera za CCM sio Kuandika upuuzi..
 
Nimekakuta sehemu
Screenshot_20200923-103547.jpg
 
Back
Top Bottom