Kampuni ya basi la Shabiby, hii ni hatari sana kwa abiria wenu

Kampuni ya basi la Shabiby, hii ni hatari sana kwa abiria wenu

Ndani ya basi wanatakiwa kuingia abiria tu waliokata tiketi na wafanyakazi wa basi tu sio mtu mwingine

waliokukumna na kukuvuta miguu wamekuhurumia walitakiwa wakutandike mangumi na makofi juu

Ungempigia simu mkeo ashuke achukue hivyo vipesa vyako koko chini sio wewe upande basi

Ukome kabisa tabia hito ya kupanda ndani ya basi wakati wewe sio abiria
[emoji23][emoji23][emoji23]
 
Kama yalivyo mawazo ya baadhi ya wadau, naona huu mgogoro na huyo dereva uliununua mwenyewe! Sijaona sababu ya wewe kuingia kwenye basi ambalo liko tayari kwa safari na maspika yanayo ashiria wewe ni mmachinga!

Wakati mwingine, ni vizuri tu ukaheshimu taratibu zao. Na kama umekasirika sana kwa kudhalilishwa mbele ya mke wako, basi hamia kampuni nyingine! Panda Machame Inv. Nayo yako kama Shabiby tu kwa ubora, nk.
 
Hii comment ndio final say.
Kama yalivyo mawazo ya baadhi ya wadau, naona huu mgogoro na huyo dereva uliununua mwenyewe!
Sijaona sababu ya wewe kuingia kwenye basi ambalo liko tayari kwa safari na maspika yanayo ashiria wewe ni mmachinga!

Wakati mwingine, ni vizuri tu ukaheshimu taratibu zao. Na kama umekasirika sana kwa kudhalilishwa mbele ya mke wako, basi hamia kampuni nyingine! Panda Machame Inv. Nayo yako kama Shabiby tu kwa ubora, nk.
Kule machame ndio watakubali?
 
Hiyo spika ilikuwa kubwa kiasi gani mpaka Dereva akutoe Kwa nguvu?

Wakati wa Vurugu mkeo kwanini hakuwajuza kuwa ni mtu wake kweli?

Na alipokueleza utoke kwanini hukumwita Mkeo afuate Pesa nje?

Inaonekana hao watu walikosa uvumilivu ila na wewe ulikosa utulivu wa akili pia. Hili suala halikupaswa kufikia kukamatana mashati kama nyote mngetumia busara
 
Kuna wapuuzi wanasema mleta uzi ana kosa.

Wajinga sana.

Hata kama ni muuza vitu kuna namna ya kumkataza mtu kitu na mkaachana kwa heshima tu.

Ila mleta uzi inaonyesha ulijibu kwa ubabe kwasababu mtu akikukataza kitu na jibu lako likawa kumuelewesha unachofanya sicho anachofikiria hakuna namna huyo mtu atakukunja. Labda akwambie mpe kwa dirishani.

Labda uelezee kabla hajakukunja ulimjibu nini? Haukumuambia kwamba mshahara wake unamlipa ndani ya siku na taa ya gari lako inaweza kumlisha yeye na ukoo wake?
 
Kuna wapuuzi wanasema mleta uzi ana kosa.

Wajinga sana.

Hata kama ni muuza vitu kuna namna ya kumkataza mtu kitu na mkaachana kwa heshima tu.

Ila mleta uzi inaonyesha ulijibu kwa ubabe kwasababu mtu akikukataza kitu na jibu lako likawa kumuelewesha unachofanya sicho anachofikiria hakuna namna huyo mtu atakukunja. Labda akwambie mpe kwa dirishani.

Labda uelezee kabla hajakukunja ulimjibu nini? Haukumuambia kwamba mshahara wake unamlipa ndani ya siku na taa ya gari lako inaweza kumlisha yeye na ukoo wake?
Mbele ya mke wake lazima avimbe. Ndio kumemponza huko mpaka kufukuzwa kama kibaka
 
Hizi ni hasira za kudhibitiwa....
lkn kwanini upande na spika sijui maiki kwenye gari ya watu ya biashara.....
 
