Tetesi: kampuni la kuchimba madini lasitisha rasmi kupitisha mizigo yake bandari ya dar es salaam?

Tetesi: kampuni la kuchimba madini lasitisha rasmi kupitisha mizigo yake bandari ya dar es salaam?

taarifa za uhakika zinasema kampuni la kuchimba madini Glencore linajipanga kuachana na biashara ya kupitisha mizigo yake Tanzania kutokana kile kinachosemwa kuwa ni figisu-figisu za kodi zisizoeleweka. mizigo yake sasa itapita Durban kwa Madiba. hii ina maana Tanzania itapoteza mapato iliyokuwa ikipata kutoka katika mzigo wa madini ya shaba ya tani 20,000 kila mwezi yaliyokuwa yakipita bandari ya salama kwenda ughaibuni. Tusisahau tena kuwa vijana wetu kwa mamia watapoteza ajira. pia vikampuni vidogodogo vitajiuliza 'ikiwa mwenye tani elf 20 kwa mwezi anasepa sisi wa tani 1000, 2000, 3000 tunabaki kufanya nini?'

hatari ni aje?

Kodi imepanda au walikuwa wakikwepa, waende zao tu, sasaivi tumejipanga!
 
Ni kweli,tutaanza kutumia vyanzo vipya vilivyopendekezwa na wabunge "makini" wa ccm,sasa tutaanza kutoza kodi za kuku,mbuzi,bata,paka,panya,mbwa,kunguni,viroboto,chawa na kila mdudu atambaaye chini ya nchi,lengo likiwa ni kufikia kwa haraka Tanzania ya viwanda.
Wabunge wa chadema wamechoka washabiki wamechoka. Huu mchango wako kama vile wewe naye ni mteja wa milembe vile
 
Hao njia za mikato zilizozibwa ndio zinawakimbiza, na waende salama.
 
Kwa mnaosema waende hamjui uchumi wa copper na faida kwetu, iko hivi tonne 20,000 kwa mwezi kwa wastani wa 26 tonnes ni truck 25 per day! Sasa iko hivi 90% ya copper hubebwa na magari ya ki tz! Ina maana truck zetu zitakosa mzigo! Zitarud tupu! Maana kama huo mgodi wanapeleka mizigo Durban hakuna gari ya tz inaweza kwenda huko maana wa south Africans wana magari ya kujitosheleza! Ina maana kwa siku trucks 22 zinakosa kazi! Pia copper husindikizwa na wa kampuni za ki tz kwa ajili ya security one truck one security guard it means another 22 people per day! Acha ma agent mama ntilie etc! Je hizo kodi walizoongeza zina justify hizi ajira zote zilizopotea na mapato!
 
kwa jicho la mahaba ya uchama huwezi kuona athari zake sasa. hakuna ubunifu katika vyanzo vya kodi na viwango vyake. kuna nyingi ziko duplicated tena katika viwango ambavyo ukitajiwa unakuwa kichaa yaani ni kama vya kukomoana
 
Back
Top Bottom