KAMPUNI HUDUMA ZA SIMU SASA ZINAIBIA WATUMIAJI/wateja

KAMPUNI HUDUMA ZA SIMU SASA ZINAIBIA WATUMIAJI/wateja

enk

Member
Joined
Jan 11, 2012
Posts
87
Reaction score
12
Ndg Wananchi wenzangu tuweni makini na watoa huduma za mawasiliano hasa hawa wa simu za mkononi ukitoa TTCL
Nasikitika sana kusema hili maana sijui ni wangapi wameshaibiwa na malampuni haya ambayo hayaishi kila mara kutangaza promotion hii mara ile na mengine kuthubutu kutaja viwango vya kupiga simu kwa muda fulani.
Mimi ni mtumiaji wa simu nikiwa nimejiunga na na mojawapo ya Kampuni inayotoa huduma hii na iliyokwisha badilisha majina yake mara tatu sasa na wao kujisema kuwa wanatoa huduma kwa thumuni na baadae robo SHILINGI Thubutu! Ukipiga tu wanakukata 100 SHILINGI NA HIYO HAINA DAKIKA YA KWANZA AMA YA NANE NI FLAT RATE "HUU NI WIZI" watanzania wenzangu angalia salio kabla ya kupiga simu PILI simu nyingi sasa zinaonyesha muda uliotumia baada ya kukata simu linganisha na maneno yao wanayotangaza utaona maajabu kama kuna mhusika hapa jamvini apeleke habari hii ofisini kwao kuwa tumeshitukia na hili litafanyiwa kazi kwa kujitolea hadi kieleweke TUMECHOKA.
 
Wengine tushaamua kuacha kupga simu.
Hilo swala sio kwamba hawalijui, ni wizi tu. Kwa sasa jitahidi kupunguza kupiga simu zisizo na muhimu kupunguza gharama.
 
Back
Top Bottom