Ndani ya basi wanatakiwa kuingia abiria tu waliokata tiketi na wafanyakazi wa basi tu sio mtu mwingine

Waliokukunja na kukuvuta miguu wamekuhurumia walitakiwa wakutandike mangumi na makofi juu

Ungempigia simu mkeo ashuke achukue hivyo vipesa vyako koko chini sio wewe upande basi

Ukome kabisa tabia hiyo ya kupanda ndani ya basi wakati wewe sio abiria
madhara ya chanjo yameanza mapema
 
Pole mkuu Ila binafsi sipendi mabasi yanayoruhusu hovyo wamachinga na watu ambao sio abiria, inawezekana hukuwa na Nia ya kufanya biashara Ila Kuna kitu hujaweka wazi. Kwa hili shabiby wasilaumiwe saana
 
Nimekuwa mpenzi wa kutumia usafiri wa basi la Shabiby mimi na familia yangu kwa miaka zaidi ya mitano

Dar, Dodoma, Dodoma Arusha.

Ila leo kwa yaliyo nikuta kupitia dereva huyu, imeniuma sana

Tulikata tiketi siti namba 4 kwa ajili ya mke wangu kusafiri toka Arusha kuelekea Dodoma ni katika basi linalo wasili Arusha saa nne asubuhi ili kuelekea Dodoma.

Katika pilikapilika za safari nikajikuta nimesahau kadi yangu ya benki ambayo nilidhamiria kuitumia kutoa pesa ili kumpa mke wangu pesa ya matumizi njiani na hii ndio ikawa sababu kwa mimi kukutana na maumivu niliyoyapata kwa dereva nisiye mfahamu jina lake ila ndiye dereva wa basi tulilo kata tiketi hii,yaani basi la Shabiby.

Kutokana na kusahau kadi ya benki nililazimika kumuacha ndani ya gari mke wangu ambaye nilikuwa nikimsindikiza kutafuta namna nyingine ya kupata pesa ili nimpe ya kula njiani,

Baada ya kufanikiwa nikarejea ndani ya gari, kwa lengo la kumpa hiyo pesa mke wangu,ndipo dereva huyu wa shabiby baada ya kuona kuwa mkononi mwangu nimeshika speaker ndogo ambayo huwa naitumia kwa ujasiliamali ,yeye akahisi labda naingia kuuza bidhaa fulani

Hata hivyo kwa upole nilimweleza kuwa, mimi siingi kuuza ila lengo langu ni kumpa mke wangu pesa ya matumizi njiani.

Kilicho niumiza, bado aliendelea kuni zuia kibabe

Hakuishia hapo tu alinikunja huku kondakta wake akinivuta mguu kwa nje,mbele za mke wangu,abiria na watu wengine,kiukweli nimedhslilishwa,naamini kosa langu ni kuutumia usafiri wa shabiby kumsafirisha mke wangu,halafu kuamua kumletea pesa ya matumizi mke wangu.

Kweli nimejaribu kumwelezea mtu niliye fahamishwa kuwa ni kiongozi wake hata sijaridhishwa na namna alivyoshughulikia kudhalilishwa kwangu,kiukweli nimeamua,maana mimi huwa hakuna aina ya biashara mbayo huwa naifanya ndani ya mabasi,zaidi ya leo kumsindikiza mke wangu.

Kweli,kama kampuni ya mabasi ya shabiby haita muwajibisha huyu,aliye nikunja hata kunitishia kunipiga,kisa,nimemweleza kuwa nampa mke wangu pesa ya matumizi njiani, basi kwa mimi binafsi na familia yangu nitafikiria kuto penda kuutukimia usafiri huu kwa mara nyingine,maana nimeaibishwa sana.

Nimejaribu kutafuta mawasiliano ya kampuni ya basi la shabiby makao makuu ili kutoa taarifa ya kero hii, ila sijatambua namna ya kuwapata,ndio maana nimeandika hapa ili wahusika wapatapo ujumbe angalau walishughulikie hili kama wana upendo na wateja wao,tafadhali wasilifumbie macho

Muda huu basi hilo bado lipo njiani kuelekea dodoma, mke wangu niliye msafirisha anaitwa Silvero Mwacha ,yupo sit namba 4, tafadhali wahusika popote mlipo nimekereka, naomba msilifumbie macho hili.

Ni mimi Emmamuel.
Nyuma ya basi huwa kuna namba

Sent from my SM-N960F using JamiiForums mobile app
 
Unalalamika sana, kwanini huyo mkeo hakukutetea au kufata hela huko chini?
Naamini ulitangaza humo ndani
 
Back
Top Bottom